NAHODHA AZAM FC AAHIDI MATOKEO MAZURI | AZAM FC v BIASHARA UTD | TPL ROUND 24 by @Azam FC - Post Details

NAHODHA AZAM FC AAHIDI MATOKEO MAZURI | AZAM FC v BIASHARA UTD | TPL ROUND 24

WAKATI zikiwa zimesalia siku mbili kabla ya Azam FC kumenyana na Biashara United, kikosi hicho kimejinasibu kuendelea kupata matokeo mazuri ili kufikia malengo yake. Mabingwa hao wa makombe mawili msimu huu baada ya kufanikiwa kutetea Kombe la Kagame na Mapinduzi Cup, wamekuwa kwenye mwenendo mzuri msimu huu hadi sasa ikishika nafasi ya pili kwenye za Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) ikiwa na pointi 44. Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz Nahodha wa Azam FC, Agrey Moris, amesema kuwa wanajua mchezo utakuwa mgumu lakini watajipanga vema kuweza kupata matokeo. “Biashara ni timu nzuri ukiangalia wamepata kocha mpya kwa vyovyote timu inayopata kocha mpya wachezaji wanakuwa wanajitolea mara mbili zaidi ya mwanzo ila kama sisi Azam siku zote tunajipanga kuhakikisha tunapata matokeo kwenye michezo yetu. “Kwa sababu hii ni ligi ni safari ndefu bila kushinda mechi inayokuja mbele huwezi ukafikia lengo, tumejipanga vizuri wachezaji wote wako vizuri tutahakikisha tunapata matokeo kwenye mchezo huo,” alisema mchezaji huyo wa muda mrefu wa Azam FC. Kihistoria timu hizo zimekutana mara moja tu kwenye ligi, tokea Biashara ipande kucheza Ligi Kuu msimu huu, ambapo mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Karume, mjini Musoma uliisha kwa suluhu. #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh #UhaiDrinkingWater #TradegentsTanzaniaLimited

Similar Posts!

VPL Highlights | Azam FC 7-0 Singida United | Chirwa aandika rekodi
VPL Highlights | Azam FC 7-0 Singida United | Chirwa aandika rekodi

#ObreyChirwa #IddNado #AzamFC #SingidaUnited Azam FC imeandika rekodi ya kwanza baada ya kupata ushindi mnono wa kihistoria kwenye mechi za mashindano, ikiichapa Singida United mabao 7-0, ukiwa ni mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL). Mabao ya Azam FC yalifungwa na Obrey Chirwa akifunga manne, Idd Seleman 'Nado', akifunga mawili huku jingine wakijifunga wenyewe Singida United. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora



VPL HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-0 MBAO FC | DJODI, CHILUNDA WAFANYA MAMBO
VPL HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-0 MBAO FC | DJODI, CHILUNDA WAFANYA MAMBO

KLABU ya Azam FC imeendelea pale ilipoishia kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) baada ya kuichapa Mbaoa mabao 2-0 jana Jumapili usiku. Mabao ya Azam FC yalifungwa na washambuliaji Richard Djodi na Shaaban Chilunda. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora



HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON
HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON

HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON



AZAM FC INAJIPANGA VILIVYO KURUDIANA NA TRIANGLE, CHECHE ATAJA USHINDI TU
AZAM FC INAJIPANGA VILIVYO KURUDIANA NA TRIANGLE, CHECHE ATAJA USHINDI TU

"Vijana wamesikitika na wasikate tamaa, watuombee dua, watusapoti tutapambana kwa ajili yao na kwa ajili ya timu yetu na nchi yetu, mpira umeanza sehemu ya kwanza, tuseme kama kipindi cha kwanza kimeanza lakini tutahakikisha kipindi cha pili tunapambana kwao kwa hali na mali ili tuweze kurudi na ushindi," alisema Kocha Msaidizi wa Azam FC, Idd Nassor 'Cheche', akiwaambia mashabiki wa timu hiyo. #TimuBoraBidhaaBora #AzamFC #TriangleUnited #CAFConfederationCup



AZAM FC YAREJEA DAR IKITOKA KUINYOA MBEYA CITY
AZAM FC YAREJEA DAR IKITOKA KUINYOA MBEYA CITY

Kikosi cha Azam FC kimerejea leo mchana jijini Dar es Salaam kikitokea mkoani Mbeya, kikiwa safi kabisa baada ya jana kuichapa Mbeya City bao 1-0 lililofungwa na beki Yakubu Mohammed. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh #UhaiDrinkingWater #TradegentsTanzaniaLimited



TPL ROUND 20 | MBEYA CITY 0-1 AZAM FC | YAKUBU AFANYA MAMBO
TPL ROUND 20 | MBEYA CITY 0-1 AZAM FC | YAKUBU AFANYA MAMBO

KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imefanya kweli mkoani Mbeya baada ya kuichapa Mbeya City bao 1-0, mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) uliofanyika Uwanja wa Sokoine, Mbeya leo jumapili. Ushindi huo unaifanya Azam FC kufikisha jumla ya pointi 66 kwenye msimamo wa ligi ikiwa nafasi ya pili ikizidiwa pointi nane na kinara Yanga aliyekuwa nazo 74, Simba iliyocheza mechi 22 ni ya tatu ikijikusanyia 57. Beki wa Azam FC, Yakubu Mohammed, aliyeonekana kucheza vema kwenye eneo la beki ya kati sambamba na beki chipukizi kutoka Azam Academy, Lusajo Mwaikenda, ndiye aliyeipatia bao pekee timu hiyo dakika ya 45 akimalizia krosi iliyopigwa na kiungo, Mudathir Yahya, kufuatia mpira wa kona alioanzishiwa na Bruce Kangwa. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh #UhaiDrinkingWater #TradegentsTanzaniaLimited