Meneja Habari na Mawasiliano wa klabu ya Yanga Ally Kamwe, amezungumza na Mpenja TV na kuelezea Mipango ya Timu yake kuelekea katika Mchezo wa CRDB Federation Cup Dhidi ya Dhidi ya Tabora United Mchezo ambao utachezwa May 1,2024 katika uwanja wa Azam Complex Pia Ally Kamwe amegusia kuhusu tetesi za Mchezaji wao Pacome Zouzoua na kuweka wazi kinachoendelea mpaka sasa.
Leo Aprili 13,2024 Wajukuu wa Mbogo maji Ihefu SC wanamualika Mnyama Simba SC katika Uwanja wa CCM LITI Singida kumenyana mchezo wa ligi kuu ya NBC,Saa 10:00 jioni.
Meneja Habari na Mawasiliano wa Yanga SC,Ally kamwe amewasili Dodoma kwa ajili ya mchezo wa kombe la Shirikisho la Benki ya CRDB,utakaochezwa Saa 2:00 usiku,Uwanja wa Jamhuri.
Leo Machi 30,2024 Katika Dimba la Benjamin Mkapa inapigwa mbungi ya mkondo wa kwanza ya ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga SC na Mamelodi Sundowns kutoka Afrika Kusini,Saa 3:00 usiku.
Leo Machi 29,2024 Mnyama Simba SC anashuka Dimba la Benjamin Mkapa kumenyana na Al Ahl kutoka Misri katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa robo fainali ya ligi ya Mabingwa Afrika,Saa 3:00
Mtangazaji Mwandamizi wa soka nchini, Baraka Adson Lamsi Mpenja, maarufu Mwamba wa Umalila, Fahari ya Itete, Sauti ya Radi, amekutana na kufanya Mazungumzo maalumu na Watangazaji vinara wa kandanda kutoka Azam Media LTD, Gharib Mzinga na Ayubu Hinjo. Wamezichambua mechi za robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika, Machi 29, Simba vs Al Ahly na Machi 30, Yanga vs Mamelodi Sundowns.
Mtangazaji kinara wa soka nchini, Baraka Mpenja, amefanya mazungumzo na Mtangazaji wa soka wa Azam Media LTD, Gharib Mohamed Ally Mzinga kuhusu Maisha yake ya nyuma lakini pia ikumbukwe leo ni kumbukizi ya kuzaliwa ya Mtangazaji machachari wa Soka Ghalibu Mzinga. Lakini pia Ghalibu mzinga ametoa mtazamo wake katika mechi ya ligi ya mabingwa Afrika kati ya Simba na Yanga kuwa zinaweza kufika hatua ya fainali katika mashindano hayo.
Meneja Habari na Mawasiliano wa Yanga SC,Ally kamwe aeleza namna ambavyo wamewapokea wapinzani wao Mamelodi Sundowns kwenye robo fainali ya ligi ya Mabingwa Afrika na namna wanavyojipanga kumenyana nao Machi 30,2024 Uwanja wa Benjamin Mkapa.