BIASHARA UNITED 2-1 MTIBWA SUGAR; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 14/02/2019)
BIASHARA UNITED 2-1 MTIBWA SUGAR; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 14/02/2019)

Timu ya Mtibwa Sugar imeendelea kupokea vipigo kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya leo kufungwa mabao 2-1 na Biashara United kwenye Uwanja wa Karume mjini Musoma. Wenyeji Biashara United ndiyo waliotangulia kupata bao dakika ya 39 kupitia kwa George Makang’a kwa mpira wa adhabu ndogo ‘free-kick’, lakini Mtibwa walisawazisha kupitia kwa kichwa cha Riphat Kamis dakika ya 64 na kisha Biashara kupata bao la ushindi dakika ya 80 kupitia kwa Innocent Edwin.



MAGOLI YOTE: BIASHARA UNITED 2-1 MTIBWA SUGAR (TPL - 14/02/2019)
MAGOLI YOTE: BIASHARA UNITED 2-1 MTIBWA SUGAR (TPL - 14/02/2019)

Timu ya Mtibwa Sugar imeendelea kupokea vipigo kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya leo kufungwa mabao 2-1 na Biashara United kwenye Uwanja wa Karume mjini Musoma. Wenyeji Biashara United ndiyo waliotangulia kupata bao dakika ya 39 kupitia kwa George Makang’a kwa mpira wa adhabu ndogo ‘free-kick’, lakini Mtibwa walisawazisha kupitia kwa kichwa cha Riphat Kamis dakika ya 64 na kisha Biashara kupata bao la ushindi dakika ya 80 kupitia kwa Innocent Edwin. Tazama mabao.



MAGOLI: AZAM FC 1-1 ALLIANCE FC (TPL – 06/02/2019)
MAGOLI: AZAM FC 1-1 ALLIANCE FC (TPL – 06/02/2019)

Azam FC, imelazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Alliance katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) uliofanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Ilibidi Azam FC iweze kusubiri hadi dakika ya 79 kuweza kupata bao la uongozi, lililofungwa na Joseph Mahundi, aliyeingia dakika ya 76, kuchukua nafasi ya Ramadhan Singano, na alifunga bao hilo kiustadi akiunganisha krosi ya Chirwa. Dakika ya 90 Alliance ilisawazisha kupitia kwa Dickson Ambundo, akimalizia mpira uliogonga mwamba kufuatia mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na Israel Patrick. Azam walionekana kulalamikia bao hilo wakidai kuwa beki wao Agrey Moris alisukumwa kabla ya kufungwa lakini, mwamuzi Abubakar Mturo (Mtwara) na Msaidizi namba moja, Mohamed Mkono (Tanga), waliamuru kuwa bao halali.



MAGOLI: TZ PRISONS 2-1 MBAO FC - Kocha wa Mbao asingizia uwanja (TPL – 06/02/2019)
MAGOLI: TZ PRISONS 2-1 MBAO FC - Kocha wa Mbao asingizia uwanja (TPL – 06/02/2019)

Tanzania Prisons imepata ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa Februari 6, 2019 kwenye Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Magoli ya Wenyeji hao wa mchezo yamefungwa na Salum kKimenya dakika ya 12 na Adam Adam dakika ya 20 huku Mbao wakipata bao lao kwa mpira wa adhabu ndogo dakika ya 34 kupitia kwa Amosi Charles. Baada ya mchezo huo makocha wa timu zote mbili wakazungumza ambapo Kocha wa Tanzania Prisons Adolf Rishard amewapongeza wachezaji wake wa ushindi huku akitaja mvua kuwa kikwazo kwa upande wao, wao kocha wa Mbao FC Ally Bushiri akilalamikia hali ya uwanja kuwa sababu ya wao kupoteza mchezo. Tazama magoli na mahojiano



AZAM FC 1-1 ALLIANCE FC: HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 6/2/2019)
AZAM FC 1-1 ALLIANCE FC: HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 6/2/2019)

Azam FC, imelazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Alliance katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) uliofanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Ilibidi Azam FC iweze kusubiri hadi dakika ya 79 kuweza kupata bao la uongozi, lililofungwa na Joseph Mahundi, aliyeingia dakika ya 76, kuchukua nafasi ya Ramadhan Singano, na alifunga bao hilo kiustadi akiunganisha krosi ya Chirwa. Dakika ya 90 Alliance ilisawazisha kupitia kwa Dickson Ambundo, akimalizia mpira uliogonga mwamba kufuatia mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na Israel Patrick. Azam walionekana kulalamikia bao hilo wakidai kuwa beki wao Agrey Moris alisukumwa kabla ya kufungwa lakini, mwamuzi Abubakar Mturo (Mtwara) na Msaidizi namba moja, Mohamed Mkono (Tanga), waliamuru kuwa bao halali. Mchezo huo ulikuwa na kasi sana, Azam FC ikianza kwa mashambulizi makali langoni mwa Alliance, ambapo dakika ya kwanza Obrey Chirwa, alikosa bao la wazi baada ya kuupiga vibaya mpira akiwa anatazamana na lango ndani ya eneo la hatari, akipokea pasi ya Donald Ngoma. Mabingwa hao waliweza kupata ugumu kuipenya safu ya ulinzi ya Alliance, kutokana na timu hiyo kusimama wengi kujilinda nyuma ya mpira wakati Azam FC ikishambulia. Mara baada ya mchezo huo kumalizika, kipa wa Azam FC, Razak Abalora, alioneshwa kadi nyekundu kufuatia kadi ya pili ya njano iliyosababishwa na lugha ya kutoridhishwa na maamuzi aliyoitoa kwa mwamuzi huyo. Sare hiyo inaifanya Azam FC kufikisha jumla ya pointi 48 katika nafasi ya pili kwenye msimamo ikiwa na mchezo mmoja mkononi, ikizidiwa pointi saba na kinara Yanga aliyefikisha 55 kufuatia suluhu yake ya jana dhidi ya Singida United.



