Mtangazaji kinara wa soka nchini, Baraka Mpenja, amefanya mazungumzo na Mtangazaji wa soka wa Azam Media LTD, Gharib Mohamed Ally Mzinga kuhusu Maisha yake ya nyuma lakini pia ikumbukwe leo ni kumbukizi ya kuzaliwa ya Mtangazaji machachari wa Soka Ghalibu Mzinga. Lakini pia Ghalibu mzinga ametoa mtazamo wake katika mechi ya ligi ya mabingwa Afrika kati ya Simba na Yanga kuwa zinaweza kufika hatua ya fainali katika mashindano hayo.
Meneja Habari na Mawasiliano wa Yanga SC,Ally kamwe aeleza namna ambavyo wamewapokea wapinzani wao Mamelodi Sundowns kwenye robo fainali ya ligi ya Mabingwa Afrika na namna wanavyojipanga kumenyana nao Machi 30,2024 Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Mtangazaji wa Soka kutoka Azam Media LTD,Gharib Mzinga ametoa mtazamo wake kuhusu wapinzani wa Yanga SC kwenye robo fainali ligi ya Mabingwa Afrika Mamelodi Sundowns na Wapinzani wa Simba SC,Al Ahly.
Mtangazaji wa soka kutoka Azam Media LTD, Gharib Mzinga ametoa mtazamo wake kiundani mchezo wa Machi 17,2024 wa Ligi Kuu ya NBC PL kati ya Azam FC na Yanga SC, utakaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa,Saa 2:15 usiku.
Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC,Ahmed Ally ameungana na baadhi ya Mashabiki kutazama Droo ya robo fainali ligi ya Mabingwa Afrika,inayochezeshwa Leo Machi 12,2024 Cairo Misri.
Leo Machi 6,2024 Mnyama Simba anashuka Dimba la Jamhuri Morogoro kumenyana na Wajelajela Tanzania Prisons katika mchezo wa ligi kuu ya NBC ,Saa 10:00 jioni.
Leo Machi 2,2024 Simba SC inaikaribisha Jwaneng Galaxy ya Botswana katika Uwanja wa Benjamin Mkapa,kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi,Saa 1:00 usiku.
Mtangazaji kinara wa soka nchini, Baraka Mpenja, amefanya mazungumzo na Mtangazaji wa soka wa Azam Media LTD, Gharib Mohamed Ally Mzinga kuhusu mechi ya YANGA SC vs CR Belouizdad. Mzinga ndiye alitangaza mchezo huu ambayo Yanga wameshinda 4-0 na kufuzu Robo Fainali Ligi ya Mabingwa Afrika.