MAGOLI YOTE: MTIBWA SUGAR 3-1 COASTAL UNION (TPL - 26/02/2019)
MAGOLI YOTE: MTIBWA SUGAR 3-1 COASTAL UNION (TPL - 26/02/2019)

Hatimaye wakata miwa wa Mtibwa, timu ya Mtibwa Sugar wamepata ushindi wa kwanza baada ya takriban mechi nane za ligi kuu Tanzania Bara, wakiichapa Coastal Union mabao 3-1 kwenye uwanja wa Manungu, mkoani Morogoro. Coastal ndiyo waliotangulia kupata bao kupitia kwa Ayoub Lyanga dakika ya 21, lakini wenyeji Mtibwa wakasawazisha kupitia kwa Dickson Daud dakika ya 40, kabla ya Jaffary Kibaya kupachika bao la pili dakika ya 55 na Riphat Khamis dakika ya 67. Ushindi huo umeifanya Mtibwa ipande juu kwa nafasi sita kutoka nafasi ya 17 hadi ya 11 baada ya kufikisha pointi 32.



MTIBWA SUGAR 1-1 AFRICAN LYON; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 08/02/2019)
MTIBWA SUGAR 1-1 AFRICAN LYON; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 08/02/2019)

Goli la dakika ya mwisho ya mchezo limeiokoa Mtibwa Sugar kwa kuipa sare ya bao 1-1 dhidi ya African Lyon katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa manungu Complex, mkoani Morogoro. Bao hilo la kusawazisha limefungwa na Jaffary Salum Kibaya akimalizia kwa kichwa kona iliyochongwa na Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ baada ya wageni katika mchezo huo African Lyon kutangulia kupata bao dakika ya 62 kupitia kwa mkongwe Ramadhan Chombo Redondo. Matokeo hayo yameipandisha Mtibwa kutoka nafasi ya 13 hadi nafasi ya 10 ikifikisha pointi 30 katika michezo 21 huku African Lyon ikiendelea kusalia mkiani na licha ya kufikisha pointi 20 baada ya kucheza michezo 25.



MTIBWA SUGAR 1-2 KCCA: HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (CAF CC - 22/12/2018)
MTIBWA SUGAR 1-2 KCCA: HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (CAF CC - 22/12/2018)

Timu ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro, imetupwa nje ya michuano wa Kombe la Shirikisho Afrika baada ya leo kuchapwa 2-1 na KCCA ya Uganda katika mchezo wa maruadiano uliopigwa kwenye Dimba la Chamazi Dar es Salaam. Kwenye mchezo huo, KCCA ndiyo waliotangulia kupata bao dakika ya 28 kupitia kwa Muzamiru Mutyaba kabla ya Salum Kihimbwa kusawazisha dakika ya 51, na kisha wageni hao kutoka Jijini Kampala Uganda kupata bao la pili dakika ya 87 kupitia kwa Allan Okello. Katika mchezo wa kwanza uliopigwa Jijini Kampala nchini Uganda, KCCA ilipata ushindi wa mabao 3-0, na hivyo inafuzu kuingia hatua ya mtoano kwa jumla ya magoli 5-1, huku Mtibwa ambayo hii ilikuwa ni mara yake ya kwanza kushiriki michuano ya CAF tangu mwaka 2002, ikifungashiwa virago.



MTIBWA SUGAR 4-0 NORTHERN DYANAMO HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (CAF CC - 27/11/2018)
MTIBWA SUGAR 4-0 NORTHERN DYANAMO HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (CAF CC - 27/11/2018)

Timu ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro imeanza vyema michuano ya Afrika kwa kuichapa Northern Dynamo mabao 4-0 katika mchezo wa hatua ya awali wa Kombe la Shirikisho barani Afrika. Katika mchezo huo uliopigwa kwenye Dimba la Azam Complex Chamazi, mshambuliaji wa Mtibwa Jaffary Salum Kibaya ameibuka shujaa kwa kupigwa hat-trick, akifunga mabao yake katika dakika za 13, 36 na 58 huku bao la nne likifungwa na Riphat Khamis aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Ismail Mhesa. Kwa matokeo haya, mtibwa wamejiweka pazuri katika njia kusonga mbele kwani watahitaji sare ya aina yoyote ili kufuzu hatua inayofuata au wasifungwe mabao zaidi ya matatu.



