VIDEO : TAZAMA KOSAKOSA ZA MAGOLI SIMBA VS AL AHLY,GOLI LA AL AHLY LIMESABABISHWA HIVI by @Dream Online Tv - Post Details

VIDEO : TAZAMA KOSAKOSA ZA MAGOLI SIMBA VS AL AHLY,GOLI LA AL AHLY LIMESABABISHWA HIVI

Mechi tamu ambayo timu zimeonyesha ubora mpaka filimbi ya mwisho, huwezi kujutia kwanini ulichelewa kulala kama umeshuhudia mechi hii katika dakika zote. Ilikuwa iko wazi kabisa kuwa ni mechi ambayo Ahly alihitaji alama 3 ili kufuta uteja baada ya kupoteza mechi mbili mfululizo mbele ya Simba. Kuna kitu Gomes amekipandikiza katika fikra za wachezaji wa Simba nako ni kujua kuwa jukumu la kuzuia si la watu fulani wachache ndani ya timu. Wakati ambao Simba haina mpira unaona wachezaji wote wanafanya mikimbio ya haraka kuhakikisha kuwa wanakuwa nyuma ya Mpira. Hiki si kitu ambacho tulikuwa tukikiona huko nyuma, kwanza timu haikuwa na nidhamu hasa wanapoupoteza mpira. Wachezaji wanajigawa mafungu mawili, kuna wale ambao wanazuia na wengine wanaamini kukaba si sehemu ya majukumu yao. Leo Simba ilicheza kwa tahadhari kubwa hasa wakati ambao Ahly wanamiliki mpira, kwanza hawakukubali kuvunja umbo lao na walikubali kuwa wadogo mbele ya mpinzani. Mbele alibaki Meddie Kagere ili kusubiri mashambulizi ya haraka pale ambapo Simba itafanikiwa kuunasa Mpira. Kwa bahati mbaya tu ni kuwa mashambulizi mengi ya Simba yalizuia na Ahly baada ya kuwa compact sana katika eneo lao. Ahly ilishajua kuwa Simba ina wachezaji wawili ambao ni hatari hasa katika eneo la mbele. Kongole kwa Pitso kwa sababu mabadiliko makubwa ya kikosi aliyoyafanya yaliendana na mahitaji ya mchezo wa leo. Ahly ilifanikiwa kuua movement nyingi za Simba kwa kuzuia wachezaji wanaohusika na build up nyingi za Simba. Kwanza ni Luis, wakahakikisha kuwa hawi na madhara kwa kumnyima uhuru wa kufanya mikimbio kutokea pembeni . Wa pili ni Chama, kila aliposhika Mpira kuna wachezaji wawili walimzonga ili kuhakikisha haoni ni wapi aipeleke pasi yake ya kwanza . Kikubwa zaidi wachezaji wa Simba wanajiamini sana wakiwa na mpira, timu nyingi za Tanzania zinapokuwa ugenini huoni wakipiga pasi na kufika katika eneo la mpinzani. Heko kwa Simba, kuna muda waliiweka Ahly katika nyakati ngumu na kama wangeongeza umakini pengine wangeondoka na sare kama sio kushinda mechi kabisa. Ni nafasi moja pekee ambayo imeamua matokeo, mbali na goli hakika Ahly walipewa mechi nzuri na waliulizwa maswali magumu pia.

Similar Posts!

KOCHA WA ZAMANI SIMBA AFUNGUKA SABABU YA DODOMA JIJI KUFUNGWA NA SIMBA 2-0 KWA MKAPA
KOCHA WA ZAMANI SIMBA AFUNGUKA SABABU YA DODOMA JIJI KUFUNGWA NA SIMBA 2-0 KWA MKAPA

FT: Simba 2-0 Dodoma Jijj 🔊 Alama tatu muhimu kwa Simba, Dodoma Jiji wamepoteza mechi ambayo naona walicheza vizuri, walikuwa na nidhamu nzuri ya kuzuia kwa bahati mbaya kosa moja kubwa likawafanya waikabidhi mechi mikononi mwa Simba. 🔊 Dodoma Jiji hawakuwaruhusu Simba kupiga penetration passes, walizuia half spaces na kuwafanya wacheze nje ya eneo la hatari muda mwingi, katika system ya low blocks defensive hukuona Simba wanatengenezaje nafasi kabla ya kosa la penati kutokea. 🔊 Ipo sehemu ya Simba kujitazama mara mbili, mara nyingi wanapokutana na timu za aina hii wanajenga mashambulizi yao taratibu hiyo inawasaidia wapinzani kujipanga kwa sababu presha inakuwa ni ndogo kwenye eneo lao. 🔊 Zipo nyakati ambazo Dodoma Jiji wangekuwa wakatili mbele ya lango la Simba pengine wangeifanya mechi kuwa ngumu zaidi, ni rahisi kukishinda kiungo cha Simba kama utaamua kuwa press na kufanya mikimbio nyuma ya safu hiyo. 🔊 Viungo wa Simba wanapitika kirahisi timu isipokuwa na mpira, tofauti ilikuwa ndogo tu, Dodoma Jiji hawakuwa na ubora katika kufanya matendo ya mwisho ya kutengeneza nafasi na kufunga magoli na hii inaficha udhaifu wa wapinzani ulioonekana



