Leo tarehe Novemba 19 ni kumbukumbu ya Siku ya Kuzaliwa ya Rais wa GSM Group of Companies pamoja na Mwekezaji wa Yanga, Ghalib Said Mohamed katika ukumbi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Dar es salaam. Mpenja Tv tunakuletea mfululizo wa matukio yote muhimu katika tukio hili kubwa.
Meneja habari na mawasiliano wa Yanga SC Ally Kamwe hii leo kupitia Mpenja Tv, Amefunguka kuhusu maandalizi ya michezo yao ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo Novemba 24 wataanzia nchini Algeria Dhidi ya CR Belouizdad. Ally Kamwe amesema kwamba kuelekea mchezo wao wa Disemba 2 dhidi ya Al Ahly wamejipanga kuhakikisha wanajaza uwanja mapema na kuleta burudani za kutosha siku ya mchezo huo.
Leo tarehe 12 Novemba Klabu ya Yanga imendaa Supu maalumu makao makuu Jagwani kwa lengo la kusherehekea ushindi walipata siku ya Novemba 05 dhidi ya Simba SC. Mpenja Tv tunakuletea matukio yote muhimu kuhusu Zoezi hili maalumu la Wana Yanga
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe ametema Cheche zake baada ya kumfunga Mtani wao Simba SC Goli 5-1,Kwenye Mchezo wa Novemba 5,2023 wa Ligi kuu ya NBC,uliopigwa Dimba la Benjamin Mkapa. Aidha Ally Kamwe ametupa kijembe kwa Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally baada ya kuona post zake mitandaoni.
Ofisa habari na mawasiliano wa Yanga Sc Ally Kamwe ametembelea ofisi za Mpenja Tv na kukutana na baadhi ya Staff wa Mpenja Tv. Aidha Ally Kamwe hajaacha kuleta utani na kugusia mchezo wa AFL kati ya Simba na Al Ahly
Mtangazaji na Mchambuzi wa soka kutoka Azam Media LTD,Gharib Mzinga ameuchambua kiundani mchezo wa Oktoba 20,2023 wa African Football League kati ya Simba SC na Al Ahly,utakaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa,Saa 12:00 jioni. Pia mzinga ameeleza namna alivyofarijika kuona Ufunguzi wa Michuano hiyo kufanyika Tanzania
Kikosi cha Al-Ahly kimetua Tanzania kumenyana na Simba kwenye Mchezo wa AFL dhidi ya Simba ambae ndio mwenyeji wa Mchezo huo. Balozi wa Misri Nchini Tanzania Sharif Ismail amezungumza baada ya Kikosi cha Al-Ahly kutua Tanzania. Mapokezi yao na baadhi mipango yote ya Mechi Balozi amezungumza hapa
Baada ya Kimya kirefu hatimae Ofisa Habari na Mawasiliano wa Azam FC Hasheem Ibwe ameibuka tena na kuutangazia umma kuwa wanautaka Ubingwa Msimu. Ibwe amezungumza kinachoendelea kwenye Kikosi cha Azam FC Wakati huu ambao Ligi imesimama pamoja na Nyota wanatarajia kurejea hivi karibuni. Aidha ametoa shukrani kwa Timu iliyowauzia Feisal Salum kwani walichotaka akifanye ndio anakifanya kwa sasa kwenye Kikosi cha Azam FC. Pia ametoa maoni yake juu ya Michuano ya AFL ambao Simba wanakwenda kufungua Pazia dhidi ya Al-Ahly kutoka Misri, ambapo Ibwe amewatakia Simba lolote liwakute kwani adui yake hawezi kumuombea mema. Sanjari na hayo ametuma salam kwa Baraka Mpenja kuwa asitishie kuacha kutangaza kwani Mashabiki wa Soka bado wanataka burudani.