uelekea Uzinduzi wa Jezi Mpya za Simba kwa Msimu ujao wa 2023/24 Tumezungumza na Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC Ahmed Ally na kutufahamisha shuhuli nzima itakavyokuwa siku ya Kesho Julai 19 wakati wa kukipandisha kibegi cha Jezi Mpya Juu ya Mlima Kilimanjaro
Rasmi Fabrice Luamba Ngoma ni Nyota wa Simba SC baada ya kusaini Kandarasi ya Miaka Miwili na Wekundu wa Msimbazi Simba SC. Tumezungumza na Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ally kuhusu Usajili huo kuanzia Mchakato wa kumapata na Kandarasi husika. Kuhusu Nyota wapya kuingia Kambini Nchini Uturuki Ahmed ametaja Tarehe husika ya Nyota hao kuanza Safari. Maswali kuhusu kuangwa kwa Jonas Mkude Siku ya Simba Day pia yamejibiwa hapa na Ahmed Ally. Kuhusu Chama Ahmed amewatoa hofu wana Simba pasina kusahau Kijembe kwa Watani zake kuhusu Fiston Mayele kuondoka Yanga.
Baada ya miaka 13 ya kuwatumikia Simba Sc Jonas Mkude rasmi ametaganzwa na Young Africans kuwa Nyota wao mpya. Mwamba wa umalila Baraka Mpenja ametupa uzoefu wake juu ya Jonas Mkude, nafasi ya ushindani kwenye Kikosi cha Yanga je ataweza kuingia kwenye Kikosi? Baraka ameeleza moja ya tukio kubwa ambalo hatolisahau kumhusu Mkude na Mechi ambayo Jonas alicheza kwa Kiwango kikubwa huku Baraka Mpenja akiwa anatangaza Mechi hiyo.
Mpenja Tv tumepata ugeni wa Semaji la Simba Ahmed Ally mapema Leo July 10, amefika huku Gari yake ikiwa imebandikwa Majina ya Nyota wapya ambao wamesajiliwa na Simba katika Dirisha hili. Pia Semaji limeeleza sababu za Simba kufanya Usajili mkubwa na Mipango yao ya Pre-Seasons ambayo watasafiri Kesho Julai 11/2023 kuelekea Nchini Uturuki ambapo watakaa kwa Wiki 3 kabla ya kurejea Nchini kwa ajili ya Msimu ujao wa 2023/24
Karibu kutazama Exclusive interview na Fiston Mayele, Nyota wa Kimataifa wa Congo na MVP wa Ligi Kuu ya NBC Msimu 2022/2023. Mayele ameweka sawa tetesi za kuondoka Yanga na amewatoa hofu Mashabiki wa Yanga kuwa maongezi bado yanaendelea hivyo lolote linawezekana. Aidha Fiston ameshukuru Mashabiki wa Yanga kwa Upendo wanaonyesha kwake pamoja na utofauti wa Mashabiki wa Congo na Tanzania na amekiri kuwa Mashabiki wa Tanzania wanapenda Mpira kuliko Congo. Amejibu maoni ya Wadau kuhusu kuwa Mchoyo Uwanjani haswa kwenye nafasi za kufunga na ameeleza kiupana sana kwanini huwa anafanya hivyo na hana pasi nyingi za Mwisho. Sanjari na hayo Mayele ameeleza ukaribu wake na Wachezaji ambao wamepewa Mkono wa kwaheri na Yanga na namna alivyopokea taarifa hizo. Mwisho kabisa Fiston ametaja Kikosi chake bora Msimu uliokwisha.
Clatus Chama amerudi Leo July 4 kutoka kwao Zambia kwenye mapumziko baada ya kumaliza Msimu na sasa amerejea kujiandaa na Msimu 2023/2024. Clatus amewapongeza Wachezaji walioanzisha Michezo ya Bonanza kwa lengo la kuridisha kwa jamii, amekiri kuwa anatamani kufanya kama wanavyofanya wao. Aidha Clatus ameeleza namna alivyopokea taarifa ya kuagwa kwa Jonas Mkude na Erasto Nyoni kwani ni Wachezaji aliwazoea sana na wamekuwa na kiwango bora sana. Baada ya kuwa na Msimu mgumu wa kutokuwa na Mataji Chama amewaomba Mashabiki kuwaamini na ameahidi kupambana na Msimu huu kuwa kutafuta mataji. Sanjari na hayo Clatus amepongeza Wachezaji waliofanya vizuri Msimu uliopita na ameahidi kufanya vizuri Msimu ujao na kurudi kwenye kinyang'anyiro cha MVP.
Leo ndio Leo 🔥 ndani ya Mkoa wa Morogoro Wadau na wapenzi wa Soka Watashuhudia Burudani safi ya mpira wa Miguu katika Dimba la Jamhuri 🏟.. Ni Mchezo wa Hisani WAPE TABASAMU 2023 kati ya TEAM KIBWANA SHOMARI Vs TEAM DICKSON JOB ⏰ Kuanzia Saa 08:00 Mchana JE, Unadhani nani ataibuka Mbabe 😊⁉️ Endelea Kuwa karibu na Mpenja Tv kwa Updates Zaidi.
Ally Kamwe ametoa sifa za kutosha kwa Kiungo Jonas Mkude 'Nungu nungu' kuwa ni kiungo bora wa mkabaji kwa hapa Tanzania. Aidha Kamwe ameeleza kuwa Jonas anaweza kucheza Timu yoyote Tanzania hata Young Africans kuna uwezekano wa Jonas kucheza. Sanjari na hayo Ally amejibu maswali ya Chemsha bongo na kuimba Wimbo ambao anausilikiliza sana kipindi hiki ambacho Ligi imekwisha.