HATRICK ya KAGERE na OKWI Wakabidhiwa Mipira Waionyoosha Coastal Washambuliaji nyota wa Simba, Emmanuel Okwi na Messy Kagere wameweka rekodi ya kufunga mabao sita yaani hat trick mbili ndani ya mechi moja. Wachezaji hao wote wenye asili ya Uganda kwa kuwa Okwi ni Mganda na Kagere ni Mnyarwanda mwenye asili ya Uganda, wamefunga bao hizo sita wakati Simba ikiitwanga Coastal Union kwa mabao 8-1 katika mechi ya Ligi Kuu Bara iliyomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Mabao hayo, yanamfanya Kagere kufikisha mabao 20 msimu katika ligi kuu akifikia rekodi ya mabao 20 ya Okwi msimu uliopita lakini akibakiza bao moja kufikia idadi ya mabao 21 aliyofunga Amissi Tambwe msimu wa 2015/16 akiwa mfungaji bora. Kwa mabao hayo 14, Okwi naye amemfikia nahodha wake John Bocco aliyekuwa benchi katika mechi ya leo akishuhudia 'vijana wake" wakiwagaragaza Wagosi wa Kaya. Mabao mengine yalifungwa na Hassan Dilunga na Cleotus Chama raia wa Zambia na kuifanya Simba iandike ushindi huo mnono zaidi. Kwa ushindi wa leo, Simba imefikisha pointi 81 na kupaa kileleni ikiwaacha Yanga wenye pointi 80 waliokuwa wamekaa kileleni kwa muda mrefu zaidi. Yanga wamecheza 34 huku Simba wakiwa wamefikisha mechi 31 baada ya kucheza mechi yao ambayo wametoa kipigo kikali kwa Wagosi wa Kaya. #SIMBAVsCOASTALUNION https://www.youtube.com/watch?v=N1X-f... Watch More Videos here: https://goo.gl/GvVdZw Watch More Videos here: https://goo.gl/ae33fL Website: www.globalpublishers.co.tz FaceBook: www.facebook.com/globalpublishers Instagram: www.instagram.com/globalpublishers Twitter: www.twitter.com/GlobalHabari Install Global App: ANDROID: https://goo.gl/QvT6RV Install Global App: iOS: https://goo.gl/2jDyho
Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars #SIMBASC imeendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa 1-0 JKT Tanzania Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam jioni ya leo. Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 72 baada ya kucheza mechi 28 na kuendelea kushika nafasi ya pili, nyuma ya watani wao wa jadi, #YangaSC wenye pointi 77 za mechi 33. Sifa zimuendee mfungaji wa bao hilo pekee dakika ya sita kati ya saba za nyongeza baada ya kutimia dakika 90 za kawaida, kiungo Hassan Dilunga aliyetokea benchi kipindi cha kwanza kuchukua nafasi ya Nahodha, John Raphael Bocco. Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/kidanistars
Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars SIMBA SC imeendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa 1-0 JKT Tanzania Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam jioni ya leo. Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 72 baada ya kucheza mechi 28 na kuendelea kushika nafasi ya pili, nyuma ya watani wao wa jadi, Yanga SC wenye pointi 77 za mechi 33. Sifa zimuendee mfungaji wa bao hilo pekee dakika ya sita kati ya saba za nyongeza baada ya kutimia dakika 90 za kawaida, kiungo Hassan Dilunga aliyetokea benchi kipindi cha kwanza kuchukua nafasi ya Nahodha, John Raphael Bocco. Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/kidanistars
Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars SIMBA SC imeendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa 1-0 JKT Tanzania Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam jioni ya leo. Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi 72 baada ya kucheza mechi 28 na kuendelea kushika nafasi ya pili, nyuma ya watani wao wa jadi, Yanga SC wenye pointi 77 za mechi 33. Sifa zimuendee mfungaji wa bao hilo pekee dakika ya sita kati ya saba za nyongeza baada ya kutimia dakika 90 za kawaida, kiungo Hassan Dilunga aliyetokea benchi kipindi cha kwanza kuchukua nafasi ya Nahodha, John Raphael Bocco. Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/kidanistars