MAGOLI: MTIBWA SUGAR 4-0 NORTHERN DYANAMO (CAF Conf. Cup - 27/11/2018)
MAGOLI: MTIBWA SUGAR 4-0 NORTHERN DYANAMO (CAF Conf. Cup - 27/11/2018)

Timu ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro imeanza vyema michuano ya Afrika kwa kuichapa Northern Dynamo mabao 4-0 katika mchezo wa hatua ya awali wa Kombe la Shirikisho barani Afrika. Katika mchezo huo uliopigwa kwenye Dimba la Azam Complex Chamazi, mshambuliaji wa Mtibwa Jaffary Salum Kibaya ameibuka shujaa kwa kupigwa hat-trick, akifunga mabao yake katika dakika za 13, 36 na 58 huku bao la nne likifungwa na Riphat Khamis aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Ismail Mhesa. Kwa matokeo haya, mtibwa wamejiweka pazuri katika njia kusonga mbele kwani watahitaji sare ya aina yoyote ili kufuzu hatua inayofuata au wasifungwe mabao zaidi ya matatu.



Mtibwa Sugar 2-1 Mbeya City: Walichozungumza makocha na wachezaji (TPL 01/09/2018)
Mtibwa Sugar 2-1 Mbeya City: Walichozungumza makocha na wachezaji (TPL 01/09/2018)

Timu ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro imeendeleza ushindi katika dimba lake la nyumbani la Manungu baada ya leo kuifunga Mbeya City mabao 2-1 kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL). Mara baada ya mchezo huo, Azam TV imezungumza na makocha wa timu zote mbili Ramadhan Swanzurimo wa Mbeya City na Zuberi Katwila wa Mtibwa Sugar, wote wameeleza sababu za kitaalamu za matokeo hayo. Pia Azam TV imezungumza na baadhi ya wachezaji waliong’ara kwenye mchezo huo, Stamili Mbonde ambaye ni mfungaji wa bao la kwanza la Mtibwa, Ismail Aidan Mhesa ambaye ni mfungaji wa bao la pili la Mtibwa na Eric Kyaruzi ambaye ni mfungaji wa bao pekee la Mbeya City.



Haya hapa magoli yote Mtibwa Sugar ikiichapa Mbeya City 2-1 Manungu (TPL 01/09/2018)
Haya hapa magoli yote Mtibwa Sugar ikiichapa Mbeya City 2-1 Manungu (TPL 01/09/2018)

Timu ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro imeendeleza ushindi katika dimba lake la nyumbani la Manungu baada ya leo kuifunga Mbeya City mabao 2-1 kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL). Katika mchezo huo ambao timu zote zimeonesha uwezo unaokaribiana, Mtbwa ndiyo waliotangulia kupata mabao kupitia kwa Stamili Mbonde dakika ya 9 na Ismail Mhesa dakika ya 42 huku Mbeya City walioonesha uhai zaidi kipindi cha pili wakipata bao lao dakika y 48 ya mchezo kupitia kwa Eric Kyaruzi. Haya hapa mabao yote yaliyofungwa kwenye mchezo huo.




« Previous Next »


Popular Tags

#Best Goals  #Michael Jordan  #Paul Pogba  #New York Knicks  #James Harden  #Lionel Messi  #Counter Attack Goals Football  #Goal Celebrations  #Gareth Bale  #Gareth Bale  

Popular Users

#DanicaPatrick  #Buster_ESPN  #instagram  #DeAndre  #RealSkipBayless  #TheChristinaKim  #KingJames  #blakegriffin23  #JayBilas  #StephenCurry30  #nyt4thdownbot  #GNev2  #KDTrey5  #floydmayweather