Azam TV's user profile page. Match highlights, posts and more on site!“” Report User |
"Wachezaji wako tayari, viongozi wako tayari" - Maneno yaliyosikika wakati Meneja wa Habari na Mawasiliano wa @yangasc, @alikamwe akifanya mahojiano na viongozi wa msafara waliombatana nao DR Congo kwa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya TP Mazembe. Aidha, Kamwe ameeleza kwamba mashabiki wa Yanga tayari wapo mjini Lubumbashi kwa ajili ya kuwapa nguvu wachezaji kwenye mchezo huo wa Jumamosi Desemba 14, 2024. Game itapigwa saa 10:00 jioni na itakuwa LIVE #AzamSports1HD Mhariri ✍ @abuuyusuftz #CAFChampionsLeague #LigiYaMabingwaAfrika #CAFCL #YangaSC #TPMazembe
Yanga imerejea kwenye njia ya ushindi baada ya kupoteza mechi mbili mfululizo, ambapo leo imeshinda 2-0 ugenini dhidi ya Namungo FC, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa Majaliwa Stadium, Ruangwa, Lindi. Magoli ya Yanga yametoka kwa Kennedy Musonda dakika ya 50 na Pacome Zouzoua dakika ya 68.
Yanga imerejea kwenye njia ya ushindi baada ya kupoteza mechi mbili mfululizo, ambapo leo imeshinda 2-0 ugenini dhidi ya Namungo FC, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa Majaliwa Stadium, Ruangwa, Lindi. Magoli ya Yanga yametoka kwa Kennedy Musonda dakika ya 50 na Pacome Zouzoua dakika ya 68.
Azam FC imeitandika Singida Black Stars mabao 2-1 katika mchezo wa ligi kuu ya NBC Tanzania Bara uliopigwa kwenye Dimba la Azam Complex, Chamazi..... Magoli ya Azam FC yametoka kwa Feisal Salum na Jhonier Blanco huku Singida wakpata bao lao kupitia kwa Elvis Rupia...
Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo wa NBC Premier League kati ya Pamba Jiji dhidi ya Simba SC. Simba imeshinda kwa goli 1-0 na mfungaji ni Leonel Ateba.
Yanga SC imepoteza mchezo wa pili mfululizo kwenye ligi baada ya kukubali kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa tabora United, mchezo wa ligi kuu ya NBC uliopigwa leo Azam Complex, Chamazi. Offen Chikola amefunga magoli mawili dakika ya 19 na 45 ... huku Nelson Munganga akifunga la tatu dakika ya 78. Goli la kufutia machozi kwa Yanga limefungwa na Clement Mzize dakika ya 90. Yanga pia walipata penati dakika ya 45 ikipigwa na Stephane Aziz ki lakini ikadakwa na golikikpa Hussein Masalanga....
Simba SC imeichakaza KMC mabao 4-0 katika mchezo wa ligi kuu ya NBC uliopigwa leo kwenye Dimba la KMC Complex, Mwenge Dar es Salaam..... Magoli ya Simba yamefungwa na Awesu Ally Awesu dakika ya 25, Jean Charles Ahoua mawili dakika ya 38' kwa penati na dakika ya 69', na lingine limetoka kwa Edwin Balua dakika ya 66. Haya hapa magoli yote manne.....
Baada ya kushinda mechi nane mfululizo, Yanga SC leo imepoteza kwa mara ya kwanza kwa kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Azam FC, mchezo wa ligi kuu ya NBC uliopigwa kwenye dimba la Azam Complex, Chamazi. Goli pekee la mchezo limefungwa na Gibril Sillah dakika ya 33 ikiwa ni dakika 10 baada ya beki wa Yanga kutolewa kwa kadi nyekundu..... Hili hapa ni goli na kilichosababisha kadi nyekundu...
Matukio kwa ufupi kwenye mechi ya FKF Premier League wakati Tusker akiondoka na ushindi wa goli moja dhidi ya Kariobangi ...
Tazama matukio muhimu na kwa ufupi yaliyojiri kwenye mchezo wa FKF Premier League uliozikutanisha Gor Mahia dhidi ya AFC ...
Tazama Polisi Tanzania ilivyoichakaza Mtibwa Sugar katika mchezo wa NBC Premier League. Magoli ya Polisi yalifungwa ...
Tazama matukio na magoli yaliyoipa ushindi Namungo FC dhidi ya Azam FC, mabao ya Namungo yamefungwa na Hassan ...
Tazama matukio na goli pekee la Edwin Balua wa Tanzania Prisons lililotosha kabisa kuwapa alama tatu 'Wajelajela'.
Goli pekee la Mubarak Hamza akipeleka ushindi kwa Wagosi wa Kaya dhidi ya Ihefu kwenye mchezo wa NBC Premier League.
Haya hapa matukio mbalimbali yaliyojiri katika Uwanja wa Nyankumbu, Mjini Geita wakati Mbeya City akiondoka na ushindi wa ...