Magoli | Azam FC 2-2 Simba SC | NBC Premier League 24/02/2025
Magoli | Azam FC 2-2 Simba SC | NBC Premier League 24/02/2025

MZIZIMA DERBY | Ni sare ya 2-2 kati ya Simba SC dhidi ya Azam FC, mchezo wa ligi kuu ya NBC, uliopigwa kwenye Dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Azam wametangulia kwa goli la Gibril Sillah dakika ya 01, kabla ya Elie Mpanzu kusawazisha dakika ya 25 na Abdulrazak Hamza kuongeza la pili dakika ya 76. Nyota wa mchezo ni ‘Super Sub’, Zidane Sereri ndiye aliyeweka mambo sawa kwa kuifungia Azam FC bao la kusawazisha dakika ya 88, kwa assist ya aina yake kutoka kwa Feisal Salum Feitoto.



Magoli na kadi nyekundu | Fountain Gate 1-1 Simba SC | NBC Premier League 06/02/2025
Magoli na kadi nyekundu | Fountain Gate 1-1 Simba SC | NBC Premier League 06/02/2025

Simba SC imekabwa koo na kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Fountain Gate katika mchezo wa ligi kuu ya NBC uliopigwa kwenye Dimba la Tanzanite, Kwaraa, Babati Manyara... Simba wametangulia kupata bao kupitia kwa Lionel Ateba dakika ay 57 lakini kiungoLadack Chasambi akajifunga na kuisawazishia Fountain Gate dakika ya 75. Katika mchezo huu pia, Fountain Gate ilipata pigo kwa golikipa wake John Noble kutolewa kwa kadi nyekundu, ikiwa ni njano ya pili....



Magoli | Burkina Faso 1-2 Zanzibar Heroes | Fainali Mapinduzi Cup 13/01/2025
Magoli | Burkina Faso 1-2 Zanzibar Heroes | Fainali Mapinduzi Cup 13/01/2025

Timu ya taifa ya Zanzibar… #ZanzibarHeroes imeibuka na ubingwa wa Kombe la Mapinduzi 2025 kwa kuichapa Burkina Faso mabao 2-1 katika mchezo wa fainali uliopigwa leo kwenye Dimba Gombani, Pemba. Zanzibar walitangulia kupata bao dakika ya 41 kwa kisigino cha Ibrahim Hamad Hilika, kisha Burkina Faso wakachomo dakika ya 69 kupitia kwa Aboubacar Traore…. Lakini dakika za majeruhi, Hassan Ali Cheda akafunga la pili na la ushindi kwa Zanzibar.



Magoli | Tabora United 2-1 Azam FC | NBC Premier League 13/12/2024
Magoli | Tabora United 2-1 Azam FC | NBC Premier League 13/12/2024

Azam FC imekula mweleka ikipokea kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Tabora United mchezo wa ligi kuu ya NBC Tanzania Bara kwenye Dimba la Ali Hassan Mwinyi, Tabora. Heritier Makambo amefunga goli la kwanza kwa tabora United na kusababisha goli la pili ambalo golikipa Mohamed Mustafa amejifunga...... Goli pekee la Azam FC limefungwa na beki Yoro Diaby.




« Previous Next »


Popular Tags

#Shaquille O'Neal  #Anthony Davis  #Goalkeeper Saves  #Shot Goals  #Russell Westbrook  #Miami Heat  #Stephen Curry  #Franck Ribery  #Best Champions League  #Zlatan Ibrahimovi  

Popular Users

#shakira  #TheCUTCH22  #taylorswift13  #ArianaGrande  #Joey7Barton  #KimKardashian  #strombone1  #baseballpro  #SteveNash  #Harry_Styles  #sportspickle  #twitter  #MichelleDBeadle  #dougferguson405  #geniebouchard