Ni mchezo wa ufunguzi ulioshuhudia Simba ikitoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya mabingwa wa Afrika, Al Ahly kwenye Dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Magoli ya Simba yamefungwa na Kibu Denis dakika ya 53, na Sadio Kanoute dakika ya 59 huku magoli ya Al Ahly yakifungwa na Reda Slim (45'+1) na Mahamoud Karahba dakika ya 63.
Simba SC imeendeleza ushindi katika mchezo wa tano mfululizo, ikiitandika Singida Big Stars mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Liti, mkoani Singida. Magoli ya Simba yametoka kwa Saidi ntibazonkiza dakika ya 26 na Moses Phiri dakika ya 83 huku goli la Singida likitokea kwa Deus Kaseke dakika ya 52.
Simba SC imepata sare ya bao 1-1 dhidi ya Power Dynamos na kufuzu hatua ya makundi barani Afrika kwa faida ya goli la ugenini. Hii ni kufuatia sar ya mabao 2-2 katika mchezo wa kwanza uliochezwa nchini Zambia na kufanya matokeo ya jumla yawe sare ya mabao 3-3. Katika mchezo wa leo, magoli yote yamefungwa na wachezaji wa Power Dynamos wakianza dakika ya 16 kupitia kwa Andy Boyeli na kisha kujifunga dakika ya 68 kupitia kwa Kondwani Chiboni.
Hivi sasa hatuwaangalii wapinzani wetu nini wanafanya, badala yake tunaelekeza nguvu zetu katika maandalizi ya kikosi chetu. Mabao mawili tuliyoyapata kule ugenini yatatusaidia hapa na wao yaliwaumiza lakini tunaporudi nyumbani hatutakiwi kuzubaa. -- Dar24 ni chanzo namba moja cha habari kwa watanzania mahali popote walipo duniani. Kwa habari za uhakika kutoka nyanja mbali mbali. JE, NA WEWE UNA HABARI? ⚫️ WASILIANA NA DAR24 MEDIA: +255 679 979 786 ⚫️ Email: dar24newsroom@gmail.com ⚫️ Website: www.dar24.com ⚫️ Instagram: @Dar24news ⚫️ Facebook: @dar24 ⚫️ Twitter: @Dar24News #simbasc #zambia #tanzania
KUFUZU AFCON WANAWAKE: Timu ya Taifa ya Wanawake, #TwigaStars imeitupa nje Ivory Coast kwa mikwaju ya penati 4-2 baada ya kupindua matokeo ya 2-0 na kufanya matokeo ya jumla kuwa 2-2. Ni katika mchezo wa marudiano kuwania tiketi ya kufuzu AFCON kwa Wanawake #WAFCON uliopigwa leo kwenye Dimba la Azam Complex, Chamazi. Kwenye mchezo huo, Twiga Stars imepata mabao yake kupitia kwa Donisia Minja dakika ya 50 na Opah Clement dakika ya 52 kabla ya kenda kwenye matuta.... Haya hapa magoli mawili na mikwaju yote tisa ya penati.
Tabora United (Kitayosce) imeishushia kipigo cha mabao 3-1 Tanzania Prisons, mchezo wa #NBCPremierLeague uliopigwa kwenye Dimba la Ali Hassan Mwinyi, Tabora...... Magoli mawili ni kutoka kwa John Ben Nakibinge dakika ya 42 na 90 , na moja la Eric Okutu , huku Tanzania Prisons wakipata bao la kutoka kwa Samson Mbangula dakika moja tu baada ya kuingia akitokea benchi.
https://www.youtube.com/@Wasafi_Media?sub_confirmation=1 WATCH WASAFI TV📺 AZAM - 411 | DSTV - 296 | ZUKU - 028 | STAR TIMES - 444 & 333 | COCONUT TV - 20 | DODOMA CABLE - 113 LISTEN WASAFI FM 📻 88.9 DAR/ZNZ/PWANI 📻 | 104.1 DODOMA 📻 | 94.5 ARUSHA 📻 | 97.3 MBEYA 📻 | 94.9 MWANZA 📻 | SHINYANGA 106.3 📻 | KIGOMA 101.7 📻 Follow Us On: INSTAGRAM: http://instagram.com/wasafitv || http://instagram.com/wasafifm/ TWITTER: https://twitter.com/wasafitv || https://twitter.com/wasafifm/ FACEBOOK: https://www.facebook.com/wasafitv/ 𝑪𝒐𝒑𝒚𝒓𝒊𝒈𝒉𝒕 ©2021 𝑾𝒂𝒔𝒂𝒇𝒊 𝑴𝒆𝒅𝒊𝒂. 𝑨𝒍𝒍 𝒓𝒊𝒈𝒉𝒕𝒔 𝒓𝒆𝒔𝒆𝒓𝒗𝒆𝒅. #wasafi #wasafitv #wasafifm
YANGA vs JKT: Yanga SC imeichakaza JKT Tanzania mabao 5-0 katika mchezo wa ligi kuu ya NBC uliopigwa kwenye Dimba la Azam Complex, Chamazi....... Magoli ya Yanga kwenye mchezo huu yametoka kwa Stephane Aziz Ki kwa free kick dakika ya 45+5, Kenedy Musonda dakika ya 54, Yao Kouassi dakika ya 64 na Max Nzengeli aliyefunga mawili dakika ya 79 na 88. Haya hapa magoli yote......