Ngoma awaahidi makubwa mashabiki Azam FC | Ngoma First Action At Azam FC by @Azam FC - Post Details

Ngoma awaahidi makubwa mashabiki Azam FC | Ngoma First Action At Azam FC

BAADA ya jana kucheza mechi yake ya kwanza Azam FC akitokea kwenye majeruhi, mshambuliaji Donald Ngoma, ameonesha kufurahishwa sana huku akiwaahidi makubwa mashabiki wa timu hiyo. Azam FC iliyokuwa ikicheza na Lipuli jana usiku na kutoka suluhu, ilishuhudiwa Ngoma akiingia dakika ya 62 kuchukua nafasi ya kiungo mkabaji Mudathir Yahya, mchezo huo pia ukiwa ni wa kwanza kwake tokea asajiliwe na timu hiyo msimu huu akitokea Yanga. Licha ya kutoka kwenye majeraha ya takribani mwaka mmoja, Ngoma alionekana kuanza vema jana mechi yake ya kwanza akicheza kwa kujituma na kupambana na mabeki wa Lipuli huku akipata nafasi muhimu mbili za kufunga moja ikiwa ni ile ya kuangushwa katika eneo la hatari na kipa.

Similar Posts!

VPL Highlights | Azam FC 7-0 Singida United | Chirwa aandika rekodi
VPL Highlights | Azam FC 7-0 Singida United | Chirwa aandika rekodi

#ObreyChirwa #IddNado #AzamFC #SingidaUnited Azam FC imeandika rekodi ya kwanza baada ya kupata ushindi mnono wa kihistoria kwenye mechi za mashindano, ikiichapa Singida United mabao 7-0, ukiwa ni mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL). Mabao ya Azam FC yalifungwa na Obrey Chirwa akifunga manne, Idd Seleman 'Nado', akifunga mawili huku jingine wakijifunga wenyewe Singida United. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora



VPL HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-0 MBAO FC | DJODI, CHILUNDA WAFANYA MAMBO
VPL HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-0 MBAO FC | DJODI, CHILUNDA WAFANYA MAMBO

KLABU ya Azam FC imeendelea pale ilipoishia kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) baada ya kuichapa Mbaoa mabao 2-0 jana Jumapili usiku. Mabao ya Azam FC yalifungwa na washambuliaji Richard Djodi na Shaaban Chilunda. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora



HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON
HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON

HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON



AZAM FC INAJIPANGA VILIVYO KURUDIANA NA TRIANGLE, CHECHE ATAJA USHINDI TU
AZAM FC INAJIPANGA VILIVYO KURUDIANA NA TRIANGLE, CHECHE ATAJA USHINDI TU

"Vijana wamesikitika na wasikate tamaa, watuombee dua, watusapoti tutapambana kwa ajili yao na kwa ajili ya timu yetu na nchi yetu, mpira umeanza sehemu ya kwanza, tuseme kama kipindi cha kwanza kimeanza lakini tutahakikisha kipindi cha pili tunapambana kwao kwa hali na mali ili tuweze kurudi na ushindi," alisema Kocha Msaidizi wa Azam FC, Idd Nassor 'Cheche', akiwaambia mashabiki wa timu hiyo. #TimuBoraBidhaaBora #AzamFC #TriangleUnited #CAFConfederationCup



AZAM FC YAREJEA DAR IKITOKA KUINYOA MBEYA CITY
AZAM FC YAREJEA DAR IKITOKA KUINYOA MBEYA CITY

Kikosi cha Azam FC kimerejea leo mchana jijini Dar es Salaam kikitokea mkoani Mbeya, kikiwa safi kabisa baada ya jana kuichapa Mbeya City bao 1-0 lililofungwa na beki Yakubu Mohammed. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh #UhaiDrinkingWater #TradegentsTanzaniaLimited



TPL ROUND 20 | MBEYA CITY 0-1 AZAM FC | YAKUBU AFANYA MAMBO
TPL ROUND 20 | MBEYA CITY 0-1 AZAM FC | YAKUBU AFANYA MAMBO

KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imefanya kweli mkoani Mbeya baada ya kuichapa Mbeya City bao 1-0, mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) uliofanyika Uwanja wa Sokoine, Mbeya leo jumapili. Ushindi huo unaifanya Azam FC kufikisha jumla ya pointi 66 kwenye msimamo wa ligi ikiwa nafasi ya pili ikizidiwa pointi nane na kinara Yanga aliyekuwa nazo 74, Simba iliyocheza mechi 22 ni ya tatu ikijikusanyia 57. Beki wa Azam FC, Yakubu Mohammed, aliyeonekana kucheza vema kwenye eneo la beki ya kati sambamba na beki chipukizi kutoka Azam Academy, Lusajo Mwaikenda, ndiye aliyeipatia bao pekee timu hiyo dakika ya 45 akimalizia krosi iliyopigwa na kiungo, Mudathir Yahya, kufuatia mpira wa kona alioanzishiwa na Bruce Kangwa. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh #UhaiDrinkingWater #TradegentsTanzaniaLimited