Yanga SC 2-0 Simba SC | Highlights | Kariakoo Derby | NBC PL 25/06/2025
Yanga SC 2-0 Simba SC | Highlights | Kariakoo Derby | NBC PL 25/06/2025

KARIAKOO DERBY | Magoli ya Pacome Zouzoua kwa penati na Clement Mzize yameipa Yanga pointi tatu muhimu dhidi ya mtani wake Simba SC na kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC 2024/25 baada ya kufikisha alama 82 dhidi ya 78 za Simba... Huu ulikuwa ni mchezo wa mwisho wa msimu ambao pia ulikuwa ukisubiriwa kutoa maamuzi ya nani awe bingwa wa ligi hii msimu huu... Mbungi imepigwa kwenye Dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.



#KariakooDerby |  Ramadhan Ngoda alivyoifungua Dabi ya Kariakoo ya kufungia msimu na kuamua bingwa
#KariakooDerby | Ramadhan Ngoda alivyoifungua Dabi ya Kariakoo ya kufungia msimu na kuamua bingwa

Itazame Dar es Salaam, itazame Benjamin Mkapa, watazame watani wa jadi…!!! #NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #KariakooDerby #DabiYaKariakoo #HainaKipengele #YangaSC #SimbaSC #YangaSimba #WataniWaJadi



Tanzania Prisons 0-5 Yanga SC | Highlights | NBC Premier League 18/06/2025
Tanzania Prisons 0-5 Yanga SC | Highlights | NBC Premier League 18/06/2025

Yanga SC imeichakaza Tanzania Prisons kwa kichapo cha mabao 5-0 kwenye mchezo wa raundi ya 29 Lig kuu ya NBC uliopigwa Sokoine Stadium, Mbeya... Pacome Zouzoua amefunga magoli mawili, huku mengine yakitoka kwa Mudathir Yahya aliyefungua milango dakika ya 31, Clatous Chama, na Israel Mwenda..



Simba SC 1-3 Singida Black Stars | Highlights | Nusu Fainali CRDB Bank Fed. Cup 31/05/2025
Simba SC 1-3 Singida Black Stars | Highlights | Nusu Fainali CRDB Bank Fed. Cup 31/05/2025

Magoli mawili ya Emmanuel Keyekeh na moja la Jonathan Sowah yameipa ushindi wa 3-1 Singida Black Stars dhidi ya Simba na kutinga fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank. Ni katika mchezo wa nusu fainali uliopigwa kwenye Dimba la Tanzanite Kwaraa, Babati Manyara ambapo Simba imepata goli lake la kufutia machozi kupitia kwa free-kick ya Jean Charles Ahoua. Kwa matokao haya, safari ya Simba imeishia hapa.... na Singida BS wanakwenda fainali kuwakabili Yanga...



Simba SC 1-0 Singida Black Stars | Highlights | NBC Premier League 28/05/2025
Simba SC 1-0 Singida Black Stars | Highlights | NBC Premier League 28/05/2025

Steven Mukwala amefunga goli pekee na la ushindi kwa Simba, dhidi ya Singida Black Stars, mchezo wa Ligi Kuuya NBC uliopigwa kwenye Dimba la KMC, Mwenge Dar es Salaam.



Yanga SC 2-0 JKT Tanzania | Highlights | CRDB Bank Federation Cup 18/05/2025
Yanga SC 2-0 JKT Tanzania | Highlights | CRDB Bank Federation Cup 18/05/2025

Yanga imetinga fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank kwa kuichapa JKT Tanzania mabao 2-0 kwenye mchezo wa nusu fainali uliopigwa Mkwakwani Stadium, jijini Tanga.... Magoli ya Yanga kwenye mchezo huu yamefungwa na Prince Dube dakika ya 41 na Mudathir Yahya dakika ya 90.



Simba SC 5-1 Pamba Jiji | Highlights | NBC Premier League 08/05/2025
Simba SC 5-1 Pamba Jiji | Highlights | NBC Premier League 08/05/2025

Jean Charles Ahoua amepiga hattrick Simba ikiinyuka Pamba Jiji FC kichapo cha mabao 5-1 kwenye Dimba la KMC Complex, Dar es Salaam. Ahoua amefunga magoli yake dakika ya 16' kwa penati, 37' na 48' huku mawili yakifungwa na Lionel Ateba Mbida dakika ya 80 na 84. Goli pekee la kufutia machozi kwa Pamba limefungwa na Mathew Momanyi Tegis dakika ya 86....



JKT Tanzania 0-1 Simba SC | Highlights | NBC Premier League 05/05/2025
JKT Tanzania 0-1 Simba SC | Highlights | NBC Premier League 05/05/2025

Fabrice Ngoma amefunga goli pekee lililowapa Simba ushindi wa 1-0 ugenini dhidi ya JKT Tanzania, mchezo wa ligi kuu ya NBC ukipigwa Meja Jenerali Isamuhyo, Mbweni Dar es Salaam.




« Previous Next »


Popular Tags

#Best Goalkeeper Saves  #Best Goals  #Michael Jordan  #Gareth Bale  #Best Goals Ever  #Paul George  #New York Knicks  #Shot Goals  #Shot Goals  #Boston Celtics  

Popular Users

#Buster_ESPN  #TheEllenShow  #JasonDufner  #RealSkipBayless  #richarddeitsch  #TimTebow  #RyanBabel  #KimKardashian  #KingJames  #dougferguson405  #instagram  #narendramodi  #BMcCarthy32  #DjokerNole