SPOTI HINTS: OKWI, JUUKO OUT! AFRICAN LYON VS SIMBA LIGI Kuu Tanzania Bara inaendelea tena leo kwa michezo mbalimbali kupigwa katika viwanja Tofauti ikiwemo Mechi kati yaAfrican Lyon dhidi ya Simba katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha huku Kocha Mkuu Patrick Aussems akithibitisha kuwakosa wachezaji wake Emmanuel Okwi na Juuko Murshid. Lakini pia gumzo ambalo lilikuwa likiendelea katika mitandao ya kijamii ikimuhusu Beki Mkongwe Kelvin Yondani kutompa mkono Nahodha wake Ibrahim Ajibu leo wanayanga wameamua kuonyesha video ambayo inawaonyesha wako sawa huku wakikimbizana katika kambi yao waliyoweka jijini Mwanza wakijiandaa na mchezo wao dhidi ya Mbao FC. #OKWI #JUUKO https://www.youtube.com/watch?v=N1X-f... Watch More Videos here: https://goo.gl/GvVdZw Watch More Videos here: https://goo.gl/ae33fL Website: www.globalpublishers.co.tz FaceBook: www.facebook.com/globalpublishers Instagram: www.instagram.com/globalpublishers Twitter: www.twitter.com/GlobalHabari Install Global App: ANDROID: https://goo.gl/QvT6RV Install Global App: iOS: https://goo.gl/2jDyho
SUBSCRIBE HAPA https://www.youtube.com/channel/UC_m6Lmu4NexLFzafJH5InYA?view_as=subscriber tembelea WEBSITE YETU https://bmtvtanzania.com/ INSTAGRAM https://www.instagram.com/bmtvtanzania FACEBOOK https://www.facebook.com/bmtvtanzania TWITTER https://twitter.com/bmtvtanzania1
Mbao FC imepata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Katika mchezo huo uliokuwa mkali, Mbao wamepata bao hilo dakika ya 33 kupitia kwa Raphael Siame dakika 33.
#LigiKuuTanzaniaBara #MbaoFcVsCoastalUnion #LipuliVsAzamFc #africanlyionvsRuvushooting #MwaduifcVsKagera sugar #NdandaFcvsMtibwaSugar #TZprisonsvsStand United
Coastal Union imefanikiwa kuchukua pointi tatu ugenini kwa kuichapa Mbao FC bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Licha ya Mbao kumiliki zaidi mpira na kufanya mashambulizi mengi langoni kwa Coastal, nafasi pekee aliyoipata Raizin Hafidh dakika ya 60 aliitumia na kuipatia Coastal bao pekee lililoipa alama tatu ugenini
Coastal Union imefanikiwa kuchukua pointi tatu ugenini kwa kuichapa Mbao FC bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Licha ya Mbao kumiliki zaidi mpira na kufanya mashambulizi mengi langoni kwa Coastal, nafasi pekee aliyoipata Raizin Hafidh dakika ya 60 aliitumia na kuipatia Coastal bao pekee lililoipa alama tatu ugenini.
Tanzania Prisons imepata ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa Februari 6, 2019 kwenye Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Magoli ya Wenyeji hao wa mchezo yamefungwa na Salum kKimenya dakika ya 12 na Adam Adam dakika ya 20 huku Mbao wakipata bao lao kwa mpira wa adhabu ndogo dakika ya 34 kupitia kwa Amosi Charles. Baada ya mchezo huo makocha wa timu zote mbili wakazungumza ambapo Kocha wa Tanzania Prisons Adolf Rishard amewapongeza wachezaji wake wa ushindi huku akitaja mvua kuwa kikwazo kwa upande wao, wao kocha wa Mbao FC Ally Bushiri akilalamikia hali ya uwanja kuwa sababu ya wao kupoteza mchezo. Tazama magoli na mahojiano
Timu ya Alliance FC imepata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Lipuli FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa kwenye Dimba la Nyamagana jijini Mwanza. Magoli ya Alliance yote mawili yamepatikana kipindi cha kwanza kupitia kwa Dickson Ambundo dakika ya 9 na Juma Nyange dakika ya 30. Ushindi huo umeifanya Alliance kusogea hadi nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi ikifikisha pointi 31 nyuma ya Mbao FC na Lipuli FC ambao wote wana pointi 33.