Wananchi wamefika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kumpokea msanii kutoka kundi la KKL BOMOKO nchini Congo DR anayetamba na kibao cha "Tabulele", kwa ajili ya hamasa kuelekea mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, @yangasc dhidi ya Al Ahly siku ya Novemba 2, 2023, Uwanja wa Benjamin Mkapa. Baada ya kusubiri sana hatimaye Mwamba ndani ya nyumba, ndani ya Jiji kubwa la Kibiashara la Dar Es Salaam, anasema Yanga kwake ni zaidi ya timu, imempa thamani kubwa.
NIFUATE 2023: Team Samatta chini ya mwanandinga Mbwana Samatta imeendeleza ubabe dhidi ya Team Kiba iliyo chini ya msanii Alikiba kwa kupata ushindi wa mabao 4-2 katika mchezo wa hisani chini ya #SamakibaFoundation uliopigwa leo kwenye Dimba la Azam Complex, Chamazi. Abdul Suleiman Sopu amepiga #hattrick dakika ya 45', 63' na 71 huku goli lingine likifungwa na John Bocco aliyefungua mlango wa magoli dakika ya 21. Magoli ya Team Kiba yametoka kwa Ayoub Lyanga 69 na Msanii wa bongo fleva, Mario dakika ya 90'+4. Haya hapa magoli... #Nifuate2023 #NifuateDay #SamakibaFoundation #SAMAKIBA #TeamSamatta #TeamKiba #UpendoWaZambarau #SamattaFriends #AlikibaFriends #UpendoWaZambarau
Msanii wa bongofleva Tunda man amejigamba akisema hakuna kama simba afika baada ya ushindi wa 3;1 dhidi ya Singida Big ...
SAMAKIBA 2022: Team Kiba iliyo chini ya msanii Alikiba imebeba Kombe la Nifuate 2022 kwa kuichapa Team Samatta iliyo chini ya nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta kwa mikwaju ya penati 4-2 kufuatia sare ya mabao 3-3. Katika muda wa kawaida, magoli ya Team Kiba yamefungwa na Saimon Msuva aliyefunga mawili pamoja na Alikiba mwenyewe kwa penati huku magoli ya Team Samatta ayakifungwa na Kelvin John, Mbwana Samatta na Idd Gamba kwa penati. Mechi hii ni tamasha maalum la hisani kwa ajili ya kurejesha jamii ambalo hufanyika kila mwaka chini ya taasisi ya Samakiba Foundation, na mwaka huu limefanyika kwenye Dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, na kushuhudia Team Kiba wakibeba ndoo.
Vita ya Alama Tatu Inashuhudiwa Uwanja wa Benjamin Mkapa Dar es Saalam Baina ya Simba SC dhidi ya Kagera Sugar Majira ...
Sahabiki na Msanii wa Tasnia ya Uchekeshaji Steve 'Nyerere' akitoa maoni kuhusiana na mchezo wa Simba dhidi ya Yanga ...
Mpenja TV tumefanya mahojiano na Msanii wa Vichekesho nchini, Haji Salum maarufu MBOTO ambaye ni shabiki kindakindaki wa Yanga SC. Mboto amemwaga tambo nyingine kuelekea Derby ya watani wa Jadi Jumamosi Novemba 11, 2021, uwanja wa Benjamin Mkapa. #Mboto #SimbaVsYanga #NBCPremierLeague #MpenjaTV
Ni Msanii kutokea Bongo Flevani Marioo ambae anatoka burudani katika kilele cha wiki ya Simba SC yaani Simba DAY kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.