Badhi ya Nyota watakao kipiga kwenye Mchezo wa Timu Samatta dhidi ya Timu Kiba wakiwa wanawasili kwenye Dimba la Azam Complex. Aidha wadau wakubwa wa Michezo wakiwemo Wasanii wa Muziki pia wamefika hapa kushuhudia Mbungi la Timu Samatta dhidi ya Timu Kiba
Mpenja Tv tumezungumza na Mchambuzi wa Soka kutoka Azam Media Limited Ramadhan Mbwaduke kuhusu takwimu za Kocha Roberto Oliveira "Robertinho" ndani ya Klabu ya Simba tangu alivyoanza kuifundisha na nini anakiona kwa Simba Msimu ujao wa 2023/2024. Pia amesema licha ya Simba SC kumaliza ligi wakiwa nafasi ya pili bado kocha Robertinho ana Takwimu Bora ukilinganisha na kocha Nasreddine Nabi ambaye ametwaa Ubingwa wa Makombe yote makubwa ngazi ya Klabu Nchini,Fainali Kombe la Shirikisho Afrika.
Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ tayari ipo kambini kujiandaa na mechi ya Kundi F dhidi ya Niger kuwania kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika ‘Afcon 2023’ itakayopigwa Jumapili kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, huku timu hiyo ikihitaji ushindi kwa lengo la kujiweka pazuri kwenda Ivory Coast.
Magoli mawili ya Singida Big Stars…. Wauaji ni Bruno Gomes na Medie Kagere… .
NBCPL Magoli mawili ya Singida Big Stars…. Wauaji ni Bruno Gomes na Medie Kagere… . FT: Singida BS 2-1 Ruvu Shooting.
USM Alger walishinda kwenye Dimba la Benjamin Mkapa na Yanga wameenda kushinda Kwenye Dimba la July 5, kila mmoja ameshindwa kwenye Ardhi ya Ugenini lakini Kombe limeenda kwa USM Alger. Hii ni tathmini ya Gharib Mzinga 'KILWA FINEST' Kuhusu Mchezo wa Pili wa Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika. Mzinga ameeleza kuhusu mipango ya Timu za Algeria kuhakikisha wanakuza vipaji na kufikia Nchi ya ahadi yenye Mafanikio ya Kisoka. Aidha ameeleza kuwa USM Alger hawajabadilika bali Yanga ndio walibadilika.
Leo Tarehe 29 Mei,Mpenja Tv tumefanya Mahojiano na Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba Sc Ahmed Ally na kuweka wazi Mwenendo wa Timu hiyo wakati huu ambao Ligi Kuu imesimama wakiwa wamebakiza Mechi Mbili Msimu kwisha.
Mchambuzi wa Soka kutoka Azam Media LTD ,Gharib Mzinga amewachambua kiundani wapinzani wa Yanga SC, USM Alger ambao watacheza nao Mchezo wa Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika,Jumapili hii Mei 28 2023,Katika Dimba la Benjamin Mkapa.