Waandishi wa habari waandamizi wa nchini Tunisia, Umaima Jubeli kutoka Radio Express FM na Hosni Gharbi wa Tunisia Press Agency waimwagia sifa Simba SC kuelekea mechi ya leo dhidi ya CS Sfaxien ya nchini humo. Ni mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika na itapigwa leo Jumapili ya Januari 5, 2025 saa 1:00 usiku LIVE #AzamSports1HD #SimbaSC #CSSfaxien #CAFCC #SimbaTunisia
Yanga imekuwa timu ya kwanza kushinda 5-0 kwenye ligi kuu msimu huu, wakiwachakaza Fountain Gate FC kwenye Dimba la KMC Complex, Dar es Salaam. Magoli ya Yanga yamefungwa na Pacome Zouzoua aliyefunga mawili, Mudathir Yahya, Jackson Shiga aliyejifunga na Clement Mzize dakika ya 88. haya hapa magoli yote...
Fabrice Ngoma amefunga goli pekee na la ushindi, Simba ikiitandika Singida Black Stars bao 1-0 nyumbani kwao kwenye Dimba la Liti.... Hii ni Ligi Kuu ya NBC #NBCPremierLeague
Goli pekee la mkwaju wa penati dakika za nyongeza limeipa Simba alama tatu muhimu kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Tanzania, mchezo ukipigwa kwenye Dimba la KMC Complex, Mwenge Dar es Salaam. Mfungaji wa goli ni Jean Charles Ahoua....
Beki Ibrahim Hamad Abdullah Bacca amefunga magoli mawili katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Tanzania Prisons, mchezo wa ligi kuu ya NBC uliopigwa KMC Complex, Mwenge Dar es Salaam. Magoli mengine kwenye mchezo huo yametoka kwa Prince Dube na Clement Mzize ambaye ndiye aliyefungua ukurasa wa mabao....
Hatimaye Simba imevunja mwiko wa kutopata ushindi kwenye Uwanja wa Kaitaba dhidi ya Kagera Sugar, baada ya leo kuitandika magoli 5-2, mchezo wa ligi kuu ya NBC Tanzania. Magoli ya Simba yametoka kwa Shomary Kapombe 13', Jean Charles Ahoua 44', Fabrice Ngoma 53, na Stephen Desse Mukwala aliyefunga mawili dakika ya 66 na 85. Magoli ya Kagera Sugar yamefunga na Datius Peter dakika ya 79 na Cleophace Mkandala dakika ya 90. Ilikuwa ni mechi ambayo pia imemshuhudia kwa mara ya kwanza kiungo mpya wa Simba, Ellie Mpanzu aliyecheza kwa takriban dakika 70.
Tazama magoli yote matano yaliyofungwa kwenye mchezo wa NBC Premier League kati ya Yanga SC dhidi ya Mashujaa FC. Yanga imeshinda kwa jumla ya magoli 3-2 Magoli yote matatu ya Yanga yamefungwa na Prince Dube Magoli ya Mashujaa FC yamefungwa na Idrisa Stambuli na David Ulomi