Waziri Mwakyembe aimwagia sifa Azam FC; Asema ni Kiwanda cha Soka Tanzania by @Azam FC - Post Details

Waziri Mwakyembe aimwagia sifa Azam FC; Asema ni Kiwanda cha Soka Tanzania

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwankyembe, leo alifanya ziara ya kutembelea Makao Makuu ya Azam FC ‘Azam Complex’ na kukiri kuwa timu hiyo ni kiwanda cha soka nchini. Ziara hiyo ya Mwakyembe ilikuwa ni maalumu kwa ajili ya kuangalia Azam FC ilipofikia kwenye uboreshaji wa uwanja huo ikiwa ni maandalizi ya kuelekea fainali za Mataifa ya Afrika kwa Vijana chini ya umri wa miaka 17 (AFCON U-17) zitakazofanyika nchini mwakani. Uwanja wa Azam Complex ni miongoni mwa viwanja vitatu nchini vilivyoteuliwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kwa kushirikiana na la hapa nchini (TFF), vingine viwili vikiwa ni Uwanja wa Taifa na ule wa Uhuru. Kigogo huyo aliambatana na Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Taifa (BMT), Alex Nkeyenge na Mkurugenzi wa Mashindano TFF, Salum Madadi, ambao walikaribishwa na wenyeji wao akiwemo Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Wakurugenzi, Nassor Idrissa ‘Father’, Makamu Mwenyekiti Omary Kuwe, Meneja wa timu, Philllip Alando. Akitoa neno kwenye ziara hiyo, Waziri Mwakyembe, aliupongeza uongozi wa Azam FC kwa kazi kubwa waliyofanya kwenye kuboresha uwanja huo kwa ajili ya fainali hizo ambazo zitafanyika kwa mara ya kwanza nchini. “Kwa kweli ni mara yangu ya kwanza kutembelea Azam Complex na nimejiridhisha mwenyewe kwamba hiki ni kiwanda cha soka, kiwanda cha michezo kuna kila kitu hapa na tukifikia hatua ambayo pengine timu zetu zenye sura ya Kitaifa hata zikawa tatu, nne, tano zikawa na mfumo ulioko hapa Azam Complex tayari sisi Tanzania tumeshakuwa nchi ya soka. “Na nadhani tutaanza kuuza wachezaji wengi sana duniani ambao pia watachangia sana katika pato la Taifa maana wenzetu wengi kama nchi ya Brazil inaendeshwa na pesa kama hiyo, Azam hongereni sana mmefanya kazi kubwa sana,” alisema.

Similar Posts!

VPL Highlights | Azam FC 7-0 Singida United | Chirwa aandika rekodi
VPL Highlights | Azam FC 7-0 Singida United | Chirwa aandika rekodi

#ObreyChirwa #IddNado #AzamFC #SingidaUnited Azam FC imeandika rekodi ya kwanza baada ya kupata ushindi mnono wa kihistoria kwenye mechi za mashindano, ikiichapa Singida United mabao 7-0, ukiwa ni mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL). Mabao ya Azam FC yalifungwa na Obrey Chirwa akifunga manne, Idd Seleman 'Nado', akifunga mawili huku jingine wakijifunga wenyewe Singida United. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora



VPL HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-0 MBAO FC | DJODI, CHILUNDA WAFANYA MAMBO
VPL HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-0 MBAO FC | DJODI, CHILUNDA WAFANYA MAMBO

KLABU ya Azam FC imeendelea pale ilipoishia kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) baada ya kuichapa Mbaoa mabao 2-0 jana Jumapili usiku. Mabao ya Azam FC yalifungwa na washambuliaji Richard Djodi na Shaaban Chilunda. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora



HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON
HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON

HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON



AZAM FC INAJIPANGA VILIVYO KURUDIANA NA TRIANGLE, CHECHE ATAJA USHINDI TU
AZAM FC INAJIPANGA VILIVYO KURUDIANA NA TRIANGLE, CHECHE ATAJA USHINDI TU

"Vijana wamesikitika na wasikate tamaa, watuombee dua, watusapoti tutapambana kwa ajili yao na kwa ajili ya timu yetu na nchi yetu, mpira umeanza sehemu ya kwanza, tuseme kama kipindi cha kwanza kimeanza lakini tutahakikisha kipindi cha pili tunapambana kwao kwa hali na mali ili tuweze kurudi na ushindi," alisema Kocha Msaidizi wa Azam FC, Idd Nassor 'Cheche', akiwaambia mashabiki wa timu hiyo. #TimuBoraBidhaaBora #AzamFC #TriangleUnited #CAFConfederationCup



AZAM FC YAREJEA DAR IKITOKA KUINYOA MBEYA CITY
AZAM FC YAREJEA DAR IKITOKA KUINYOA MBEYA CITY

Kikosi cha Azam FC kimerejea leo mchana jijini Dar es Salaam kikitokea mkoani Mbeya, kikiwa safi kabisa baada ya jana kuichapa Mbeya City bao 1-0 lililofungwa na beki Yakubu Mohammed. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh #UhaiDrinkingWater #TradegentsTanzaniaLimited



TPL ROUND 20 | MBEYA CITY 0-1 AZAM FC | YAKUBU AFANYA MAMBO
TPL ROUND 20 | MBEYA CITY 0-1 AZAM FC | YAKUBU AFANYA MAMBO

KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imefanya kweli mkoani Mbeya baada ya kuichapa Mbeya City bao 1-0, mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) uliofanyika Uwanja wa Sokoine, Mbeya leo jumapili. Ushindi huo unaifanya Azam FC kufikisha jumla ya pointi 66 kwenye msimamo wa ligi ikiwa nafasi ya pili ikizidiwa pointi nane na kinara Yanga aliyekuwa nazo 74, Simba iliyocheza mechi 22 ni ya tatu ikijikusanyia 57. Beki wa Azam FC, Yakubu Mohammed, aliyeonekana kucheza vema kwenye eneo la beki ya kati sambamba na beki chipukizi kutoka Azam Academy, Lusajo Mwaikenda, ndiye aliyeipatia bao pekee timu hiyo dakika ya 45 akimalizia krosi iliyopigwa na kiungo, Mudathir Yahya, kufuatia mpira wa kona alioanzishiwa na Bruce Kangwa. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh #UhaiDrinkingWater #TradegentsTanzaniaLimited