#TPLRound24 KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendeleza wimbi la ushindi kwenye mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) baada ya kuichapa Biashara United mabao 2-1. Mabao ya Azam FC, yamefungwa na kiungo Salum Abubakar 'Sure Boy' (46') kwa kichwa na Ramadhan Singano 'Messi' (62'), huku bao la kufuatia machozi la Biashara likiwekwa kimiani na Daniel Manyenye (2'). #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh #UhaiDrinkingWater #TradegentsTanzaniaLimited