MASHABIKI wengi wa soka wamekuwa wakiwa na maswali mengi kuhusu staili ya ushangiliaji ya winga Ramadhan Singano ‘Messi’, aliyofanya jana Alhamisi mara baada ya kufunga bao dhidi ya Ruvu Shooting. Singano akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz amesema kuwa ameshangilia bao kwa staili hiyo akimshukuru Mwenyezi Mungu baada ya kumjalia mke wake kupata mtoto wa kiume mwanzoni mwa wiki hii, akiwa ni mtoto wake wa kwanza kwenye maisha yake. “Staili yangu ni kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumjalia mke wangu kunipa mtoto wa kiume, shangilia ile ilikuwa inamaanisha herufi ya ‘Y’ jina la baba yangu Yahya na mtoto wangu nikimpa jina la Yahya Ramdhan Singano,” alisema winga wa Azam FC, Ramadhan Singano 'Messi'. #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh
KLABU ya Azam FC imeanza vema kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania (VPL) msimu 2020/2021 baada ya kuichapa Polisi Tanzania bao 1-0 kwenye mchezo wa kwanza. Bao pekee la Azam FC limewekwa kambani na mshambuliaji Obrey Chirwa, dakika ya 44 akiunganisha krosi safi ya mshambuliaji mpya, Prince Dube. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora #SARAFU #AzamUkwaju #AzamUbuyu #AzamStrawberry #UhaiDrinkingWater
#ObreyChirwa #IddNado #AzamFC #SingidaUnited Azam FC imeandika rekodi ya kwanza baada ya kupata ushindi mnono wa kihistoria kwenye mechi za mashindano, ikiichapa Singida United mabao 7-0, ukiwa ni mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL). Mabao ya Azam FC yalifungwa na Obrey Chirwa akifunga manne, Idd Seleman 'Nado', akifunga mawili huku jingine wakijifunga wenyewe Singida United. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora
KLABU ya Azam FC imeendelea pale ilipoishia kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) baada ya kuichapa Mbaoa mabao 2-0 jana Jumapili usiku. Mabao ya Azam FC yalifungwa na washambuliaji Richard Djodi na Shaaban Chilunda. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora
HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON
Kikosi cha Azam FC kimeendeleza wimbi la ushindi ugenini kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) kwa kupata ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Alliance. Mabao matatu ya Obrey Chirwa (hat-trick) na mawili ya Shaaban Chilunda, yalitosha kabisa kuihakikishia ushindi mwingine Azam FC mkoani Mwanza, ikifanikiwa kuvuna pointi zote sita. #ObreyChirwa #ShaabanChilunda #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora