Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars MAKOSA ya safu ya ulinzi ya Simba, jana yaliigharimu timu hiyo na kujikuta ikipigwa mabao 2-0 na JS Saoura nchini Algeria lakini wamesisitiza kwamba nguvu zote sasa ni kwa AS Vita Jumamosi. Simba sasa imeelekeza nguvu zote kwenye mechi ya AS Vita ili kucheza karata ya mwisho ya kutafuta nafasi ya kufuzu robo fainali. Hesabu zinaibeba Simba kwani ikishinda mchezo huo itafi kisha pointi tisa na kusonga mbele. Kwenye mechi ya jana safu ya ulinzi ya Simba chini ya Paschal Wawa, Mohammed Tshabalala na Paul Bukaba haikuwa na uelewano mzuri jambo ambalo liliwapa Saoura nguvu ya kushambulia. Mabao ya wenyeji yalifungwa na Yahya Sherrif kwa shuti la kiufundi huku la pili likipachikwa na Mohammed Amine kwa penalty. Amine alifanyiwa faulo na Bukaba ambaye kipindi cha kwanza nusura ajifunge alipokuwa akiokoa. Sasa Simba imeelekeza nguvu zake kwa mechi ya Jumamosi saa moja usiku kwenye Uwanja wa Taifa ambayo wamesisitiza kwamba hata kama Mwinyi Zahera wa Yanga atauza siri zao kwa Vita potelea mbali lakini ushindi lazima. Kocha wa Simba,Patrick Aussems amefunga ukurasa wa mchezo wa jana na kuanzia leo ni kazi moja tu huku mashabiki nao wakisisitiza kupambana. Zahera aliliambia Spoti Xtra kwamba; “Simba atamfunga Vita kwenye Uwanja wa Taifa na wanaweza kwenda robo fainali, lakini haiwezi kubeba ubingwa wa Afrika.” “Haina timu yenye uwezo huo. Lakini ni ukweli usiofi chika kwamba mimi Vita nitawapa mbinu za Simba kwavile wale ni rafi ki zangu na kocha wao ni bosi wangu kwenye timu ya Taifa. “Siwezi kuwafi cha, ila itakuwa ni mechi ngumu sana na nzuri,”alisema Zahera ambaye anadai kwamba Simba inamuombea mabaya kwenye Ligi Kuu na FA. Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/kidanistars
Hooliganism once again reared its ugly head in a match involving AFC Leopards and Ulinzi Stars at the Kenyatta Stadium on Sunday during and after the match as angry Ingwe fans expressed their frustrations on the team's loss to the soldiers.
Azam FC, imelazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Alliance katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) uliofanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Ilibidi Azam FC iweze kusubiri hadi dakika ya 79 kuweza kupata bao la uongozi, lililofungwa na Joseph Mahundi, aliyeingia dakika ya 76, kuchukua nafasi ya Ramadhan Singano, na alifunga bao hilo kiustadi akiunganisha krosi ya Chirwa. Dakika ya 90 Alliance ilisawazisha kupitia kwa Dickson Ambundo, akimalizia mpira uliogonga mwamba kufuatia mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na Israel Patrick. Azam walionekana kulalamikia bao hilo wakidai kuwa beki wao Agrey Moris alisukumwa kabla ya kufungwa lakini, mwamuzi Abubakar Mturo (Mtwara) na Msaidizi namba moja, Mohamed Mkono (Tanga), waliamuru kuwa bao halali. Mchezo huo ulikuwa na kasi sana, Azam FC ikianza kwa mashambulizi makali langoni mwa Alliance, ambapo dakika ya kwanza Obrey Chirwa, alikosa bao la wazi baada ya kuupiga vibaya mpira akiwa anatazamana na lango ndani ya eneo la hatari, akipokea pasi ya Donald Ngoma. Mabingwa hao waliweza kupata ugumu kuipenya safu ya ulinzi ya Alliance, kutokana na timu hiyo kusimama wengi kujilinda nyuma ya mpira wakati Azam FC ikishambulia. Mara baada ya mchezo huo kumalizika, kipa wa Azam FC, Razak Abalora, alioneshwa kadi nyekundu kufuatia kadi ya pili ya njano iliyosababishwa na lugha ya kutoridhishwa na maamuzi aliyoitoa kwa mwamuzi huyo. Sare hiyo inaifanya Azam FC kufikisha jumla ya pointi 48 katika nafasi ya pili kwenye msimamo ikiwa na mchezo mmoja mkononi, ikizidiwa pointi saba na kinara Yanga aliyefikisha 55 kufuatia suluhu yake ya jana dhidi ya Singida United.
