Azam FC's user profile page. Match highlights, posts and more on site!

“”

 Report User

Highlights

SURE BOY, MESSI WAIFANYIA UBAYA BIASHARA UNITED | AZAM FC 2-1 BIASHARA UTD | TPL 2018/2019 ROUND 24
SURE BOY, MESSI WAIFANYIA UBAYA BIASHARA UNITED | AZAM FC 2-1 BIASHARA UTD | TPL 2018/2019 ROUND 24

#TPLRound24 KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendeleza wimbi la ushindi kwenye mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) baada ya kuichapa Biashara United mabao 2-1. Mabao ya Azam FC, yamefungwa na kiungo Salum Abubakar 'Sure Boy' (46') kwa kichwa na Ramadhan Singano 'Messi' (62'), huku bao la kufuatia machozi la Biashara likiwekwa kimiani na Daniel Manyenye (2'). #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh #UhaiDrinkingWater #TradegentsTanzaniaLimited



NAHODHA AZAM FC AAHIDI MATOKEO MAZURI | AZAM FC v BIASHARA UTD | TPL ROUND 24
NAHODHA AZAM FC AAHIDI MATOKEO MAZURI | AZAM FC v BIASHARA UTD | TPL ROUND 24

WAKATI zikiwa zimesalia siku mbili kabla ya Azam FC kumenyana na Biashara United, kikosi hicho kimejinasibu kuendelea kupata matokeo mazuri ili kufikia malengo yake. Mabingwa hao wa makombe mawili msimu huu baada ya kufanikiwa kutetea Kombe la Kagame na Mapinduzi Cup, wamekuwa kwenye mwenendo mzuri msimu huu hadi sasa ikishika nafasi ya pili kwenye za Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) ikiwa na pointi 44. Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz Nahodha wa Azam FC, Agrey Moris, amesema kuwa wanajua mchezo utakuwa mgumu lakini watajipanga vema kuweza kupata matokeo. “Biashara ni timu nzuri ukiangalia wamepata kocha mpya kwa vyovyote timu inayopata kocha mpya wachezaji wanakuwa wanajitolea mara mbili zaidi ya mwanzo ila kama sisi Azam siku zote tunajipanga kuhakikisha tunapata matokeo kwenye michezo yetu. “Kwa sababu hii ni ligi ni safari ndefu bila kushinda mechi inayokuja mbele huwezi ukafikia lengo, tumejipanga vizuri wachezaji wote wako vizuri tutahakikisha tunapata matokeo kwenye mchezo huo,” alisema mchezaji huyo wa muda mrefu wa Azam FC. Kihistoria timu hizo zimekutana mara moja tu kwenye ligi, tokea Biashara ipande kucheza Ligi Kuu msimu huu, ambapo mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Karume, mjini Musoma uliisha kwa suluhu. #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh #UhaiDrinkingWater #TradegentsTanzaniaLimited



Undani wa shangilia ya Messi vs Ruvu Shooting; Amtaja mwanaye
Undani wa shangilia ya Messi vs Ruvu Shooting; Amtaja mwanaye

MASHABIKI wengi wa soka wamekuwa wakiwa na maswali mengi kuhusu staili ya ushangiliaji ya winga Ramadhan Singano ‘Messi’, aliyofanya jana Alhamisi mara baada ya kufunga bao dhidi ya Ruvu Shooting. Singano akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz amesema kuwa ameshangilia bao kwa staili hiyo akimshukuru Mwenyezi Mungu baada ya kumjalia mke wake kupata mtoto wa kiume mwanzoni mwa wiki hii, akiwa ni mtoto wake wa kwanza kwenye maisha yake. “Staili yangu ni kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumjalia mke wangu kunipa mtoto wa kiume, shangilia ile ilikuwa inamaanisha herufi ya ‘Y’ jina la baba yangu Yahya na mtoto wangu nikimpa jina la Yahya Ramdhan Singano,” alisema winga wa Azam FC, Ramadhan Singano 'Messi'. #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh



TPL ROUND 14 | Azam FC 2-1 Ruvu Shooting | Match Highlights
TPL ROUND 14 | Azam FC 2-1 Ruvu Shooting | Match Highlights

KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imefanya kweli baada ya kuinyuka mabao 2-1 Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) uliomalizika kwenye Uwanja wa Azam Complex leo Alhamisi usiku. Ushindi huo unaihakikishia Azam FC nafasi ya kuendelea kubakia kileleni mwa msimamo wa ligi ikifikisha pointi 33 baada ya kushinda mechi 10 na sare tatu ikiwa haijapoteza mchezo hata mmoja.



Kagera vs Azam FC Post Match Press | Azam FC yajipanga kuendelea na moto TPL
Kagera vs Azam FC Post Match Press | Azam FC yajipanga kuendelea na moto TPL

BENCHI la ufundi la Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, limejipanga vilivyo kuwajenga wachezaji kisaikolojia na kisawasawa ili kuendelea na rekodi nzuri waliyoanza katika Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) msimu huu. Azam FC iliyoichapa Kagera Sugar leo bao 1-0 lililofungwa na Donald Ngoma, ipo kileleni kwa takribani wiki nne sasa ikifikisha jumla ya pointi 30 baada ya ushindi wa mechi tisa na sare tatu huku ikiwa haijapoteza mchezo hata mmoja. #AzamFCUnbeaten #AzamFCPopoteInakanyaga




« Previous Next »


User Detail Page

You can find user latest posts and related content on the page. Friends, comments for events / matches are also available on the page. Even you can find users who are same pleasure with current user.

#Travel, #SupportYourTeam, #AllAboutSports