GOLI & PENATI: TOWNSHIP ROLLERS 0-1 YANGA SC (CAF CL - 24/8/2019) by @Azam TV - Post Details

GOLI & PENATI: TOWNSHIP ROLLERS 0-1 YANGA SC (CAF CL - 24/8/2019)

Timu ya Yanga SC imefanikiwa kusonga mbele na kuingia raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika (CAF CL) ikiitupa nje Township Rollers ya Botswana kwa jumla ya mabao 2-1. Yanga imekamilisha ushindi huo kwenye mchezo wa marudiano wa raundi ya awali uliopigwa leo kwenye Dimba la Taifa la Botswana, ikishinda bao 1-0 lililofungwa na Juma Balinya dakika ya 42 kwa mpira wa ‘free-kick’. Katika mchezo huo, kipa wa Yanga Metacha Mnata ameibuka shujaa kwa kufuta penati ya Towship Rollers iliyopatikana dakika ya 66 baada ya mchezaji wake kuchezewa madhambi ndani ya eneo la hatari. Katika mchezo wa kwanza uliopigwa wiki mbili zilizopita, timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1 kwenye Dimba la Taifa Dar es Salaam, Yanga ikisawazisha kwa penati kupitia kwa Patrick Sibomana baada ya kutanguliwa. Baada ya kufanikiwa kupenya katika hatua hiyo, sasa mabingwa hao wa kihistoria wa Tanzania Bara huenda wakakutana na Zesco ya Zambia inayonolewa na kocha wake wa zamani George Lwandamina. Zesco ambao leo wanarudiana na Green Mamba, wana nafasi kubwa ya kufuzu kwani tayari walishajiwekea kibindoni mabao 2-0 ugenini.

Similar Posts!

USIKU WA VITASA | Karim Mandoga Vs Mada Maugo (TKO) - 11/04/2024
USIKU WA VITASA | Karim Mandoga Vs Mada Maugo (TKO) - 11/04/2024

Kwa TKO raundi ya sita, Mada Maugo amemkalisha Karim Mandonga.



Mashujaa FC 1-1 (6-5) Simba SC | Penati | CRDB Bank Federation Cup - 09/04/2024
Mashujaa FC 1-1 (6-5) Simba SC | Penati | CRDB Bank Federation Cup - 09/04/2024

Tazama mikwaju yote ya penati iliyopigwa kwenye mchezo CRDB Bank Federation Cup kati ya Mashujaa FC dhidi ya Simba SC. Simba imetolewa kwa jumla ya penati 6-5 Waliopiga kwa upande wa Simba ni Mohamed Hussein, Israel Mwenda, Freddy Michael Koublan, Willy Onana, Mzamiru Yassin, Ladack Chasambi, Sadio Kanoute Waliopiga kwa upande wa Mashujaa ni Zuberi Dabi, Samson Madeleke, Masinda, Idrissa Stambuli, Adam Adam, Mpoki Mwakinyuke, Baraka Mtui



Yanga kupeleka malalamiko CAF yaliyojiri mechi yao na Mamelodi Sundowns
Yanga kupeleka malalamiko CAF yaliyojiri mechi yao na Mamelodi Sundowns

“Kama klabu lazima tuoneshe kwamba kuna namna ambavyo hatujaridhishwa na kile ambacho kimetokea katika mchezo ule” sehemu ya maneno ya Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe akizungumzia hatua ambazo timu hiyo imepanga kuzichukua juu ya yale yaliyojiri katika dimba la Loftus kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Mamelodi Sundowns.



MSHIKESMSHIKE VIWANJANI - 03/04/2024
MSHIKESMSHIKE VIWANJANI - 03/04/2024

Tazama taarifa mbalimbali za maandalizi ya Simba na Yanga SC kuelekea mechi zao za marudiano za robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika Afrika.



MSHIKEMSHIKE VIWANJANI 01/04/2024
MSHIKEMSHIKE VIWANJANI 01/04/2024

Tazama kipindi cha Mshikemshike Viwanjani ambacho kimekusanya habari mbalimbali ikiwemo taarifa ya Rais wa Yanga, Hersi Said akizungumzia mchakato wa mabadiliko ya klabu hiyo. Mashabiki wa Yanga wameanza safari ya kwenda Mamelodi



Azam FC 2 -1 Yanga SC | Highlights | NBC Premier League 17/03/2024
Azam FC 2 -1 Yanga SC | Highlights | NBC Premier League 17/03/2024

DAR DERBY: Yanga SC imeangukia pua kwa kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Azam FC, katika #DarDerby iliyopigwa leo Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Yanga imetangulia kupata bao kupitia kwa Clement Mzize dakika ya 10 kabla ya Azam kuchomoa dakika ya 19 kwa goli la Gibril Sillah na kisha Feisal Salum akafunga la ushindi dakika ya 51.



Magoli | Azam FC 2-1 Yanga SC | NBC Premier League 17/03/2024
Magoli | Azam FC 2-1 Yanga SC | NBC Premier League 17/03/2024

DAR DERBY: Yanga SC imeangukia pua kwa kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Azam FC, katika #DarDerby iliyopigwa leo Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Yanga imetangulia kupata bao kupitia kwa Clement Mzize dakika ya 10 kabla ya Azam kuchomoa dakika ya 19 kwa goli la Gibril Sillah na kisha Feisal Salum akafunga la ushindi dakika ya 51.



Simba 2-0 Mashujaa | Highlights | NBC Premier League 15/03/2024
Simba 2-0 Mashujaa | Highlights | NBC Premier League 15/03/2024

Clatous Chama amefunga magoli mawili muhimu dakika ya 57 na 73, Simba ikipata ushindi wa 2-0 dhidi ya Mashujaa FC, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa #AzamComplex, Chamazi .