Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars Unaweza kusema ni 'Mwendo Mdundo kwa Simba' baada ya leo kumefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Nkana FC ya Zambia katika mchezo wa marudiano uliochezwa uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Matokeo hayo yanaipa nafasi Simba kutinga hatua ya Makundi baada ya kufanikiwa kushinda kwa jumla ya mabao 4-3 kwa kuwa mchezo wa kwanza walishinda kwa jumla ya mabao 2-1 na leo wapinzani wao wamekubali kupigwa mabao 3-1. Nkana walikuwa wa kwanza kufunga bao kupitia kwa Walter Bwalya na kuwafanya Simba waongeze kasi na kusawazisha dakika ya 26 kupitia kiungo Jonas Mkude aliyemalizia pasi ya Claytous Chama na dakika ya 45 Meddie Kagere alifunga bao la 2 kwa kichwa akimaliza pasi ya James Kotei. Kipindi cha pili Simba walifanya mabadiliko kwa kumtoa Meddie Kagere dakika ya 56 nafasi yake ikachukuliwa na Hassan Dilunga na Emmanuel Okwi alitoka dakika ya 79 akaingia Shiza Kichuya hali iliyoweza kuongeza mashambulizi. Iliwalazimu Simba wasubiri mpaka dakika ya 88 ambapo Hassan Dilunga alipiga pasi kwa guu la kushoto iliyomkuta Claytous Chama na kumalizia kwa kutumia kisigino kilichomchanganya mlinda mlango wa Nkana FC. Matokeo hayo yanaipeleka Simba kwenye hatua ya Makundi kibabe huku kikosi cha Nkana FC kikishuka kupambana kwenye mashindano ya kombe la Shirikisho. Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars/ Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars/ Twitter: https://twitter.com/kidanistars
HICHI NDICHO KIKOSI CHA SIMBA KITAKACHOIVAA NKANA LEO
#SIMBASC #NKANAFC Timu ya Simba wanafanya mazoezi ya Kufa na kupona katika Uwanja wa Boko jijini Dar kujiandaa na NKANA FC mchezo wa Ligi ya MABINGWA. Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars/ Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars/ Twitter: https://twitter.com/kidanistars
Timu ya Simba leo imefanya mazoezi katika Uwanja wa Boko jijini Dar es Salaam Kujiandaa na timu ya Nkana Fc siku ya Jumapili katika Uwanja wa Taifa, Mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa marudiano. #KUFANAKUPONA #SIMBASC #NKANA Katika Mchezo wa Kwanza Simba walifungwa bao 2-1 nchini Zambia Kitwe
Hii ni sehemu ya kipindi cha Dakika 90 kilichoruka Jumatatu Desemba 17 Azam Sports 2 ambapo wachambuzi wetu Charles Abel na Thobias Sebastian wameyaweka wazi makossa yaliyofanywa na wachezaji wa Simba kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Nkana FC. Fuatilia mjadala huu.
#simbavsnkana Kuelekea mchezo wa jumamosi wa Simba dhidi ya Nkana wamesema lazma wawafunge nkana kuvuka hatua ya makundi league ya mabingwa Africa