Goli la penati kutoka kwa Marcel Kaheza lililowapa Polisi Tanzania pointi tatu dhidi Ndanda SC kwenye Uwanja wa Ushirika, Moshi. Kocha wa Polisi Malale Hamsini akiri kuzidiwa licha ya ushindi. FT: Polisi Tanzania 1-0 Ndanda SC #LigiKuuTanzaniaBara #VodacomPremierLeague #VPLUpdates #VPL #PolisiTanzania #NdandaSC Tazama Vodacom Premier League, taarifa ya Habari na vipindi vingine vya Habari na Matukio LIVE kutoka Azam TV na UTV kupitia Azam TV Decoder au AzamTV Max App. Unaweza kupata AzamTV Max App kwa ajili ya Android kutoka hapa: ► https://bit.ly/2wB6zmR Tufuatilie kwenye mitandao ya kijamii ►INSTAGRAM: https://www.instagram.com/azamtvtz/ ►INSTAGRAM: https://www.instagram.com/azamsports2/ ►TWITTER: https://twitter.com/azamtvtz ►FACEBOOK: http://www.facebook.com/azamtvtz ►WEBSITE: http://www.azamtv.co.tz
Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars KIKOSI cha Yanga, leo kimepoteza mchezo wake wa kombe la SportPesa ikiwa ni hatua ya robo fainali kwa kukubali kufungwa mabao 3-2 dhidi ya KK Sharks ya Kenya mchezo uliochezwa Uwanja wa Taifa. Michuano ya SportPesa Cup ambayo kwa sasa ni msimu wake wa tatu imeshirikisha timu nane ikiwa ni nne kutoka Tanzania ambazo ni Singida United, Simba, Mbao na Yanga na zile za kutoka Kenya ni pamoja na KK Sharks, Bandari, AFC Leopards na Gor Mahia ambao ni mabingwa watetezi. Kipindi cha kwanza Yanga walikubali kupoteza kutokana na uzembe wa mabeki ambapo dakika ya 9 KK Sharks waliandika bao la kwanza kupitia kwa Abuye Duke na baada ya kuzidisha mashambulizi wakaandika bao la pili dakika ya 37 kupitia kwa Abege George. Mpaka kipindi cha kwanza kinakamilika Yanga walikuwa nyuma kwa mabao mawili, kipindi cha pili baada ya kufanya mabadiliko kwa kumtoa Haruna Moshi na kuingia Amiss Tambwe pamoja na Abdallah Shaibu na kuingia Thaban Kamusoko, Mrisho Ngassa nafasi yake kuchukuliwa na Deus Kaseke pamoja na Paul Godfery nafasi yake kuchukuliwa na Juma Abdul kasi ya Yanga ilianza kuonekana. Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars/ Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars/ Twitter: https://twitter.com/kidanistars
Kuna mwengi yametikisa michezoni wiki hii lakini kurasa za mwisho za magazeti ambazo huandika habari za michezo, zimetoa kipaumbele zaidi kwa habari ya usajili ndani ya klabu ya Yanga, ambao wametumia dirisha dogo kumnasa kiungo Haruna Moshi Boban. Taarifa nyingine iliyopewa uzito ni kuelekea mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Nkana FC dhidi ya Simba SC unaopigwa leo Desemba 15, 2018 nchini Zambia. Ndani ya Studio Philip Cyprian yuko na wanahabari nguli wa michezo, wanafanya uchambuzi na mjadala kuhusu yaliyopewa uzito kwenye kurasa hizo. Vilevile tumetembelea vibanda vya magazeti na kuzungumza na wafuatiliaji wa habari za michezo magazetini, wengi wakiwa ni mashabiki wa soka. Kipindi hiki ni kila Jumamosi saa 3:30 asubuhi Azam Sports 2.
Timu ya Alliance FC ya Jijini Mwanza imebanwa mbavu kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1 na African Lyon kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo CCM Kirumba Jijini Mwanza. Mkongwe, Haruna Moshi 'Boban' ndiye aliyetanguliza African Lyon kwa bao la dakika ya 8 kazi nzuri ikifanywa na Victor Da Costa. Baada ya mshambulizi ya muda mrefu hatimaye Michael Chinedu aliyeingia kutoka benchi aliipa kashikashi safu ya ulinzi ya African Lyon na kuisawazishia timu yake ya Alliance FC dakika za nyongeza. Hata hivyo dakika ya 78 ya mchezo, Alliance walikwamisha mpira nyavuni lakini haikuwa bao ikionekana kuwa kuna faulo ilifanyika kabla yay a bao hilo.
Mkongwe, Haruna Moshi 'Boban' anaitanguliza African Lyon dhidi ya Alliance kwenye dimba la CCM Kirumba, kazi nzuri ikifanywa na Victor Da Costa. Ni mchezo wa raundi ya pili ya Ligi Kuu Tanzania Bara.