COASTAL UNION 1-1 MBAO FC; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 28/09/2018)
COASTAL UNION 1-1 MBAO FC; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 28/09/2018)

Coastal Union ya Jijini Tanga imepata sare ya bao 1-1 na Mbao FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo kwenye Uwanja wa Mkwakwani Jijini humo. Katika mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua, Coastal ndiyo waliotangulia kupata bao kupitia kwa Ayoub Lyanga dakika ya 31 kabla ya Mbao kureje kwa nguvu zaidi kipindi cha pili na kusawazisha kupitia kwa said Hamis Said Jr dakika ya 50. Baada ya mchezo huo makocha wa timu zote mbili Amri Said wa Mbao na Juma Mgunda wa Coastal Union wameuzungumzia mchezo huo



“…unaweza ukaumia” - Alikiba ataja kinachomfanya asionekane dimbani kwenye mechi za TPL?
“…unaweza ukaumia” - Alikiba ataja kinachomfanya asionekane dimbani kwenye mechi za TPL?

Mchezaji wa Coastal Union ambaye pia ni msanii wa bongo fleva, Alikiba ametegua kitendawili kuhusu siku ambayo ataanza rasmi kucheza kwenye mfululizo wa michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara. Kiba amezungumza na Azam TV mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mbao FC uliopigwa kwenye dimba la Mkwakwani Jijini Tanga na kumalizika kwa sare ya bao 1-1. Katika mahijiano haya pia Alikiba ameichambua timu yake kwa jinsi alivyoutazama mchezo. Mchezaji huyo aliyesajiliwa Coastal Union msimu huu, hajacheza mchezo wowote tangu kuanza kwa ligi hiyo mwishoni mwa mwezi Agosti.



Magoli yote, Mbao FC ikiilazimisha Coastal Union sare ya bao 1-1 (TPL - 28/09/2018)
Magoli yote, Mbao FC ikiilazimisha Coastal Union sare ya bao 1-1 (TPL - 28/09/2018)

Coastal Union ya Jijini Tanga imepata sare ya bao 1-1 na Mbao FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo kwenye Uwanja wa Mkwakwani Jijini humo. Katika mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua, Coastal ndiyo waliotangulia kupata bao kupitia kwa Ayoub Lyanga dakika ya 31 kabla ya Mbao kureje kwa nguvu zaidi kipindi cha pili na kusawazisha kupitia kwa said Hamis Said Jr dakika ya 50. Haya ndiyo magoli yenyewe



Tazama 'Off-Side' ya utata; Coastal Union1-0 Biashara United (TPL 25/
Tazama 'Off-Side' ya utata; Coastal Union1-0 Biashara United (TPL 25/

Ilikuwa ni free-kick iliyopigwa na Biashara United, na mpira uzama kimiani, lakini mwamuzi wa pembeni akaamua kuwa ilikuwa ni off side. Ni kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania uliopigwa kwenye dimba la Mkwakwani Jijini Tanga, Agosti 25, mwaka huu. Itazame, kisha toa maoni yako, wewe umeionaje?



HIGHLIGHTS: COASTAL UNION 1-0 BIASHARA UNITED; (TPL 25/08/2018)
HIGHLIGHTS: COASTAL UNION 1-0 BIASHARA UNITED; (TPL 25/08/2018)

Timu ya Coastal Union ya Tanga imepata ushindi wa bao 1-0 kwenye mchezo wa raundi ya pili ya Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo kwenye Dimba la CCM Mkwakwani, Jijini Tanga. Bao pekee la Coastal Union kwenye mchezo huo limefungwa na Haji Ugando dakika ya 20 ya mchezo. Katika mchezo huo, Coastal walianza kwa kasi na kufanikiwa kutikisa nyavu dakika ya 4 lakini ilikuwa ni off side, na kisha kupata penati dakika ya 13 lakini Mkwaju wa Mtenje Juma ukapanguliwa na kipa wa Biashara United Balora Nasridine. Biashara United walionekana kumlalamikia mwamuzi wa pembani baada ya kukataa bao lao la dakika ya 45 kwa madai kuwa mfungaji alikuwa ameotea. Mara baada ya mchezo, manahodha wa pande zote mbili wamezungumza. Tazama highlights.



MAGOLI: COASTAL UNION 1-1 LIPULI FC (TPL 22/08/2018)
MAGOLI: COASTAL UNION 1-1 LIPULI FC (TPL 22/08/2018)

Coastal Union ya Jijini Tanga imeshindwa kufurukuta katika dimba lake la nyumbani, Mkwakwani, baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Lipuli FC kwenye mchezo wa kwanza la Ligi Kuu Tanzania msimu huu. Wageni Lipuli FC ndiyo waliotangulia kupata bao dakika ya 59 kupitia kwa Zawadi Mauya na dakika kumi baadaye Coastal wakasawazisha kupitia kwa Bakar Mwamnyeto dakika ya 69. Haya hapa mabao yenyewe.



Coastal Union ilivyojipanga kutoshuka daraja, kamati ya usajili yamwaga mikakati
Coastal Union ilivyojipanga kutoshuka daraja, kamati ya usajili yamwaga mikakati

Siku chache baada ya ratiba ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara kuwekwa hadharani, Klabu ya Coastal Union ya Tanga imesema imeweka mikakati kabambe ya kufanya vizuri. Ikiwa imerejea katika ligi baada ya kuikosa msimu uliopita, uongozi wa Coastal Union umesema upo katika mikakati mizito kuhakikisha timu hiyo inafanya vizuri katika msimu ujao wa ligi hiyo. Timu hiyo inayotumia Uwanja wa Mkwakwani uliopo Tanga kama uwanja wake wa nyumbani, katika msimu ujao wa ligi kuu imepangwa kufungua dimba na Lipuli FC ya Iringa Agosti 22, mwaka huu mjini Tanga. Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Coastal Union, Steven Mguto, amesema kamwe safari hii hawatakubali kushindwa na kushuka tena daraja kwenda kucheza Ligi Daraja la Kwanza.




« Previous


Popular Tags

#Best Ball Controls  #Kawhi Leonard  #Paul George  #Stephen Curry  #Kawhi Leonard  #Lionel Messi  #Sergio Aguero  #Los Angeles Lakers  #Goalkeeper Saves  #Chris Paul  

Popular Users

#KimKardashian  #fauxpelini  #obj  #JLo  #nfl  #akshaykumar  #imVkohli  #DanicaPatrick  #josecanseco  #MikePereira  #oldhossradbourn  #blakegriffin23  #JJWatt  #themichaelowen