KOCHA SIMBA AZIDI KUWA MBOGO CAF by @Dream Online Tv - Post Details

KOCHA SIMBA AZIDI KUWA MBOGO CAF

IKICHEZA kwa kujiamini na mbinu za hali ya juu, juzi Jumamosi Simba ililazimisha suluhu ugenini dhidi ya wenyeji, UD Songo ya Msumbiji. Katika mechi hiyo iliyochezwa mjini Beira, Kocha wa Simba, Patrick Aussems alisisitiza kwamba; “Tunakwenda kumaliza kazi Dar.” Simba iliandika rekodi ndani ya msimu mpya baada ya kutoruhusu bao lolote ikianzia mashindano hayo makubwa ugenini. Msimu uliopita kwenye hatua ya awali Simba ilianzia nyumbani dhidi ya Mbabane ikashinda 4-1, ugenini ikashinda mabao 4-0. Baada ya hapo katika mechi zote ilizocheza ugenini ikaruhusu mabao mengi. Katika mchezo wa jana Simba ilionekana kucheza kwa kujiamini huku safu ya ulinzi ikifanya kazi ya ziada. Ndani ya dakika 45 za kwanza Simba ilipiga mashuti matatu ambayo hayakuwa na madhara lakini mengine mawili nusura yawaamshe mashabiki kwani kipa alipangua yakawa kona. Wekundu hao walipata kona nne za haraka huku wakionekana kutawala zaidi eneo la katikati na kuwalazimisha wenyeji kupiga pasi ndefu ambazo hata hivyo walionyesha udhaifu mkubwa kwenye umaliziaji kwani walikuwa wakipaisha au kupiga pasi fyongo ambazo zilikuwa mboga kwa Benno Kakolanya. UD Songo walicheza mpira wa kuvizia kipindi cha pili lakini wakadhibitiwa na Nyoni na Wawa ambao walionekana kujiamini. Shiboub ambaye ni raia wa Sudan katika mechi jana alitawala kiungo na kuziba mianya mingi ya wenyeji kuwafikia mabeki wa Simba. Mkude muda mwingi alikuwa akiinasa mipira, kuidhibiti na kumpa Chama ambaye kazi yake ilikuwa kusambaza tu. Kwa mujibu wa kocha na viongozi wa Simba, uwanja uliochezwa mechi hiyo wa Campo Do Ferroviario Da Beira ulikuwa chakavu sana na haukuruhusu kucheza kiwango chao ingawa suluhu bado inawabeba. Aussems alisisitiza kwamba wana nafasi kubwa ya kushinda Dar es Salaam kwenye mechi ya marudiano na kusonga mbele na hawana wasiwasi. “Ulikuwa mchezo wa wazi, walikuwa wakijaribu kufunga na kwetu ilikuwa hivyo, jambo muhimu hatujaruhusu goli. Mchezo wa marudiano utakaochezwa Dar ni muhimu, kwa ushangiliaji wa mashabiki wetu na uwanja mzuri nafikiri tutafanya vizuri,” alisema Kocha Aussems.

Similar Posts!

KOCHA WA ZAMANI SIMBA AFUNGUKA SABABU YA DODOMA JIJI KUFUNGWA NA SIMBA 2-0 KWA MKAPA
KOCHA WA ZAMANI SIMBA AFUNGUKA SABABU YA DODOMA JIJI KUFUNGWA NA SIMBA 2-0 KWA MKAPA