There was a shock result in the Kenyan Premier League as bottom of the table Mount Kenya United come from a goal down to beat league leaders Mathare United 2-1 for their first win of the season.Chrispin Oduor had given the Slum boyz the lead but Peter Amani scored twice for Mount Kenya to end Mathare's nine matches unbeaten run. Ulinzi Star drew 1-1 against Chemelil Sugar while Posta Rangers held Tusker to a barren draw at the Kenyatta stadium. On Sunday, Bandari host AFC Leopards in Mombasa, Kakamega Homeboyz battle Vihiga United, Kariobangi Sharks face Sofapaka, Nzoia play Sony Sugar and Zoo welcome KCB to Kericho.
Mabingwa wa Tanzania Bara Simba SC wamepoteza mchezo wao wa kwanza wa raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika (CAF CL) kwa kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Mashetani Wekundu wa Nkana FC katika mchezo uliopigwa mjini Kitwe nchini Zambia. Simba ilionekana kuelemewa zaidi kipindi cha kwanza cha mchezo na kuruhusu bao la kwanza lilifungwa na Ronald Kampamba dakika ya 27 baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Hassan Kessy. Kipindi cha pili Simba walionekana kuimarika na kukianza kwa kusukuma mashambulizi langoni kwa Nkana lakini walijikuta wakifanya makosa katika safu yao ya ulinzi na kuruhusu bao la pili, lililotiwa kimiani na Kelvin Kampamba dakika ya 56. Simba walipata bao lao pekee dakika ya 73 kwa mkwaju wa penati uliofungwa na Nahodha wao John Bocco baada ya Meddie Kegere kuangushwa ndani ya eneo la hatari. Kwa matokeo hayo sasa Simba itahitaji ushindi wa kuanzia bao 1-0 katika mchezo wa marudiano utakaopigwa Jijini Dar es Salaam, wiki moja ijayo.
Vijana wa Alliance FC leo wamewachapa wakongwe Mtibwa Sugar bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza. Bao pekee la Alliance limefungwa na Dickson Ambundo dakika ya 54 akimalizia pasi ya Michael Chinedu baada ya kipa wa Mtibwa Shaaban Kado kuutema mpira uliopigwa na Siraji Juma. Katika mchezo huo, Alliance imetawala zaidi mchezo pamoja na kufanya mashabulizi zaidi kuliko Mtibwa huku ikionekana kujiimarisha zaidi katika safu yake ya ulinzi na kudhibiti mashambulizi ya Mtibwa yaliyoongozwa na Juma Luizio, Kelvin Sabato, Ismail Mhesa na Salum Kihimbwa. Matokeo hayo yanaifanya Alliance kufikisha pointi 13 na kukaa nafasi ya 16 wakati Mtibwa ikiendelea kukaa nafasi ya nne ikiwa na pointi 23.
Timu ya Alliance FC ya Jijini Mwanza imebanwa mbavu kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1 na African Lyon kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo CCM Kirumba Jijini Mwanza. Mkongwe, Haruna Moshi 'Boban' ndiye aliyetanguliza African Lyon kwa bao la dakika ya 8 kazi nzuri ikifanywa na Victor Da Costa. Baada ya mshambulizi ya muda mrefu hatimaye Michael Chinedu aliyeingia kutoka benchi aliipa kashikashi safu ya ulinzi ya African Lyon na kuisawazishia timu yake ya Alliance FC dakika za nyongeza. Hata hivyo dakika ya 78 ya mchezo, Alliance walikwamisha mpira nyavuni lakini haikuwa bao ikionekana kuwa kuna faulo ilifanyika kabla yay a bao hilo.