UD SONGO Wamfanyia Kitu Mbaya CHAMA ,simba, “Katika mchezo huo Chama hakufanikiwa kufanya vizuri "
UD SONGO Wamfanyia Kitu Mbaya CHAMA ,simba, “Katika mchezo huo Chama hakufanikiwa kufanya vizuri "

#chama #simbasc #udsongo KIUNGO wa Simba raia wa Zambia, Clatous Chama, Jumamosi iliyopita ilikumbana na balaa katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya UD Songo uliofanyika nchini Msumbiji.   Katika mchezo huo, Chama anadaiwa kupewa ulinzi mkali na wapinzani ili kuhakikisha hapati nafasi ya kuanzisha mashambulizi kama ambavyo alikuwa akifanya katika michuano hiyo msimu uliopita.   Akizungumza na DREAM ONLINE TV mmoja wa wachezaji wa Simba ambaye hakutaka kutajwa jina lake alisema kuwa, kama Chama katika mchezo huo angekuwa sawa basi wangepata ushindi.   “Tunamshukuru Mungu tumerudi salama japokuwa hatukupata ushindi lakini kazi ilifanyika, pia wapinzani wetu walijitahidi sana kuzijua mbinu zetu ambazo tumekuwa tukizitumia kupata ushindi.   “Katika mchezo huo Chama hakufanikiwa kufanya vizuri kutokana na ulinzi mkubwa aliokuwa amewekewa na wapinzani wetu hao, kwani kila alivyokuwa akishika mpira tayari kuna watu wawili wanamzunguka jambo ambalo lilisababisha asifanye vizuri kama tulivyotarajia.   “Hata hivyo ni matumaini yetu ni kuwa kocha atakuwa ameliona hilo na atalifanyia kazi ili katika mchezo wa marudiano tutakaocheza hapa nchini tuweze kupata ushindi,” alisema mchezaji huyo.   Alipoulizwa Kocha Mkuu wa Simba, Mbelgiji, Patrick Aussems alisema: “Mchezo huo ulikuwa wa wazi na tulikuwa tukishambuliana kwa zamu na zaidi wapinzani wetu walijitahidi sana kuhakikisha wanadhibiti sehemu yetu ya kiungo ili viungo wetu wasipate nafasi ya kutengeneza nafasi za kufunga, hata hivyo katika mchezo wa marudiano tutahakikisha tunafanya vizuri katika uwanja wetu wa nyumbani.”



KOCHA SIMBA AZIDI KUWA MBOGO CAF
KOCHA SIMBA AZIDI KUWA MBOGO CAF

IKICHEZA kwa kujiamini na mbinu za hali ya juu, juzi Jumamosi Simba ililazimisha suluhu ugenini dhidi ya wenyeji, UD Songo ya Msumbiji. Katika mechi hiyo iliyochezwa mjini Beira, Kocha wa Simba, Patrick Aussems alisisitiza kwamba; “Tunakwenda kumaliza kazi Dar.” Simba iliandika rekodi ndani ya msimu mpya baada ya kutoruhusu bao lolote ikianzia mashindano hayo makubwa ugenini. Msimu uliopita kwenye hatua ya awali Simba ilianzia nyumbani dhidi ya Mbabane ikashinda 4-1, ugenini ikashinda mabao 4-0. Baada ya hapo katika mechi zote ilizocheza ugenini ikaruhusu mabao mengi. Katika mchezo wa jana Simba ilionekana kucheza kwa kujiamini huku safu ya ulinzi ikifanya kazi ya ziada. Ndani ya dakika 45 za kwanza Simba ilipiga mashuti matatu ambayo hayakuwa na madhara lakini mengine mawili nusura yawaamshe mashabiki kwani kipa alipangua yakawa kona. Wekundu hao walipata kona nne za haraka huku wakionekana kutawala zaidi eneo la katikati na kuwalazimisha wenyeji kupiga pasi ndefu ambazo hata hivyo walionyesha udhaifu mkubwa kwenye umaliziaji kwani walikuwa wakipaisha au kupiga pasi fyongo ambazo zilikuwa mboga kwa Benno Kakolanya. UD Songo walicheza mpira wa kuvizia kipindi cha pili lakini wakadhibitiwa na Nyoni na Wawa ambao walionekana kujiamini. Shiboub ambaye ni raia wa Sudan katika mechi jana alitawala kiungo na kuziba mianya mingi ya wenyeji kuwafikia mabeki wa Simba. Mkude muda mwingi alikuwa akiinasa mipira, kuidhibiti na kumpa Chama ambaye kazi yake ilikuwa kusambaza tu. Kwa mujibu wa kocha na viongozi wa Simba, uwanja uliochezwa mechi hiyo wa Campo Do Ferroviario Da Beira ulikuwa chakavu sana na haukuruhusu kucheza kiwango chao ingawa suluhu bado inawabeba. Aussems alisisitiza kwamba wana nafasi kubwa ya kushinda Dar es Salaam kwenye mechi ya marudiano na kusonga mbele na hawana wasiwasi. “Ulikuwa mchezo wa wazi, walikuwa wakijaribu kufunga na kwetu ilikuwa hivyo, jambo muhimu hatujaruhusu goli. Mchezo wa marudiano utakaochezwa Dar ni muhimu, kwa ushangiliaji wa mashabiki wetu na uwanja mzuri nafikiri tutafanya vizuri,” alisema Kocha Aussems.