FT: Simba 2-0 Dodoma Jijj 🔊 Alama tatu muhimu kwa Simba, Dodoma Jiji wamepoteza mechi ambayo naona walicheza vizuri, walikuwa na nidhamu nzuri ya kuzuia kwa bahati mbaya kosa moja kubwa likawafanya waikabidhi mechi mikononi mwa Simba. 🔊 Dodoma Jiji hawakuwaruhusu Simba kupiga penetration passes, walizuia half spaces na kuwafanya wacheze nje ya eneo la hatari muda mwingi, katika system ya low blocks defensive hukuona Simba wanatengenezaje nafasi kabla ya kosa la penati kutokea. 🔊 Ipo sehemu ya Simba kujitazama mara mbili, mara nyingi wanapokutana na timu za aina hii wanajenga mashambulizi yao taratibu hiyo inawasaidia wapinzani kujipanga kwa sababu presha inakuwa ni ndogo kwenye eneo lao. 🔊 Zipo nyakati ambazo Dodoma Jiji wangekuwa wakatili mbele ya lango la Simba pengine wangeifanya mechi kuwa ngumu zaidi, ni rahisi kukishinda kiungo cha Simba kama utaamua kuwa press na kufanya mikimbio nyuma ya safu hiyo. 🔊 Viungo wa Simba wanapitika kirahisi timu isipokuwa na mpira, tofauti ilikuwa ndogo tu, Dodoma Jiji hawakuwa na ubora katika kufanya matendo ya mwisho ya kutengeneza nafasi na kufunga magoli na hii inaficha udhaifu wa wapinzani ulioonekana



ONA ALICHOKISEMA SHABIKI WA SIMBA ANAEMKUBALI FISTON MAYELE BAADA YA SIMBA KUWAFUNGA DODOMA JIJI
ONA ALICHOKISEMA SHABIKI WA SIMBA ANAEMKUBALI FISTON MAYELE BAADA YA SIMBA KUWAFUNGA DODOMA JIJI

✍Simba SC hawakuwa katika ubora ambao wenyewe wangetamani lakini wamevuna alama 3 , katika mechi zote za msimu ngumu mechi zote ucheze kwa kiwango cha juu , muhimu ni kukusanya alama tatu ndio waliciofanya leo dhidi ya Dodoma FC ambao hawakuonesha madhara kwenda mbele . ✍Dodoma FC dakika kama 5 au 10 za mwanzo walianza na BACK 3 lakini wakaibadilisha haraka na kwenda 4-3-3 wakiwa na mpira na 4-4-2 bila mpira , hawakutaka kuzidiwa idadi ya wachezaji katikati ya uwanja na pembeni ya uwanja... lakini bado mara kadhaa waliacha spaces kubwa sana baina ya mstari mmoja na mwingine na mchezaji kwa mchezaji ✍Ni Simba tu wenyewe , Dodoma ni kama vile hawakuwa na mpango au maono ya kutafuta goli, walikuwa tayari kufungwa ( Dodoma was there for taking ) ...Simba hasa kipindi cha kwanza walikuwa slow sana , umakini unakosekana , walikuwa wanacheza kama wanaongoza 3 au 4 , mpira haukutembea kwa haraka kutoka sehemu moja kwenda nyingine ...viungo watatu ( Chama Nyoni Mzamiru ) + mawinga wawili ( Banda na Sakho ) wote wanacheza mbele ya Dodoma ...hakukuwa na mikimbio ya kutosha nyuma ya kiungo cha Dodoma na safu ya ulinzi ya Dodoma ( Easy to defend ) ✍Nafikiri Dodoma walicheza bila imani kwamba wanaweza kufunga au kupata chochote kitu dhidi ya Simba ,kuna muda walikuwa " Casual " sana , jinsi idadi ya mipira waliyokuwa wanapoteza kirahisi , iwe kwenye kiungo mpaka pembeni ya uwanja ( Sloppy ) nafikiri hata Wawa na Onyango wanaweza wakaangaliana na kujiuliza " Hivi leo mbona hatuna kitu cha kuzuia ? " 😀 NOTE 1: George Wawa sijui alikuwa anafikiria nini ? Alijua refa hatomuona kushika mpira kwa staili ile ? Doh 😀😀 na bado akabisha,Chama Jr alituliza akili licha ya wachezaji wa Dodoma kumfanyia " Mind game" 2: Cleophace Mkandala ..amekosa tu msaada kutoka kwa wenzake,maana ndio mchezaji pekee ambaye akiwa na mpira ndio unaona anaweza kufanya jambo. 3: Positive nyingine kwa Simba ukiacha alama 3 ni kurejea kutoka kwenye majeraha baadhi ya wachezaji 4: Peter Banda hakuacha kujaribu kutengeneza nafasi mpaka akapata assist yake kwa Kagere. Never give up 5: Dodoma inaonekana bado inasukwa ..muda unakimbia FT: Simba 2-0 Dodoma FC



