Leo Simba itakuwa kibaruani kumenyana na Coastal Union mchezo wa ligi kuu Uwanja wa Mkwakwani huku ikitarajiwa kuwakosa nyota wake wawili ambao wanasumbuliwa na majeruhi. #Wawa #Murshid #Simba #DreamOnlineTv
Viporo vyaanza kumtia presha Kocha Aussems, Coastal Union yajipanga kuiduwaza Simba #DreamOnlineTv #Simba #Aussems Simba baada ya kutolewa katika Ligi ya Mabingwa sasa inaanza kupambana katika ligi ikiwa na mechi nyingi mkononi
Hata hao wanaobeza penalti ya John Bocco watambue Simba hii ni moto wa kuotea mbali na usishangae kuona mpira umetangulia Lubumbushi na wachezaji wanakwenda kumalizia kazi #DreamOnlineTv #Simba #TPMazembe
Beki Wawa ameichezea Simba katika michezo yote ya Ligi ya Mabingwa kabla ya kuumia dhidi ya TP Mazembe, Inawezekana kabisa kuwa ni pigo kubwa kwa klabu ya Simba ambapo mchezaji wake kutoka Ivory Coast, Serges Wawa, atakuwa nje ya dimba kwa muda wa wiki mbili. #DreamOnlineTv #TPMazembe #Simba #Wawa
KIUNGO mpaka rangi wa Simba, Clatous Chama raia wa Zambia, amehuzunika kwa kushindwa kuwafunga TP Mazembe kwenye Dimba la Taifa lakini akaweka wazi kwamba hukohuko kwao DR Congo watafungika. #DreamOnlineTv #Cham #ThisisSimba #Congo
KUTOKANA na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (Caf) kufanya mabadiliko ya waamuzi wa mchezo wa Ligi ya Mabingwa hatua ya robo fainali kati ya TP Mazembe na Simba uongozi wa Simba umeandika barua kwa Caf.#DreamOnlineTv #Tanzania #Simba
UONGOZI wa timu ya Simba umetoa tamko baada ya kulalamikia mabadiliko ya ghafla ya waamuzi wa mchezo wa marudiano kwenye mchezo wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya TP Mazembe, utakaochezwa Mjini Lubumbashi Jumamosi ya Aprili 13. #DreamOnlineTv #Manara #simba #Waamuzi
NAHODHA wa TP Mazembe, Rainford Kalaba, amesema kuwa kitendo chao cha kushindwa kupata bao lolote katika mchezo wa juzi Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa dhidi ya Simba kimewaweka katika nafasi mbaya ya kutinga hatua ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika. #DreamOnlineTv #TPMazembe #DrCongo