SIMBA SC 0-0 AZAM FC; FULL HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 13/05/2019)
SIMBA SC 0-0 AZAM FC; FULL HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 13/05/2019)

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara Simba SC wameng’ang’aniwa kwenye Uwanja wa Uhuru kwa kulazimishwa sare ya bila kufungana na Azam FC. Timu zote zilionesha soka la kiwango cha juu ambapo Simba walifanya mashambulizi mengi zaidi langoni kwa Azam lakini walishindwa kupata bao kutokana na uimara wa safu ya ulinzi ya Azam iliyokuwa chini ya Agrey Moris na Yakubu Mohamed. Licha ya kushambuliwa zaidi, Azam walipoteza nafasi mbili za wazi kupitia kwa Donald Ngoma dakika ya 29 na Obrey Chirwa dakika ya 87, hivyo mchezo kumalizika kwa suluhu. Matokeo hayo yanaifanya Simba kubakiza pointi nane pekee ili kutetea taji lake, ikiwa imefikisha pointi 82 na mechi tano mkononi, wakati wapinzani wao wa karibu, Yanga wakiwa na pointi 81 na mechi tatu mkononi. Azam wao wanaendelea kukaa nafasi ya tatu wakifikisha pointi 69 na mechi mbili mkononi.



SIMBA SC 1-0 JKT TANZANIA; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 30/4/2019)
SIMBA SC 1-0 JKT TANZANIA; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 30/4/2019)

Bao pekee la Hassan Dilunga likifungwa dakika za majeruh, limetosha kuipa Simba pointi tatu muhimu dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) uliopigwa leo kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Dilunga amefunga goli hilo akimalizia pasi ya Emmanuel Okwi wakati zikiwa zimebaki sekunde chache mpira kumalizika katika mechi ngumu na ya ushindani wa aina yake. JKT walionekana wagumu zaidi hasa katika safu yao ya ulinzi iliyoweza kudhibiti mashambulizi makali ya Simba hadi ilipofika dakika ya 90 kabla ya dakika saba kuongezwa lakini Dilunga akafanikiwa kufunga bao hilo kwenye dakika ya saba ya muda nyongeza. Ushindi huo umeifanya Simba kufikisha pointi 72 na kuendeleza ‘gap’ la pointi tano kati yake ya vinara Yanga SC wenye pointi 77 wakati Azam FC wakiwa nafasi ya tatu na pointi 66. Kwa upande wao JKT Tanzania wamebaki na pointi zao 39 katika nafasi ya 13.