UTACHEKA!! SHABIKI SIMBA ATEMA SHOMBO BAADA YA KUWAFUNGA 2-0 DODOMA JIJI KWA MKAPA
UTACHEKA!! SHABIKI SIMBA ATEMA SHOMBO BAADA YA KUWAFUNGA 2-0 DODOMA JIJI KWA MKAPA

✍Simba SC hawakuwa katika ubora ambao wenyewe wangetamani lakini wamevuna alama 3 , katika mechi zote za msimu ngumu mechi zote ucheze kwa kiwango cha juu , muhimu ni kukusanya alama tatu ndio waliciofanya leo dhidi ya Dodoma FC ambao hawakuonesha madhara kwenda mbele . ✍Dodoma FC dakika kama 5 au 10 za mwanzo walianza na BACK 3 lakini wakaibadilisha haraka na kwenda 4-3-3 wakiwa na mpira na 4-4-2 bila mpira , hawakutaka kuzidiwa idadi ya wachezaji katikati ya uwanja na pembeni ya uwanja... lakini bado mara kadhaa waliacha spaces kubwa sana baina ya mstari mmoja na mwingine na mchezaji kwa mchezaji ✍Ni Simba tu wenyewe , Dodoma ni kama vile hawakuwa na mpango au maono ya kutafuta goli, walikuwa tayari kufungwa ( Dodoma was there for taking ) ...Simba hasa kipindi cha kwanza walikuwa slow sana , umakini unakosekana , walikuwa wanacheza kama wanaongoza 3 au 4 , mpira haukutembea kwa haraka kutoka sehemu moja kwenda nyingine ...viungo watatu ( Chama Nyoni Mzamiru ) + mawinga wawili ( Banda na Sakho ) wote wanacheza mbele ya Dodoma ...hakukuwa na mikimbio ya kutosha nyuma ya kiungo cha Dodoma na safu ya ulinzi ya Dodoma ( Easy to defend ) ✍Nafikiri Dodoma walicheza bila imani kwamba wanaweza kufunga au kupata chochote kitu dhidi ya Simba ,kuna muda walikuwa " Casual " sana , jinsi idadi ya mipira waliyokuwa wanapoteza kirahisi , iwe kwenye kiungo mpaka pembeni ya uwanja ( Sloppy ) nafikiri hata Wawa na Onyango wanaweza wakaangaliana na kujiuliza " Hivi leo mbona hatuna kitu cha kuzuia ? " 😀 NOTE 1: George Wawa sijui alikuwa anafikiria nini ? Alijua refa hatomuona kushika mpira kwa staili ile ? Doh 😀😀 na bado akabisha,Chama Jr alituliza akili licha ya wachezaji wa Dodoma kumfanyia " Mind game" 2: Cleophace Mkandala ..amekosa tu msaada kutoka kwa wenzake,maana ndio mchezaji pekee ambaye akiwa na mpira ndio unaona anaweza kufanya jambo. 3: Positive nyingine kwa Simba ukiacha alama 3 ni kurejea kutoka kwenye majeraha baadhi ya wachezaji 4: Peter Banda hakuacha kujaribu kutengeneza nafasi mpaka akapata assist yake kwa Kagere. Never give up 5: Dodoma inaonekana bado inasukwa ..muda unakimbia FT: Simba 2-0 Dodoma FC