Kwa mujibu wa kipindi hiki cha terehe 08/11/2018, bao la pili alilofunga Meddie Kagere kwenye mchezo kati ya JKT Tanzania vs Simba SC uliopigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga Jumamosi ya Novemba 2, 2018, halikuwa bao halali kwa kuwa mfungaji alikuwa ameotea kabla ya kufunga. Pamoja na matukio mengine yaliyojiri kwenye mchezo huo, pia palikuwa na matukio mawili ya wachezaji wa JKT kudai penati wakidai wachezaji wa Simba Mohamed Hussein na Erasto Nyoni kwa nyakati tofauti, walishika mpira ndani ya eneo la hatari hadi kusababisha mchezaji wa JKT Ahmed Shiboli kutolewa nje kwa kadi nyekundu. Mbali na mchezo huo, kipindi hiki kimechambua mechi kdhaa za raundi ya 13 ya Ligi Kuu Tanzania Bara ukiwemo mchezo wa Yanga vs Ndanda SC na ule wa Kagera Sugar vs Azam FC. Tukio kubwa katika mchezo wa Kagera Sugar na Azam FC ni mchezaji wa Azam FC Donald Ngoma kupewa kadi nyekundu, kadi ambayo wengi hawakuelewa sababu za adhabu hiyo kumkumba. Waamuzi wawili wastaafu ambao ni magwiji, Osman Kazi na Omary Abdulkadir wamechambua matukio yote na kuonesha ni wapi waamuzi walikosea na wapi waamuzi walipatia, na nini walipaswa kufanya. Kipyenga cha Mwisho ni kila Alhamis saa 3:30 usiku Azam Sports 2.
LIGI YA VIJANA U17 | Ni Kariakoo Derby ya vijana, Yanga U17 na Simba U17, mchezo umemalizika kwa sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa TFF, Kigamboni Dar es Salaam. Yanga wametangulia kwa goli la Issa Ramadhan dakika ya 15, na Simba kuchomoa dakika za majeruhi... Tazama highlights
Kiungo Allan Okello amefunga magoli mawili katika ushindi wa 3-1, Yanga dhidi ya Namungo FC, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa KMC Complex, Dar es Salaam. Aliyeitanguliza Yanga kwenye mchezo huu alikuwa ni Duke Abuya, kabla ya Hassan Kabunda kuchomoa kipindi cha kwanza... na Allan Okello akapiga mawili kipindi cha pili.
Kiungo Allan Okello amefunga magoli mawili katika ushindi wa 3-1, Yanga dhidi ya Namungo FC, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa KMC Complex, Dar es Salaam. Aliyeitanguliza Yanga kwenye mchezo huu alikuwa ni Duke Abuya, kabla ya Hassan Kabunda kuchomoa kipindi cha kwanza... na Allan Okello akapiga mawili kipindi cha pili. Haya hapa magoli...
Yamefungwa magoli matatu.... chuma mbili zikiwekwa kambani na Allan Okello na goli lingine likifungwa na Mudathir Yahya kwenye Uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam. Hii ni Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara.
#CRDBBankFederationCup: Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo kati ya Simba dhidi ya TRA United kwenye mchezo wa robo fainali ya CRDB Bank Federation Cup. Magoli ya Simba yamefungwa na Clatous Chama, Anicet Oura, Selemani Mwalimu na Bashiri Kibaila. Mchezo wa nusu fainali ni Coastal Union dhidi ya Simba SC. FT: Simba SC 4-0 TRA United #KombeLaShirikishoLaCRDBBank #CRDBCup #FACup #SimbaSCVsTRAUnited #SimbaSC #TRAUnited #SimbaTRAUnited
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara, Yanga SC wamepoteza mchezo kwa mara ya kwanza msimu huu, wakichapwa 3-2 na Dodoma Jiji, mchezo, mchezo ukipigwa Airtel Stadium, Singida. Magoli ya Yanga yamefungwa na Allan Okello dakika ya 2 na 41, huku magoli ya Dodoma Jiji yakitoka kwa Bakari Mwamnyeto aliyejifunga dakika ya 29, Mwana Kibuta David dakika ya 90 na Wazir Junior Shemtembo dakika za nyongeza. Haya hapa magoli yote..
#NBCPL: Tazama magoli yote matano yaliyofungwa kwenye mchezo wa NBC Premier League kati TRA United dhidi ya Azam FC. FT: TRA United 4-1 Azam FC Magoli ya TRA United yamefungwa na Ally Ng'azi, Ammy Mapaka na Ramadhan Salum 'Chobwedo' Goli la Azam FC limefungwa na Jephte Kitambala Bola. #NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidi #TRAUnitedvsAzamFC #TRAUnited #AzamFC #TRAUnitedAzamFC
KARIAKOO DERBY | Imepigwa dabi moja ya maana sana kwenye Dimba la Amaan, Zanzibar, Yanga na Simba wakimaliza dakika 90 bila bao, lakini burudani za kutosha. Hii ni mechi ya Ligi Kuu ya NBC Tanzania