Baada ya Yanga kuchapwa bao 1-0 na Mtibwa Sugar,nahodha wa timu hiyiop Ibrahim Ajib amewatupia lawama waamuzi kuwa wamekuwa hawaitendei haki timu yao katika mechi nyingi za Ligi Kuu Bara. Bao la Riphat Khamis dakika ya 52 lilitosha kuipa ushindi Mtibwa Sugar na kuendeleza rekodi yao bora inapocheza nyumbani kwani katika michezo mitano mfululizo iliyopita iliyocheza Morogoro imeshinda yote. Kukataliwa kwa bao lililofungwa na Amissi Tambwe dakika ya 89 ndiko kulisababisha Ajib kutoa ya moyoni ukuhusu waamuzi kuwa wamekuwa hawatendi haki licha ya wachezaji kupambana sana uwanjani kutafuta matokeo. Mwamuzi Hans Mabena wa Tanga alikataa bao hilo baada ya kumuangalia mwamuzi wa pembeni ambaye alinyoosha kibendera kuashiriki mfungaji alikuwa ameotea. "Waamuzi hawachezeshi kwa haki kwani huwa hawako upande wetu mechi nyingi. Kwani tunajitahidi kwa uwezo wetu lakini inaumiza unapambana sana lakini anatokea mwingine anakurudisha nyuma"alisema. Ajib amesema wataendela kupambana katika michezo iliyobaki kwani licha ya wapinzani wao Simba ambao wanawafuukuza wana mechi nyingi hivyo lolote. Kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga, Meddie Kagere amefunga mabao mawili na kuikoa timu yake isipate kipigo kutoka kwa Coastal Union. Simba ilijikuta ikishangazwa dakika ya kwanza tu baada ya Raizin Hafidhi kuifungia Coastal Union bao kutokana na beki Erasto Nyoni kujichanganya na kipa wake Aishi Manula katika kuokoa mpira huo. Kagere aliisawazishia Simba bao kwa penalti dakika ya 48, penalti iliyotokana na Emmanuel Okwi kuangushwa na kipa wa Coastal Union Sudi Mohammed. Dakika ya 68 Kagere aliipata Simba bao la pili kwa shuti kali akimalizia pasi ya Clatous Chama hivyo kufikisha mabao 16 kwenye ligi na kumfikia kinara Salum Aiyee wa Mwadui FC huku akimzidi bao moja Heritier Makambo wa Yanga mwenye mabao 15.
Vijana wa Mbeya City leo wamebanwa mbavu na Chama la Wana Stand United kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Mbeya City ndiyo waliotangulia kupata bao dakika ya 54 mfungaji akiwa ni John Kabanda wakati Jacob Masawe akiisawazishia Stand dakika ya 86.
Vijana wa Mbeya City leo wamebanwa mbavu na Chama la Wana Stand United kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya. Mbeya City ndiyo waliotangulia kupata bao dakika ya 54 mfungaji akiwa ni John Kabanda wakati Jacob Masawe akiisawazishia Stand dakika ya 86.
Kwa mujibu wa kipindi hiki cha terehe 08/11/2018, bao la pili alilofunga Meddie Kagere kwenye mchezo kati ya JKT Tanzania vs Simba SC uliopigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga Jumamosi ya Novemba 2, 2018, halikuwa bao halali kwa kuwa mfungaji alikuwa ameotea kabla ya kufunga. Pamoja na matukio mengine yaliyojiri kwenye mchezo huo, pia palikuwa na matukio mawili ya wachezaji wa JKT kudai penati wakidai wachezaji wa Simba Mohamed Hussein na Erasto Nyoni kwa nyakati tofauti, walishika mpira ndani ya eneo la hatari hadi kusababisha mchezaji wa JKT Ahmed Shiboli kutolewa nje kwa kadi nyekundu. Mbali na mchezo huo, kipindi hiki kimechambua mechi kdhaa za raundi ya 13 ya Ligi Kuu Tanzania Bara ukiwemo mchezo wa Yanga vs Ndanda SC na ule wa Kagera Sugar vs Azam FC. Tukio kubwa katika mchezo wa Kagera Sugar na Azam FC ni mchezaji wa Azam FC Donald Ngoma kupewa kadi nyekundu, kadi ambayo wengi hawakuelewa sababu za adhabu hiyo kumkumba. Waamuzi wawili wastaafu ambao ni magwiji, Osman Kazi na Omary Abdulkadir wamechambua matukio yote na kuonesha ni wapi waamuzi walikosea na wapi waamuzi walipatia, na nini walipaswa kufanya. Kipyenga cha Mwisho ni kila Alhamis saa 3:30 usiku Azam Sports 2.