Kipa wa Kagera Sugar, Juma K Juma, alimlaumu mwamuzi Hans Mabena aliyechezesha mchezo wao dhidi ya Azam FC akisema refa huyo alikuwa anawaadhibu wao kwa kufanya madhambi ambayo hata Azam FC waliyafanya lakini akawaacha. Video hii inakuletea rafu zote ambazo Kagera Sugar walizifanya siku hiyo. Walifanya faulo zaidi ya 20 huku wakioneshwa kadi za njano mbili tu
Danny Usengimana alimvamia golikipa wa Kagera Sugar, Juma Kaseja, na kumchezea madhambi.
Kipa wa Kagera Sugar, Juma K Juma, alimlaumu mwamuzi Hans Mabena aliyechezesha mchezo wao dhidi ya Azam FC akisema refa huyo alikuwa anawaadhibu wao kwa kufanya madhambi ambayo hata Azam FC waliyafanya lakini akawaacha. Video hii inakuletea rafu zote ambazo Azam FC walizifanya siku hiyo. Walifanya faulo zaidi ya 13 huku wakioneshwa kadi moja tu ya njano.
Nahodha wa zamani wa Azam FC, John Bocco akiongozana na wenzake wawili waliohama Azam FC na kujiunga na Simba, Aishi Manula na Erasto Nyoni(Shomary Kapombe hakucheza) wakirejerea Chamazini kwa mara ya kwanza baada ya kuondoka mwishoni mwa msimu wa 2016/17. Kocha wao, Joseph Marus Omog pia alikuwepo Azam FC
Baada ya kuanza kuanza vibaya ligi kuu licha ya usajili wa kushtua, timu ya Singida United, ilipata ushindi wake wa kwanza wa ligi kuu dhidi ya Mbao FC ya Mwanza. Mchezo huu ulifanyika kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma kwa sababu uwanja wao wa Namfua mjini Singida ulikuwa bado kwenye matengenezo