Kocha Biashara United afafanua kisa cha kufokeana na kipa wake hadharani, ataja adhabu
Kocha Biashara United afafanua kisa cha kufokeana na kipa wake hadharani, ataja adhabu

Kocha mkuu wa Biashara United Amri Said ametoa ufafanuzi juu ya sakata la mlinda mlango wake Nouridine Balora ambaye walipishana kauli wakati wa mchezo wa raundi ya nne ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports walipokuwa wakicheza dhidi ya Yanga. Amri Said amesema kuwa balora alifanya kitendo cha utovu wa nidhamu baada ya kufanyiwa mabadiliko kwenye mchezo huo ambapo, wakati anaelekea kwenye benchi alikuwa akiongea maneno ambayo si mazuri kama mchezaji. Katika mchezo huyo Yanga ilishinda kwa penati 5-4 baada ya sare ya mabao 2-2.



AFRICAN LYON 0-1 YANGA SC; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 20/12/2018)
AFRICAN LYON 0-1 YANGA SC; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 20/12/2018)

Bao pekee kutoka kwa beki Abdallah Haji Shaibu ‘Ninja’ limetosha kuipa Yanga pointi tatu mbele ya African Lyon katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha. Ninja amefunga goli hilo kwa kichwa dakika ya 64 akimalizia mpira wa adhabu ndogo ulipigwa na Ibrahim Ajibu, bao lililodumu hadi mwisho wa mchezo na kuendeleza rekodi ya ushindi na kutopoteza mchezo kwa Yanga tangu kuanza kwa ligi msimu huu. Ushindi huo unaifanya Yanga izidi kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi ikifikisha pointi 47, mbele ya Azam wenye pointi 40 na Simba wenye pointi 30.



KIPYENGA CHA MWISHO: "Goli moja la Simba dhidi ya JKT Tanzania halikuwa halali" (08/11/2018)
KIPYENGA CHA MWISHO: "Goli moja la Simba dhidi ya JKT Tanzania halikuwa halali" (08/11/2018)

Kwa mujibu wa kipindi hiki cha terehe 08/11/2018, bao la pili alilofunga Meddie Kagere kwenye mchezo kati ya JKT Tanzania vs Simba SC uliopigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga Jumamosi ya Novemba 2, 2018, halikuwa bao halali kwa kuwa mfungaji alikuwa ameotea kabla ya kufunga. Pamoja na matukio mengine yaliyojiri kwenye mchezo huo, pia palikuwa na matukio mawili ya wachezaji wa JKT kudai penati wakidai wachezaji wa Simba Mohamed Hussein na Erasto Nyoni kwa nyakati tofauti, walishika mpira ndani ya eneo la hatari hadi kusababisha mchezaji wa JKT Ahmed Shiboli kutolewa nje kwa kadi nyekundu. Mbali na mchezo huo, kipindi hiki kimechambua mechi kdhaa za raundi ya 13 ya Ligi Kuu Tanzania Bara ukiwemo mchezo wa Yanga vs Ndanda SC na ule wa Kagera Sugar vs Azam FC. Tukio kubwa katika mchezo wa Kagera Sugar na Azam FC ni mchezaji wa Azam FC Donald Ngoma kupewa kadi nyekundu, kadi ambayo wengi hawakuelewa sababu za adhabu hiyo kumkumba. Waamuzi wawili wastaafu ambao ni magwiji, Osman Kazi na Omary Abdulkadir wamechambua matukio yote na kuonesha ni wapi waamuzi walikosea na wapi waamuzi walipatia, na nini walipaswa kufanya. Kipyenga cha Mwisho ni kila Alhamis saa 3:30 usiku Azam Sports 2.




« Previous Next »


Popular Tags

#Best Champions League  #LeBron James  #Shaquille O'Neal  #Goalkeeper Saves  #Tristan Thompson  #Counter Attack Goals Football  #Ronaldinho  #Miami Heat  #Football Defensive Skills  #Stephen Curry  

Popular Users

#BMcCarthy32  #OleksiakPenny  #JohnCena  #AdamSchefter  #justinbieber  #jimmyfallon  #KDTrey5  #CMPunk  #KevinHart4real  #nytimes  #Cristiano  #incarceratedbob  #_BAnderson30_  #billbarnwell