MAGOLI YOTE YA GOR MAHIA VS JKU 1-0 KAGAME CUP Kocha wa Gor Mahia FC, Dylan Kerr, amelishauri Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kuwa mashindano ya KAGAME yatakayofanyika mwakani yasiwe na kiingilio. Kerr ambaye timu yake imemaliza mashindano hayo jana katika nafasi ya tatu baada ya kuifunga JKU mabao 2-0, ametoa ushauri huo ili mashabiki wajitokeze kwa wingi uwanjani. Kocha huyo ameeleza hayo akisema KAGAME ya mwaka huu haijafana kutokana na mechi zao nyingi walizocheza kukosa mashabiki hivyo ni vema kama yakafanyika bila kiingilio mwakani itakuwa vema zaidi. Uwepo wa mashabiki wengi Kerr anaamini unatia hamasa kubwa kwa wachezaji kujituma kwa nguvu zote Uwanjani kutokana na mchango wao mkubwa wa kushangilia, kitu ambacho kinatia morali kwa wachezaji. "Ni vema zaidi KAGAME ijayo ikafanyika bila kiingilio ili mashabiki wajitokeze kwa wingi Uwanjani sababu wanaleta hamasa kubwa kwa wachezaji, sioni haja ya kuweka kiingilio sababu yanakosa ladha" amesema Kerr. Fainali za KAGAME zimemalizika jana kwa Azam kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Simba SC na kufanikiwa kuutetea ubingwa huo baada ya kuutwaa kwa mara ya kwanza mwaka 2015 wakiifunga Gor Mahia FC kwa mabao 2-0. Install GlobalPublishersApp Android: http://bit.ly/2AAQe1d iOS: http://apple.co/2Assf4M Subscribe http://www.youtube.com/c/uwazi FACEBOOK: https://www.facebook.com/Globalpublis... TWITTER: https://twitter.com/GlobalHabari Visit https://globalpublishers.co.tz/, Subscribe http://www.youtube.com/c/uwazi1 Kupata video nyingine za aina hii, subscribe kwenye chanell yetu kwa kubofya… http://www.youtube.com/c/uwazi1 http://www.youtube.com/c/uwazi1 http://www.youtube.com/c/uwazi1 WEBSITE: https://globalpublishers.co.tz/ FACEBOOK: https://www.facebook.com/Globalpublis... TWITTER: https://twitter.com/GlobalHabari INSTAGRAM: https://www.instagram.com/globalpubli..
Rekodi ya Simba SC dhidi ya Azam FC ni ya kuvutia baada ya kukutana mara 29, katika mashindano yote Ligi Kuu , Kombe la Mapinduzi, Azam Sports Federation Cup, Kombe la Kagame, Kombe la Ujirani Mwema, Kombe la Banc ABC Super 8 na Ngao ya Jamii. Simba SC imeshinda mara 13 ikiwa ni pamoja na leo, Azam FC ikishinda 10 na mechi 6 zikimalizika kwa sare.
Singida United imepata ushindi wake wa nne mfululizo katika mashindano ya Kombe Mapinduzi yanayoendelea dimba la Amaan visiwani Zanzibar kwa kuichapa JKU mabao 2-0, mchezo uliopigwa leo Januari 06, mwaka huu