GOLI LA MEDDIE KAGERE - SIMBA VS AZAM FC 1 -0
GOLI LA MEDDIE KAGERE - SIMBA VS AZAM FC 1 -0

GOLI LA MEDDIE KAGERE - SIMBA VS AZAM FC 1 -0 MEDDIE Kagere, mshambuliaji wa Simba ameendeleza moto wake wa kucheka na nyavu baada ya kupachika bao lake la saba ndani ya ligi na kuipa pointi tatu timu ya Simba mbele ya Azam FC. Mchezo wa leo ambao umechezwa uwanja wa Taifa ulikuwa na ushindani mkubwa na ulitawaliwa na ubabe mwingi kutokana na kila timu kuhitaji kupata pointi tatu. Simba wakiwa wenyeji wa mchezo iliwabidi wasubiri mpaka dakika ya 49 kuandika bao la kuongoza lililopachikwa kimiani na Kagere akimalizia pasi ya Francis Kahata kwa kichwa. Ushindi huo unaifanya Simba kuzidi kujikita kileleni ikiwa na pointi 15 na imecheza michezo mitano kwa kusepa na pointi zote tatu. Beki wa Simba, Pascal Wawa ndiye alikuwa nyota wa mchezo kwani aliokoa hatari nyingi kutoka kwa Chirwa ambaye alikuwa msubufu langoni akihaha kupata goli la ushindi ila bahati haikuwa yao. Simba ilifanya mabadiliko kipindi cha pili kwa kumtoa Sharaf Shiboub nafasi yake ikachukuliwa na Clatous Chama, Hassan Dilunga alimpisha Miraj Athuman, Francis Kahata alimpisha Ibrahim Ajib kwa upande wa Azam FC alitoka Richard Djoud aliyempisha Chilunda, Frank Domayo alimpisha Donald Ngoma. YALIYOMO GLOBAL TV ONLINE (+255 657 955825 au +255 784 888982) --------------------------------------------------------------------------------------- HABARI MPYA DAILY: https://www.youtube.com/playlist?list... HISTORIA ZA VIONGOZI ZA KUSISIMUA: https://www.youtube.com/playlist?list... GLOBAL RADIO TV: https://www.youtube.com/playlist?list... EXCLUSIVE INTERVIEWS: https://www.youtube.com/playlist?li



SIMBA SC 2-1 MTIBWA SUGAR, Simba Walivyotua Taifa Kibabe
SIMBA SC 2-1 MTIBWA SUGAR, Simba Walivyotua Taifa Kibabe

Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars FULL TIME: SIMBA SC 2-1 MTIBWA SUGAR Dak ya 90+3, kadinya njano inakwenda kwa Salum Kanoni, dakika za jioni kabisa. Dakika zimeongezwa tatu kumaliza mpira, zimesalia mbili sasa. Dak ya 90, Jonas Mkude anaingia kuchukua nafasi ya Shiboub Dak ya 81, Imepigwa faulo ile kwake Kahata inamkuta na anajaribu kumalizia lakini mpira unamzidi kasi, golikiki. Dak ya 81, Mtibwa wanacheza faulo, inapigwa kuelekezwa langoni kwao, nafasi ya Simba kupata bao la tatu. Dak ya 79, Kahata anaingia kuchukua nafasi ya Chama. Dak ya 77, Kona nyingine kwa Simba, ni baada ya Kapombe kubabatizana na Kapombe. Inapigwa lakini inakuwa golikiki. Dak ya 74, Simba wanaanza tena upya, Yassin kwake Athuman, piga kwake Kado anadaka mpira. Dak 68, Mirajiiiiii, anaifungia Simba bao la pili kwa shuti kali akitoka kupokea pasi nzuri kutoka kwa Shiboub Dak ya 67, Mtibwa wanaonesha jitihada za kulinda zaidi eneo lao na wakifanya mashambulizi ya kushtukiza kwa Simba. Dak ya 63, Simba wamefanya shambulizi la kutisha langoni mwa Mtibwa lakini mawasiliano yamekuwa si mazuri na Mtibwa wanaokoa. Dak ya 62, Miraji Athuman anaingia kuchukua nafasi ya Hassan Dilunga. Dak ya 60, Simba wameanza tena, Chama anachukua, anampasia Nyoni, wanajribu kupenya ngome ya Mtibwa, kwake Kagere lakini Mtibwa wanawadhibiti. Dak ya 57, Tayari Kado ameshasimama na mpira umeshaanza, Simba wanaanza kwa kupasiana vema langoni mwa Mtibwa, unamkuta kwake Chama, anapiga shuti ambalo linapaa nje ya lango. Dak ya 55, Mpira umesimama, Kado ameumia, Kahata naye anaonekana kama anataka kuchukua nafasi ya mtu. Dak ya 52, Kado anaokoa nafasi nyingine kutoka kwa Yassin aliyepata nafasi ya kufunga, kama angekuwa dhaifu angeshafungwa zaidi ya bao mbili. Dak ya 52, Kagere anaotea, anaonekana kulalamika kwa kuonesha ana njaa ya kufunga. Dak ya 49, Aishi Manula anaanzisha upya mashambulizi, ni kipindi cha pili sasa. MAPUMZIKO: SIMBA SC 1-1 MTIBWA SUGAR Dak ya 47, Chama amepiga lakini inakwenda nje. Dak ya 46, Humud anapewa kadi ya njano baada ya kucheza madhambi, ni ya kwanza ndani ya dakika 45 za kwanza, ni faulo. Dak ya 44, Fraga anababatizana na mchezaji wa Mtibwa, mpira unakwena nje, unarushwa kuelekea Mtibwa. Dak ya 42, Tayari Shiboub alishaamka, na zikiwa zimesalia dakika mbili mpira kwenda mapumziko. Dak ya 41, Shiboub anafanyiwa madhambi, na mpira umesimama kwa muda. Dak ya 38, Kanoni anatolewa nje na machela baada ya kuumia, matokeo bado ni 1-1. Dak ya 37, Chamaaaaa, pata nafasi moja maridadi kabisa lakini shuti lake linakwenda moja kwa moja kwa Kado kwa kulidaka. Dak ya 33, Inapigwa lakini inakwenda moja kwa moja kwa Manula ambaye anapangua na kuuelekeza eneo la kati mwa uwanja. Dak ya 32, Mtibwa wanapata faulo, anakwenda kupiga Salum Kanoni, piga mkwaju mkali unapanguliwa na Manula, inakuwa kona. Dak ya 31, Mtibwa wanajichanganya eneo lao la ulinzi, Simba wanaudaka kwake Kagere, bahati si yake. Kipa anadaka. Dak ya 30, ni kona nyingine inapigwa kuelekezwa Mtibwa, anapiga Chama, piga kule lakini inababatizwa na wachezaji wa Simba, golikiki. Dak ya 28, Mpira umesimama kwa muda, mchezaji wa Mtibwa ameumia. Dak ya 27, Offside kwa, mpira unachezwa na Mtibwa. Dak ya 25, Kapombe anapasiana na Chama eneo la kati mwa Uwanja, maelewano yanakuwa si mazuri, na mpira unakuwa golikiki, unaelekezwa Simba. Dak ya 24, Mpira unarushwa kuelekea lango la Mtibwa, ni karibu na eneo la kona, umesharushwa na unatolewa tena. Dak ya 21, Rifat Hamis anaisawazishia Mtibw aSugar kwa mpira wa kichwa ulitokana na kona, ni 1-1. Dak ya 17, Goooli, Meddie Kagere anafunga bao la kwanza baada ya Simba kupasiana vema katika eneo la hatari, sasa ni 1-0. Dak ya 10, Golikiki imetokea upande wa Simba, wanaanza upya kwake Manula. Dak ya 9, Simba wanapata kona ya kwanza,wanapiga lakini inatolewa nje na Mtibwa, wanaenda kurusha, Chama anarusha. Dak ya 7, Simba wanatandaza pasi nzuri kuelekea Mtibwa, kwake Shomari Kapombe, anapiga krosi ambayo inashindwa kuzaa matunda. Dak ya 6, Kado anaokoa mpira uliopigwa na Chama akiwa peke yake, ni nafasi ambayo Simba wamngeshaandika bao. Dak ya 6, Bado Simba wanaonekana kuutawala mchezo zaidi ya Mtibwa kwa dakika hizi sita za mwanzo. Dak ya 4, Simba wanaanza faulo kwa kupasiana, anapiga Nyonii, inaokolewa na mabeki wa Mtibwa. Dak ya 3, Zimbwe Jr anakokotoa mpira na guu la kushoto kushoto mwa uwanja, mchezaji Awadhi Salum wa Mtibwa anashikana mkono, faulo. Dak ya 3, Manula anadaka mpira, anaanzisha mashambulizi upya. Dak ya 2, Rifat Hamis wa Mtibwa anapandisha mashambulizi kwenda Simba, ni la kwanza. Dak ya 1, mechi imeshaanza Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, na Simba wameanza kwa kushambulia kwa kasi lango la Mtibwa. Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/Kidanistars



MBELGIJI SIMBA AMTAJA ATAKAYEMPA CHANGAMOTO MPYA AISHI MANULA NDANI YA SIMBA
MBELGIJI SIMBA AMTAJA ATAKAYEMPA CHANGAMOTO MPYA AISHI MANULA NDANI YA SIMBA

#BENOKakolanya mlinda mlango mpya wa Simba ambaye amesaini kandarasi ya miaka miwli akitokea Yanga amemkosha, Patrick #Aussems kutokana na uwezo wake. Kakolanya alianza kwenye mchezo wa kwanza wa kimataifa hatua ya awali dhidi ya UD Songo nchini Msumbiji na hakuruhusu nyavu zake kuguswa licha ya kukumbwa na hatari nyingi langoni mwake. Aussems amesema: “Kakolanya anafanya vizuri, sina wasiwasi tena kama ilivyokuwa msimu uliopita nilivyokuwa nikipata taabu pindi Manula akiumia. “Mechi zote alizocheza amefanya vizuri kwa hiyo ni matumaini yangu kuwa kadiri siku zinavyoenda atakuwa bora zaidi na atatoa changamoto kubwa #Manula,"



SIMBA SC 0-0 AZAM FC; FULL HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 13/05/2019)
SIMBA SC 0-0 AZAM FC; FULL HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 13/05/2019)

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara Simba SC wameng’ang’aniwa kwenye Uwanja wa Uhuru kwa kulazimishwa sare ya bila kufungana na Azam FC. Timu zote zilionesha soka la kiwango cha juu ambapo Simba walifanya mashambulizi mengi zaidi langoni kwa Azam lakini walishindwa kupata bao kutokana na uimara wa safu ya ulinzi ya Azam iliyokuwa chini ya Agrey Moris na Yakubu Mohamed. Licha ya kushambuliwa zaidi, Azam walipoteza nafasi mbili za wazi kupitia kwa Donald Ngoma dakika ya 29 na Obrey Chirwa dakika ya 87, hivyo mchezo kumalizika kwa suluhu. Matokeo hayo yanaifanya Simba kubakiza pointi nane pekee ili kutetea taji lake, ikiwa imefikisha pointi 82 na mechi tano mkononi, wakati wapinzani wao wa karibu, Yanga wakiwa na pointi 81 na mechi tatu mkononi. Azam wao wanaendelea kukaa nafasi ya tatu wakifikisha pointi 69 na mechi mbili mkononi.



SIMBA SC 0-1 KAGERA SUGAR; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 10/05/2019)
SIMBA SC 0-1 KAGERA SUGAR; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 10/05/2019)

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara leo wameangukia pua baada ya kuchapwa bao 1-0 na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Bao la Kagera kwenye mchezo wa leo limepatikana baada ya beki wa Simba Mohamed Hussein Zimbwe Jr kujifunga dakika ya 42 wakati akijaribu kuokoa hatari langoni mwake baada ya kuchanganyana na kipa wake Aishi Manula. Ushindi huo ni mwendelezo wa ubabe wa timu hiyo kutoka mkoani Kagera kwa Mnyama Simba, baada ya awali kuipa kichapo cha mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Kaitaba Bukoba katika mchezo wa kwanza msimu huu. Matokeo hayo yameineemesha Kagera Sugar katika jitihada za kuepuka kushuka daraja, ikifikisha pointi 43 na kukaa nafasi ya 10 huku Simba wakisalia kileleni na pointi 81.



Goli la kujifunga la Zimbwe Jr: Simba SC 0-1 Kagera Sugar (TPL - 10/05/2019)
Goli la kujifunga la Zimbwe Jr: Simba SC 0-1 Kagera Sugar (TPL - 10/05/2019)

Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara leo wameangukia pua baada ya kuchapwa bao 1-0 na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam. Bao la Kagera kwenye mchezo wa leo limepatikana baada ya beki wa Simba Mohamed Hussein Zimbwe Jr kujifunga dakika ya 42 wakati akijaribu kuokoa hatari langoni mwake baada ya kuchanganyana na kipa wake Aishi Manula. Ushindi huo ni mwendelezo wa ubabe wa timu hiyo kutoka mkoani Kagera kwa Mnyama Simba, baada ya awali kuipa kichapo cha mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Kaitaba Bukoba katika mchezo wa kwanza msimu huu. Matokeo hayo yameineemesha Kagera Sugar katika jitihada za kuepuka kushuka daraja, ikifikisha pointi 43 na kukaa nafasi ya 10 huku Simba wakisalia kileleni na pointi 81.



MBAO FC 0-1 COASTAL UNION: HIGHLIGHTS (TPL - 11/02/2019)
MBAO FC 0-1 COASTAL UNION: HIGHLIGHTS (TPL - 11/02/2019)

Coastal Union imefanikiwa kuchukua pointi tatu ugenini kwa kuichapa Mbao FC bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Licha ya Mbao kumiliki zaidi mpira na kufanya mashambulizi mengi langoni kwa Coastal, nafasi pekee aliyoipata Raizin Hafidh dakika ya 60 aliitumia na kuipatia Coastal bao pekee lililoipa alama tatu ugenini



Bao la Coastal Union: Mbao FC 0-1 Coastal Union (TPL - 11/02/2019)
Bao la Coastal Union: Mbao FC 0-1 Coastal Union (TPL - 11/02/2019)

Coastal Union imefanikiwa kuchukua pointi tatu ugenini kwa kuichapa Mbao FC bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Licha ya Mbao kumiliki zaidi mpira na kufanya mashambulizi mengi langoni kwa Coastal, nafasi pekee aliyoipata Raizin Hafidh dakika ya 60 aliitumia na kuipatia Coastal bao pekee lililoipa alama tatu ugenini.




« Previous Next »


Popular Tags

#Goal Celebrations  #LeBron James  #Gareth Bale  #Shaquille O'Neal  #Golden State Warriors  #Counter Attack Goals Football  #Counter Attack Goals Football  #Paul Pogba  #Michael Jordan  #Zlatan Ibrahimovi  

Popular Users

#DwyaneWade  #nyt4thdownbot  #floydmayweather  #geniebouchard  #Harry_Styles  #NiallOfficial  #JohnCena  #UKCoachCalipari  #baseballpro  #obj  #alexmorgan13  #BBCBreaking  #steveaustinBSR  #itsBayleyWWE  #fauxpelini