WAKATI zikiwa zimesalia siku mbili kabla ya Azam FC kumenyana na Biashara United, kikosi hicho kimejinasibu kuendelea kupata matokeo mazuri ili kufikia malengo yake. Mabingwa hao wa makombe mawili msimu huu baada ya kufanikiwa kutetea Kombe la Kagame na Mapinduzi Cup, wamekuwa kwenye mwenendo mzuri msimu huu hadi sasa ikishika nafasi ya pili kwenye za Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL) ikiwa na pointi 44. Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz Nahodha wa Azam FC, Agrey Moris, amesema kuwa wanajua mchezo utakuwa mgumu lakini watajipanga vema kuweza kupata matokeo. “Biashara ni timu nzuri ukiangalia wamepata kocha mpya kwa vyovyote timu inayopata kocha mpya wachezaji wanakuwa wanajitolea mara mbili zaidi ya mwanzo ila kama sisi Azam siku zote tunajipanga kuhakikisha tunapata matokeo kwenye michezo yetu. “Kwa sababu hii ni ligi ni safari ndefu bila kushinda mechi inayokuja mbele huwezi ukafikia lengo, tumejipanga vizuri wachezaji wote wako vizuri tutahakikisha tunapata matokeo kwenye mchezo huo,” alisema mchezaji huyo wa muda mrefu wa Azam FC. Kihistoria timu hizo zimekutana mara moja tu kwenye ligi, tokea Biashara ipande kucheza Ligi Kuu msimu huu, ambapo mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Karume, mjini Musoma uliisha kwa suluhu. #TimuBoraBidhaaBora #AfricanFrutiImenogaFresh #UhaiDrinkingWater #TradegentsTanzaniaLimited
KLABU ya Azam FC imeanza vema kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania (VPL) msimu 2020/2021 baada ya kuichapa Polisi Tanzania bao 1-0 kwenye mchezo wa kwanza. Bao pekee la Azam FC limewekwa kambani na mshambuliaji Obrey Chirwa, dakika ya 44 akiunganisha krosi safi ya mshambuliaji mpya, Prince Dube. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora #SARAFU #AzamUkwaju #AzamUbuyu #AzamStrawberry #UhaiDrinkingWater
#ObreyChirwa #IddNado #AzamFC #SingidaUnited Azam FC imeandika rekodi ya kwanza baada ya kupata ushindi mnono wa kihistoria kwenye mechi za mashindano, ikiichapa Singida United mabao 7-0, ukiwa ni mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL). Mabao ya Azam FC yalifungwa na Obrey Chirwa akifunga manne, Idd Seleman 'Nado', akifunga mawili huku jingine wakijifunga wenyewe Singida United. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora
KLABU ya Azam FC imeendelea pale ilipoishia kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) baada ya kuichapa Mbaoa mabao 2-0 jana Jumapili usiku. Mabao ya Azam FC yalifungwa na washambuliaji Richard Djodi na Shaaban Chilunda. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora
HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON
Kikosi cha Azam FC kimeendeleza wimbi la ushindi ugenini kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) kwa kupata ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Alliance. Mabao matatu ya Obrey Chirwa (hat-trick) na mawili ya Shaaban Chilunda, yalitosha kabisa kuihakikishia ushindi mwingine Azam FC mkoani Mwanza, ikifanikiwa kuvuna pointi zote sita. #ObreyChirwa #ShaabanChilunda #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora