Ndani ya Dimba la Benjamin Mkapa Mabango ya Kieletroniki yameanza kufungwa rasmi kuelekea Mchezo wa AFL kati ya Simba dhidi ya Al-Ahly. Mpenja Tv tumezungumza na Steve Simon ambae ni Operation Manager wa Kampuni ya Formula 360 iliyopewa Tenda na Wizara ya Sanaa Utamaduni Michezo kufunga Mabango hayo. Yanachukua muda gani mpaka kukamilika? Yote utafahamu hapa. Aidha tumepata nafasi ya kufungua baadhi ya Kago za Mabango hayo ambayo yanafungwa Leo kwenye Dimba la Benjamin Mkapa
Mfahamu kwa undani shabiki na mwanachama wa Simba SC, Justine Mwakitalima historia ya maisha yake nje ya ushabiki . Mpenja Tv tumefunga safari mpaka nyumbani kwa Mwakitalima Ubungo Kisiwani, Mtaa wa Amani na kuzungumza masuala mbalimbali hususani maisha yake na namna pia anavyoishi na majirani zake tofauti na Ushabiki wa Mpira.
Leo Sep 20 ndani ya Azam Complex kunapigwa Mchezo mkubwa wa Ligi Kuu ya NBC mwenyeji ni Yanga huku Namungo FC 'Southern killers' akiwa mgeni wa Mchezo huo. Mchezo utaanza majira ya saa 1:00 za Usiku kwa saa za Afrika Mashariki, dakika 90 za nguvu zinazosimamisha shughuli za Wanamichezo na utulivu wote kuhamia Azam Complex. Mpenja Tv tunakuletea Matukio yote na Habari zinazojiri kabla na baada ya Mchezo huo kumalizika.
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC,Ally kamwe amezungumza namna Timu inavyoendelea kujifua kwa ajili ya mchezo wa ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya AL Merrikh ya Sudan,utakaochezwa Sept 16,2023 Uwanja wa Pele Kigali Rwanda. Kamwe amesema yapo Mabasi 24 kutoka Mikoa mbalimbali yatakayopeleka Mashabiki wa Yanga Rwanda,yakiwemo Mabasi ya Viongozi ambayo hadi sasa mawili yameshajaa,Basi la Rais wa Timu Eng. Hersi Said na Makamu wake Arafat Ally Haji.
Leo tarehe 29 Agosti katika dimba la Azam Complex Chamazi inapigwa mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara kati ya mwenyeji Yanga dhidi JKT Tanzania majira ya saa 1 usiku Mpenja Tv tupo Chamazi kuhakikisha unayapata matukio yote muhimu kuhusiana na mechi hii
Leo 26 Agosti,Yanga SC ikiwa nyumbani Uwanja wa Azam Complex Chamazi inamkaribisha ASAS kutoka Djibouti kwenye Mechi ya Marudiano Ligi ya Mabingwa Afrika ikiwa na Faida ya Bao 2 walizopata kwenye Mechi ya kwanza . Mpenja Tv tuko Mubashara kutokea Azam Complex hapa Chamazi kwaajili ya kukuhabarisha kila tukio linalojiri..
Leo Agosti 23 kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi Bingwa Mtetezi wa Ligi Kuu ya NBC Yanga Sc inamkaribisha KMC Fc Majira ya Saa 1:00 Usiku. Mpenja Tv tayari tumetia Timu kwaajili ya kukuletea Matukio yote kuhusu Mechi hiyo…
Leo Tarehe 22 Agosti Mpenja Tv imeanza safari kuelekea Kisiwani Zanzibar kwaajili ya Tukio la ufunguzi wa Tamasha la Kizimkazi linalofanyika kuanzia Tarehe 25 Kwenye Safari hii imewakutanisha Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba Sc pamoja na Yanga Sc Ahmed Ally pamoja na Ally Kamwe