Azam FC's user profile page. Match highlights, posts and more on site!

“”

 Report User

Highlights

Undani wa shangilia ya Messi vs Ruvu Shooting; Amtaja mwanaye
Undani wa shangilia ya Messi vs Ruvu Shooting; Amtaja mwanaye

MASHABIKI wengi wa soka wamekuwa wakiwa na maswali mengi kuhusu staili ya ushangiliaji ya winga Ramadhan Singano ‘Messi’, aliyofanya jana Alhamisi mara baada ya kufunga bao dhidi ya Ruvu Shooting. Singano akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz amesema kuwa ameshangilia bao kwa staili hiyo akimshukuru Mwenyezi Mungu baada ya kumjalia mke wake kupata mtoto wa kiume mwanzoni mwa wiki hii, akiwa ni mtoto wake wa kwanza kwenye maisha yake. “Staili yangu ni kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumjalia mke wangu kunipa mtoto wa kiume, shangilia ile ilikuwa inamaanisha herufi ya ‘Y’ jina la baba yangu Yahya na mtoto wangu nikimpa jina la Yahya Ramdhan Singano,” alisema winga wa Azam FC, Ramadhan Singano 'Messi'. #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh



TPL ROUND 14 | Azam FC 2-1 Ruvu Shooting | Match Highlights
TPL ROUND 14 | Azam FC 2-1 Ruvu Shooting | Match Highlights

KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imefanya kweli baada ya kuinyuka mabao 2-1 Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) uliomalizika kwenye Uwanja wa Azam Complex leo Alhamisi usiku. Ushindi huo unaihakikishia Azam FC nafasi ya kuendelea kubakia kileleni mwa msimamo wa ligi ikifikisha pointi 33 baada ya kushinda mechi 10 na sare tatu ikiwa haijapoteza mchezo hata mmoja.



Kagera vs Azam FC Post Match Press | Azam FC yajipanga kuendelea na moto TPL
Kagera vs Azam FC Post Match Press | Azam FC yajipanga kuendelea na moto TPL

BENCHI la ufundi la Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, limejipanga vilivyo kuwajenga wachezaji kisaikolojia na kisawasawa ili kuendelea na rekodi nzuri waliyoanza katika Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) msimu huu. Azam FC iliyoichapa Kagera Sugar leo bao 1-0 lililofungwa na Donald Ngoma, ipo kileleni kwa takribani wiki nne sasa ikifikisha jumla ya pointi 30 baada ya ushindi wa mechi tisa na sare tatu huku ikiwa haijapoteza mchezo hata mmoja. #AzamFCUnbeaten #AzamFCPopoteInakanyaga



Waziri Mwakyembe aimwagia sifa Azam FC; Asema ni Kiwanda cha Soka Tanzania
Waziri Mwakyembe aimwagia sifa Azam FC; Asema ni Kiwanda cha Soka Tanzania

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwankyembe, leo alifanya ziara ya kutembelea Makao Makuu ya Azam FC ‘Azam Complex’ na kukiri kuwa timu hiyo ni kiwanda cha soka nchini. Ziara hiyo ya Mwakyembe ilikuwa ni maalumu kwa ajili ya kuangalia Azam FC ilipofikia kwenye uboreshaji wa uwanja huo ikiwa ni maandalizi ya kuelekea fainali za Mataifa ya Afrika kwa Vijana chini ya umri wa miaka 17 (AFCON U-17) zitakazofanyika nchini mwakani. Uwanja wa Azam Complex ni miongoni mwa viwanja vitatu nchini vilivyoteuliwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kwa kushirikiana na la hapa nchini (TFF), vingine viwili vikiwa ni Uwanja wa Taifa na ule wa Uhuru. Kigogo huyo aliambatana na Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Taifa (BMT), Alex Nkeyenge na Mkurugenzi wa Mashindano TFF, Salum Madadi, ambao walikaribishwa na wenyeji wao akiwemo Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Wakurugenzi, Nassor Idrissa ‘Father’, Makamu Mwenyekiti Omary Kuwe, Meneja wa timu, Philllip Alando. Akitoa neno kwenye ziara hiyo, Waziri Mwakyembe, aliupongeza uongozi wa Azam FC kwa kazi kubwa waliyofanya kwenye kuboresha uwanja huo kwa ajili ya fainali hizo ambazo zitafanyika kwa mara ya kwanza nchini. “Kwa kweli ni mara yangu ya kwanza kutembelea Azam Complex na nimejiridhisha mwenyewe kwamba hiki ni kiwanda cha soka, kiwanda cha michezo kuna kila kitu hapa na tukifikia hatua ambayo pengine timu zetu zenye sura ya Kitaifa hata zikawa tatu, nne, tano zikawa na mfumo ulioko hapa Azam Complex tayari sisi Tanzania tumeshakuwa nchi ya soka. “Na nadhani tutaanza kuuza wachezaji wengi sana duniani ambao pia watachangia sana katika pato la Taifa maana wenzetu wengi kama nchi ya Brazil inaendeshwa na pesa kama hiyo, Azam hongereni sana mmefanya kazi kubwa sana,” alisema.



Ngoma awaahidi makubwa mashabiki Azam FC | Ngoma First Action At Azam FC
Ngoma awaahidi makubwa mashabiki Azam FC | Ngoma First Action At Azam FC

BAADA ya jana kucheza mechi yake ya kwanza Azam FC akitokea kwenye majeruhi, mshambuliaji Donald Ngoma, ameonesha kufurahishwa sana huku akiwaahidi makubwa mashabiki wa timu hiyo. Azam FC iliyokuwa ikicheza na Lipuli jana usiku na kutoka suluhu, ilishuhudiwa Ngoma akiingia dakika ya 62 kuchukua nafasi ya kiungo mkabaji Mudathir Yahya, mchezo huo pia ukiwa ni wa kwanza kwake tokea asajiliwe na timu hiyo msimu huu akitokea Yanga. Licha ya kutoka kwenye majeraha ya takribani mwaka mmoja, Ngoma alionekana kuanza vema jana mechi yake ya kwanza akicheza kwa kujituma na kupambana na mabeki wa Lipuli huku akipata nafasi muhimu mbili za kufunga moja ikiwa ni ile ya kuangushwa katika eneo la hatari na kipa.



Mzungu apagawishwa na Azam FC na kujiunga na mashabiki kushangilia ushindi
Mzungu apagawishwa na Azam FC na kujiunga na mashabiki kushangilia ushindi

Mzungu apagawishwa na Azam FC na akijiunga na mashabiki wa timu hiyo mara baada ya ushindi dhidi ya Alliance (1-0) juzi. Shuhudia uhondo kamili kwa kuangalia video hii.




« Previous Next »


User Detail Page

You can find user latest posts and related content on the page. Friends, comments for events / matches are also available on the page. Even you can find users who are same pleasure with current user.

#Travel, #SupportYourTeam, #AllAboutSports