TPL ROUND 20 | MBEYA CITY 0-1 AZAM FC | YAKUBU AFANYA MAMBO by @Azam FC - Post Details

TPL ROUND 20 | MBEYA CITY 0-1 AZAM FC | YAKUBU AFANYA MAMBO

KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imefanya kweli mkoani Mbeya baada ya kuichapa Mbeya City bao 1-0, mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) uliofanyika Uwanja wa Sokoine, Mbeya leo jumapili. Ushindi huo unaifanya Azam FC kufikisha jumla ya pointi 66 kwenye msimamo wa ligi ikiwa nafasi ya pili ikizidiwa pointi nane na kinara Yanga aliyekuwa nazo 74, Simba iliyocheza mechi 22 ni ya tatu ikijikusanyia 57. Beki wa Azam FC, Yakubu Mohammed, aliyeonekana kucheza vema kwenye eneo la beki ya kati sambamba na beki chipukizi kutoka Azam Academy, Lusajo Mwaikenda, ndiye aliyeipatia bao pekee timu hiyo dakika ya 45 akimalizia krosi iliyopigwa na kiungo, Mudathir Yahya, kufuatia mpira wa kona alioanzishiwa na Bruce Kangwa. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh #UhaiDrinkingWater #TradegentsTanzaniaLimited

Similar Posts!

HIGHLIGHTS | AZAM FC 1-0 POLISI TZ | VPL 2020/2021
HIGHLIGHTS | AZAM FC 1-0 POLISI TZ | VPL 2020/2021

KLABU ya Azam FC imeanza vema kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania (VPL) msimu 2020/2021 baada ya kuichapa Polisi Tanzania bao 1-0 kwenye mchezo wa kwanza. Bao pekee la Azam FC limewekwa kambani na mshambuliaji Obrey Chirwa, dakika ya 44 akiunganisha krosi safi ya mshambuliaji mpya, Prince Dube. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora #SARAFU #AzamUkwaju #AzamUbuyu #AzamStrawberry #UhaiDrinkingWater



VPL Highlights | Azam FC 7-0 Singida United | Chirwa aandika rekodi
VPL Highlights | Azam FC 7-0 Singida United | Chirwa aandika rekodi

#ObreyChirwa #IddNado #AzamFC #SingidaUnited Azam FC imeandika rekodi ya kwanza baada ya kupata ushindi mnono wa kihistoria kwenye mechi za mashindano, ikiichapa Singida United mabao 7-0, ukiwa ni mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL). Mabao ya Azam FC yalifungwa na Obrey Chirwa akifunga manne, Idd Seleman 'Nado', akifunga mawili huku jingine wakijifunga wenyewe Singida United. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora



VPL HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-0 MBAO FC | DJODI, CHILUNDA WAFANYA MAMBO
VPL HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-0 MBAO FC | DJODI, CHILUNDA WAFANYA MAMBO

KLABU ya Azam FC imeendelea pale ilipoishia kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) baada ya kuichapa Mbaoa mabao 2-0 jana Jumapili usiku. Mabao ya Azam FC yalifungwa na washambuliaji Richard Djodi na Shaaban Chilunda. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora



HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON
HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON

HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON



VPL HIGHLIGHTS | ALLIANCE 0-5 AZAM FC | CHIRWA APIGA HAT-TRICK, CHILUNDA MMHH!
VPL HIGHLIGHTS | ALLIANCE 0-5 AZAM FC | CHIRWA APIGA HAT-TRICK, CHILUNDA MMHH!

Kikosi cha Azam FC kimeendeleza wimbi la ushindi ugenini kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) kwa kupata ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Alliance. Mabao matatu ya Obrey Chirwa (hat-trick) na mawili ya Shaaban Chilunda, yalitosha kabisa kuihakikishia ushindi mwingine Azam FC mkoani Mwanza, ikifanikiwa kuvuna pointi zote sita. #ObreyChirwa #ShaabanChilunda #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora