Simba SC imepata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ihefu SC, mchezo wa ligi kuu ya NBC ulipigwa kwenye Dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Simba imetangulia kwa goli la Jean Baleke dakika ya 13 lakini Ihefu wakachomoa dakika ya 25 kupitia kwa Ismail Mgunda na 'super sub, Moses Phiri akatia kitu cha pili dakika ya 65. Tazama highlights.....
Kuna #hattrick kutoka kwa Jean Baleke dakika ya 28 za kwanza na pia kuna mengine mawili kutoka kwa Saidi Ntibazonkiza na Pape Ousman Sakho dakika ya 40 na 90+5… Simba wakapata ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Ihefu SC kwenye Dimba la Azam Complex, Chamazi. Ni mechi ya robo fainali ya #AzamSportsFederationCup ikishuhudia Ihefu wakipata bao la kufutia machozi kupitia kwa Raphael Daud Loth dakika ya 61 na Simba kwenda nusu fainali ambako watakutana na Azam FC kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara.
magoliyasimba #golilasakho #golilasako #simbavsihefu #magoliyaligikuu #magoliyote #mechizasimba.