GOLI LA OKWI SIMBA 1-0 AZAM
GOLI LA OKWI SIMBA 1-0 AZAM

Please watch: "MAGOLI YOTE YA SIMBA 5 - 0 MBAO" https://www.youtube.com/watch?v=lU7L3hP4BP0 --~-- SIMBA SC imezidi kuwaacha mbali wapinzani katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Azam FC jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Hongera kwake mfungaji wa bao pekee la leo, mshambuliaji Mganda Emmanuel Arnold Okwi aliyefunga dakika ya 36 baada ya kutokea patashika kwenye lango la Azam FC kufuatia krosi ya beki Mghana, Asante Kwasi. Simba SC sasa inafikisha pointi 41 baada ya kucheza mechi 17, wakiwazidi kwa pointi saba, mabingwa watetezi, Yanga SC wenye pointi 34 katika nafasi ya pili na Azam FC wanabaki nafasi ya tatu kwa pointi zao 33. Dalili za Simba inayofundishwa na kocha Mfaransa, Pierre Lechantre anayesaidiwa na Mrundi, Masoud Juma kupata bao zilionekana mapema tu mchezo huo ulipoanza kutokana na mashambulizi yake mfululizo langoni mwa wapinzani. Azam FC walizidiwa katika safu ya kiungo na kujikuta wanawapa fursa Simba kutawala mchezo sehemu kubwa ya kipindi cha kwanza. Benchi la Ufundi la Azam chini ya Mromania, Aristica Cioaba ba mzalendo, Iddi Cheche liliona hilo na mapema kipindi cha pili wakamuingiza kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’ kwenda kuchukua nafasi ya mshambuliaji Iddi Kipagwile. Mabadiliko hayo yaliipa uhai Azam FC na kuanza kupeleka mashambulizi makali langoni mwa Simba, lakini kipa namba moja nchini, Aishi Manula alisimama imara kuokoa akisaidiwa na mabeki, Yussuph Mlipili na Erasto Nyoni. Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Aishi Manula, Shomary Kapombe, Erasto Nyoni, Yussuph Mlipili, Asante Kwasi, Jonas Mkude, Shiza Kichuya, Said Ndemla/Muzamil Yassin dk59, John Bocco, Emmanuel Okwi/Nicholaus Gyan dk84 na James Kotei. Azam FC; Razak Abalora, Daniel Amoah, Bruce Kangwa, Yakubu Mohammed, Aggrey Morris, Stephan Kingue, Iddi Kipagwile/Salum Abubakar ‘Sure Boy’ dk55, Frank Domayo, Mbaraka Yussuph, Yahya Zayed/Bernard Arthur dk71 na Enock Atta-Agyei.



MASHABIKI RUVU SHOOTING WAKISHANGILIA USHINDI WA KWANZA DHIDI YA NDANDA FC
MASHABIKI RUVU SHOOTING WAKISHANGILIA USHINDI WA KWANZA DHIDI YA NDANDA FC

MASHABIKI RUVU SHOOTING WAKISHANGILIA USHINDI WA KWANZA DHIDI YA NDANDA FC Na Omary Mngindo, Mlandizi, Kibaha Vijijini, Pwani, Tanzania- Nov 18 BAO la pekee la timu ya soka ya Ruvu Shooting dhidi ya Ndanda Fc ya Mtwara lililofungwa na Abdulhaman Mussa kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) limepokelewa kwa shangwe, furaha na vifijo kutoka kwa mamia ya mashabiki wa timu hiyo wengi wao wakiwa vijana waliojiunga na Kikosi cha JKT kwa ajli ya mafunzo. Bao hilo lililofungwa kwa mkwaju wa penati na nyota huyo aliyekuwa mfungaji bora katika Ligi ya msimu uliopita akifungana na kiungo aliyekuwa anakitumikia kikosi cha Yanga Simon Msuva, limeiwezesha timu hiyo kupata ushindi wa kwanza kwenye kinyang'anyiro hicho tangu kuanza kwa ligi ya msimu huu. MWISHO.




« Previous


Popular Tags

#Kevin Durant  #Kyrie Irving  #Paul Pogba  #Best Ball Controls  #Shot Goals  #Shaquille O'Neal  #Cristiano Ronaldo  #James Harden  #Michael Jordan  #Football Skills  

Popular Users

#TimTebow  #sydneyleroux  #katyperry  #KingJames  #steveaustinBSR  #ArianFoster  #cesc4official  #HEELZiggler  #BadgerMBB  #baseballpro  #floydmayweather  #dougferguson405  #instagram  #b_ryan9  #SportsCenter