Simba yaichapa Carabat FC 2-0, Bajaber, Sowah wacheka na nyavu
Simba yaichapa Carabat FC 2-0, Bajaber, Sowah wacheka na nyavu

KUTOKA MISRI: Kikosi cha Simba kilichopo Misri, katika maandalizi ya msimu mpya wa NBC Premier League na mashindano ya kimataifa, kimecheza mchezo wa kwanza wa kirafiki wa kujipima nguvu na timu ya Carabat FC, ambapo Mnyama ameshinda magoli 2-0. Goli la kwanza lilifungwa kipindi cha kwanza na mchezaji Mohammed Bajaber huku goli la pili likifugwa kipindi cha pili na Jonathan Sowah. Wachezaji wote wawili wamesajiliwa msimu huu. #Simba #KambiYaSimba



SIMBA SC: Elie Mpanzu aanza 'tizi' kambini Misri ; Meneja Simba amaliza utata kuhusu uhalali wake
SIMBA SC: Elie Mpanzu aanza 'tizi' kambini Misri ; Meneja Simba amaliza utata kuhusu uhalali wake

KUTOKA MISRI | “….hakuna kiumbe yeyote anayeweza kujiita Eliiiii zaidi ya Simba SC” Kikosi cha Simba SC kikiwa kambini nchini Misri, jioni ya leo kimepiga tizi lililomuhusisha pia kiungo wao Elie Mpanzu ambaye ameripoti kambini hapo leo… Katika tizi hizo hilo, meneja wa kikosi hicho, Patrick Rweyemamu amefafanua machache kuhusu utata uliokuwepo juu ya mchezaji huyo, akisema “…ni propaganda…ni Gen-z ambao wameingia kwenye mfumo wa kisasa wa mpira” Rweyemamu amesema klabu hiyo haiwezi kufanya makosa ya kumsajili mchezaji wa aina hiyo kwa mkataba wa miezi sita na kusisitiza kuwa “…Elie Mpanzu yupo, na ataendelea kuwepo hadi Simba itakavyoamua vinginevyo



Highlights | Tanzania 1-0 Uganda | CECAFA 3 Nations Tounarment 22/07/2025
Highlights | Tanzania 1-0 Uganda | CECAFA 3 Nations Tounarment 22/07/2025

Goli pekee la Idd Selemani 'Nado' limeipa Tanzania #TaifaStars pointi tatu kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Uganda, katika mchezo wa ufunguzi wa michuano maalum ya CECAFA 3 Nations Tounarment #CECAFA3NT inayopigwa kwenye Uwanja wa Black Rhino, Karatu mkoani Arusha...



Yanga yatoa siri jinsi ilivyomnasa kiungo Moussa Balla Conte
Yanga yatoa siri jinsi ilivyomnasa kiungo Moussa Balla Conte

“…tuliweka kiwango kizuri cha fedha kumshawishi mchezaji na klkabu yake” Nneno la Ally Kamwe kuhusu usajili wa kiungo Moussa Balla Conte ambaye leo ametua rasmi Jangwani kwa mkataba wa miaka mitatu… Kamwe ameeleza jinsi ilivyokuwa ngumu kumpata na jinsi walivyoweza kumshawishi yeye na klabu yake licha ya kuwa na ofa nyingi….. Kuhusu hatma ya Khalid Aucho, Kamwe amesema majibu yatatoka Julai 20 baada ya kupokea ripoti ya CEO wa klabu hiyo… Mwisho, Ally Kamwe anatoa ujumbe kwa walioumizwa na usajili huo akiomba kusajiliwa na timu inayohitaji mchezaji mwenye jina la Conte…. #YangaSC #Usajili #BallaConte



Yanga SC 2-0 Simba SC | Highlights | Kariakoo Derby | NBC PL 25/06/2025
Yanga SC 2-0 Simba SC | Highlights | Kariakoo Derby | NBC PL 25/06/2025

KARIAKOO DERBY | Magoli ya Pacome Zouzoua kwa penati na Clement Mzize yameipa Yanga pointi tatu muhimu dhidi ya mtani wake Simba SC na kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC 2024/25 baada ya kufikisha alama 82 dhidi ya 78 za Simba... Huu ulikuwa ni mchezo wa mwisho wa msimu ambao pia ulikuwa ukisubiriwa kutoa maamuzi ya nani awe bingwa wa ligi hii msimu huu... Mbungi imepigwa kwenye Dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.



#KariakooDerby |  Ramadhan Ngoda alivyoifungua Dabi ya Kariakoo ya kufungia msimu na kuamua bingwa
#KariakooDerby | Ramadhan Ngoda alivyoifungua Dabi ya Kariakoo ya kufungia msimu na kuamua bingwa

Itazame Dar es Salaam, itazame Benjamin Mkapa, watazame watani wa jadi…!!! #NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #KariakooDerby #DabiYaKariakoo #HainaKipengele #YangaSC #SimbaSC #YangaSimba #WataniWaJadi



Tanzania Prisons 0-5 Yanga SC | Highlights | NBC Premier League 18/06/2025
Tanzania Prisons 0-5 Yanga SC | Highlights | NBC Premier League 18/06/2025

Yanga SC imeichakaza Tanzania Prisons kwa kichapo cha mabao 5-0 kwenye mchezo wa raundi ya 29 Lig kuu ya NBC uliopigwa Sokoine Stadium, Mbeya... Pacome Zouzoua amefunga magoli mawili, huku mengine yakitoka kwa Mudathir Yahya aliyefungua milango dakika ya 31, Clatous Chama, na Israel Mwenda..




« Previous Next »


Popular Tags

#Best Ball Controls  #Best Goalkeeper Saves  #Franck Ribery  #Cristiano Ronaldo  #Goal Celebrations  #Zlatan Ibrahimovi  #Kyrie Irving  #Best Goalkeeper Saves  #Football Defensive Skills  #Cleveland Cavaliers  

Popular Users

#darrenrovell  #RobGronkowski  #normmacdonald  #THNRyanKennedy  #sportspickle  #MieshaTate  #CMPunk  #CNN  #akshaykumar  #hunterpence  #twitter  #taylorswift13  #billsimmons  #ddlovato  #britneyspears