Simba 1-0 JKT Tanzania; Goli la Hassan Dilunga dakika majeruhi (TPL - 30/4/2019)
Simba 1-0 JKT Tanzania; Goli la Hassan Dilunga dakika majeruhi (TPL - 30/4/2019)

Bao pekee la Hassan Dilunga likifungwa dakika za majeruh, limetosha kuipa Simba pointi tatu muhimu dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) uliopigwa leo kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Dilunga amefunga goli hilo akimalizia pasi ya Emmanuel Okwi wakati zikiwa zimebaki sekunde chache mpira kumalizika katika mechi ngumu na ya ushindani wa aina yake. JKT walionekana wagumu zaidi hasa katika safu yao ya ulinzi iliyoweza kudhibiti mashambulizi makali ya Simba hadi ilipofika dakika ya 90 kabla ya dakika saba kuongezwa lakini Dilunga akafanikiwa kufunga bao hilo kwenye dakika ya saba ya muda nyongeza. Ushindi huo umeifanya Simba kufikisha pointi 72 na kuendeleza ‘gap’ la pointi tano kati yake ya vinara Yanga SC wenye pointi 77 wakati Azam FC wakiwa nafasi ya tatu na pointi 66. Kwa upande wao JKT Tanzania wamebaki na pointi zao 39 katika nafasi ya 13.



ALLIANCE FC 0-2 SIMBA SC: HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 23/4/2019)
ALLIANCE FC 0-2 SIMBA SC: HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 23/4/2019)

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania bara Simba SC wamepata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Alliance katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Magoli ya Simba yamefungwa Haruna Niyonzima dakika ya 21 akimalizia krosi ya Mzamiru Yassin na Emmanuel Okwi dakika ya 75 baada ya kuichambua safu ya ulinzi ya Alliance kutokana na pasi safi ya Nicholas Gyan. Kwa matokeo hao, Simba inafikisha pointi 63 ikisalia kwenye nafasi ya tatu nyuma ya Azam FC yenye pointi 66 huku Yanga ikiwa kileleni na pointi 74 wakati Alliance FC ikirejea hatarini tena kwa kusalia katika nafasi yake ya 16 na pointi 37. Ushindi huo unarejesha matumaini kwa Simba katika mbio zake za kutetea taji lake baada ya kupoteza mchezo wake uliopita dhidi ya Kagera Sugar mjini Bukoba, na sasa inajiandaa kwa mchezo ujao dhidi ya Alliance FC utakaopigwa Aprili 25, 2019 kwenye uwanja huo huo wa CCM Kirumba jijini Mwanza.



Ulinzi Stars 0-1 AFC Leopards SC | BRIAN MARITA GOAL | Sun, 07.04.2019 | SPL 2018-19 Round 21
Ulinzi Stars 0-1 AFC Leopards SC | BRIAN MARITA GOAL | Sun, 07.04.2019 | SPL 2018-19 Round 21

Watch Brian Marita's goal from the Ulinzi Stars vs AFC Leopards SC match which was played at the Afraha Stadium, Nakuru, on Sunday, April 7, 2019. Subscribe to our Youtube Channel for highlights from other SPL matches: https://goo.gl/9QtJNC Kenyan Premier League on Facebook: https://www.facebook.com/KPLeague/ Kenyan Premier League on Twitter: https://twitter.com/TheOfficialKPL Kenyan Premier League on Instagram: https://www.instagram.com/kenyanpremierleague



Ulinzi Stars 0-1 AFC Leopards SC | HIGHLIGHTS | Sun, 07.04.2019 | SPL 2018-19 Round 21
Ulinzi Stars 0-1 AFC Leopards SC | HIGHLIGHTS | Sun, 07.04.2019 | SPL 2018-19 Round 21

Watch highlights from the Ulinzi Stars vs AFC Leopards SC match which was played at the Afraha Stadium, Nakuru, on Sunday, April 7, 2019. Subscribe to our Youtube Channel for highlights from other SPL matches: https://goo.gl/9QtJNC Kenyan Premier League on Facebook: https://www.facebook.com/KPLeague/ Kenyan Premier League on Twitter: https://twitter.com/TheOfficialKPL Kenyan Premier League on Instagram: https://www.instagram.com/kenyanpremierleague




« Previous Next »


Popular Tags

#Kawhi Leonard  #Stephen Curry  #Russell Westbrook  #Zlatan Ibrahimovi  #Best Goalkeeper Saves  #Luis Suarez  #Zlatan Ibrahimovi  #Goalkeeper Saves  #Kyrie Irving  #Thomas Muller  

Popular Users

#sportspickle  #narendramodi  #katzm  #MariaSharapova  #CMPunk  #billbarnwell  #selenagomez  #katyperry  #josecanseco  #YouTube  #instagram  #cesc4official  #ArianFoster  #BarackObama  #itsBayleyWWE