SAMAKIBA 2022: Team Kiba iliyo chini ya msanii Alikiba imebeba Kombe la Nifuate 2022 kwa kuichapa Team Samatta iliyo chini ya nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta kwa mikwaju ya penati 4-2 kufuatia sare ya mabao 3-3. Katika muda wa kawaida, magoli ya Team Kiba yamefungwa na Saimon Msuva aliyefunga mawili pamoja na Alikiba mwenyewe kwa penati huku magoli ya Team Samatta ayakifungwa na Kelvin John, Mbwana Samatta na Idd Gamba kwa penati. Mechi hii ni tamasha maalum la hisani kwa ajili ya kurejesha jamii ambalo hufanyika kila mwaka chini ya taasisi ya Samakiba Foundation, na mwaka huu limefanyika kwenye Dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, na kushuhudia Team Kiba wakibeba ndoo.
Simba SC imenyakua Kombe la Shirikisho la CRDB Bank kwa kuichapa Azam FC bao 1-0 katika mchezo wa fainali uliopigwa kwenye Dimba la Gombani Pemba. Goli pekee la ubingwa limefungwa Yahya Zayd ambaye amejifunga dakika ya 62.
Yanga SC imehitimisha msimu wa Ligi Kuuya NBC 2025/26 kwa kishindo, ikiichapa JKT Tanzania mabao 3-0 kwenye Dimba la Meja Jenerali Isamuhyo na kutwaa ubingwa wa tano mfululizo. Magoli yamefungwa na Prince Dube, Maxi Nzengeli na Laurindo Dilson Maria Depu.
Allan Okello 'Star Boy', amepiga magoli yote matatu #Hattrick , Yanga ikishinda 3-0 dhidi ya TRA United, mchezo wa raundi ya 29, Ligi Kuu ya NBC, uliopigwa KMC Complex, Dar es Salaam. Haya hapa magoli yote.
Yanga SC imezidi kuusogelea ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu, kwa kuwachapa Azam FC mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Amaan Zanzibar. Magoli ya Yanga yamefungwa na Ibrahim Abdullah 'Bacca', Laurindo Dilson Depu, na Pacome Zouzoua. Hii ni Ligi Kuu ya NBC, raundi ya 28 (bado mbili tu) Tazama highlights
Yanga SC imezidi kuusogelea ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu, kwa kuwachapa Azam FC mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Amaan Zanzibar. Magoli ya Yanga yamefungwa na Ibrahim Abdullah 'Bacca', Laurindo Dilson Depu, na Pacome Zouzoua. Haya hapa magoli yote...
Mnyama Simba ametinga fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank kwa kuichapa Coastal Union mabao 4-0 katika mchezo mchezo wa nusu fainali uliopigwa kwenye Dimba la Sheikh Amri Abeid, Arusha. Magoli ya mchezo huu yamefungwa na Libase Gueye, Nickson Kibabage, Rushine de Reuck kwa penati na Clatous Chama.
Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo kati ya Simba SC dhidi ya Mbeya City ambapo Elie Mpanzu ndio amepeleka alama tatu unyamani. Simba imeshinda kwa goli 1-0 ndani ya dimba la Sokoine jijini Mbeya
#NBCPL: Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mechi ya NBC Premier League kati ya Simba SC dhidi ya Pamba Jiji FT: Simba SC 2-1 Pamba Jiji Magoli ya Simba yamefungwa na Elie Mpanzu na Libasse Gueye huku goli la Pamba Jiji likifungwa na Mathew Momanyi. #NBCPL #NBCPremierLeague #LigiKuuTanzania #ImenogaZaidi #SimbaVsPambaJiji #SimbaSC #PambaJiji #SimbaPamba