ONA ALICHOKISEMA SHABIKI WA SIMBA ANAEMKUBALI FISTON MAYELE BAADA YA SIMBA KUWAFUNGA DODOMA JIJI
ONA ALICHOKISEMA SHABIKI WA SIMBA ANAEMKUBALI FISTON MAYELE BAADA YA SIMBA KUWAFUNGA DODOMA JIJI

✍Simba SC hawakuwa katika ubora ambao wenyewe wangetamani lakini wamevuna alama 3 , katika mechi zote za msimu ngumu mechi zote ucheze kwa kiwango cha juu , muhimu ni kukusanya alama tatu ndio waliciofanya leo dhidi ya Dodoma FC ambao hawakuonesha madhara kwenda mbele . ✍Dodoma FC dakika kama 5 au 10 za mwanzo walianza na BACK 3 lakini wakaibadilisha haraka na kwenda 4-3-3 wakiwa na mpira na 4-4-2 bila mpira , hawakutaka kuzidiwa idadi ya wachezaji katikati ya uwanja na pembeni ya uwanja... lakini bado mara kadhaa waliacha spaces kubwa sana baina ya mstari mmoja na mwingine na mchezaji kwa mchezaji ✍Ni Simba tu wenyewe , Dodoma ni kama vile hawakuwa na mpango au maono ya kutafuta goli, walikuwa tayari kufungwa ( Dodoma was there for taking ) ...Simba hasa kipindi cha kwanza walikuwa slow sana , umakini unakosekana , walikuwa wanacheza kama wanaongoza 3 au 4 , mpira haukutembea kwa haraka kutoka sehemu moja kwenda nyingine ...viungo watatu ( Chama Nyoni Mzamiru ) + mawinga wawili ( Banda na Sakho ) wote wanacheza mbele ya Dodoma ...hakukuwa na mikimbio ya kutosha nyuma ya kiungo cha Dodoma na safu ya ulinzi ya Dodoma ( Easy to defend ) ✍Nafikiri Dodoma walicheza bila imani kwamba wanaweza kufunga au kupata chochote kitu dhidi ya Simba ,kuna muda walikuwa " Casual " sana , jinsi idadi ya mipira waliyokuwa wanapoteza kirahisi , iwe kwenye kiungo mpaka pembeni ya uwanja ( Sloppy ) nafikiri hata Wawa na Onyango wanaweza wakaangaliana na kujiuliza " Hivi leo mbona hatuna kitu cha kuzuia ? " 😀 NOTE 1: George Wawa sijui alikuwa anafikiria nini ? Alijua refa hatomuona kushika mpira kwa staili ile ? Doh 😀😀 na bado akabisha,Chama Jr alituliza akili licha ya wachezaji wa Dodoma kumfanyia " Mind game" 2: Cleophace Mkandala ..amekosa tu msaada kutoka kwa wenzake,maana ndio mchezaji pekee ambaye akiwa na mpira ndio unaona anaweza kufanya jambo. 3: Positive nyingine kwa Simba ukiacha alama 3 ni kurejea kutoka kwenye majeraha baadhi ya wachezaji 4: Peter Banda hakuacha kujaribu kutengeneza nafasi mpaka akapata assist yake kwa Kagere. Never give up 5: Dodoma inaonekana bado inasukwa ..muda unakimbia FT: Simba 2-0 Dodoma FC



UTACHEKA!! SHABIKI SIMBA ATEMA SHOMBO BAADA YA KUWAFUNGA 2-0 DODOMA JIJI KWA MKAPA
UTACHEKA!! SHABIKI SIMBA ATEMA SHOMBO BAADA YA KUWAFUNGA 2-0 DODOMA JIJI KWA MKAPA

✍Simba SC hawakuwa katika ubora ambao wenyewe wangetamani lakini wamevuna alama 3 , katika mechi zote za msimu ngumu mechi zote ucheze kwa kiwango cha juu , muhimu ni kukusanya alama tatu ndio waliciofanya leo dhidi ya Dodoma FC ambao hawakuonesha madhara kwenda mbele . ✍Dodoma FC dakika kama 5 au 10 za mwanzo walianza na BACK 3 lakini wakaibadilisha haraka na kwenda 4-3-3 wakiwa na mpira na 4-4-2 bila mpira , hawakutaka kuzidiwa idadi ya wachezaji katikati ya uwanja na pembeni ya uwanja... lakini bado mara kadhaa waliacha spaces kubwa sana baina ya mstari mmoja na mwingine na mchezaji kwa mchezaji ✍Ni Simba tu wenyewe , Dodoma ni kama vile hawakuwa na mpango au maono ya kutafuta goli, walikuwa tayari kufungwa ( Dodoma was there for taking ) ...Simba hasa kipindi cha kwanza walikuwa slow sana , umakini unakosekana , walikuwa wanacheza kama wanaongoza 3 au 4 , mpira haukutembea kwa haraka kutoka sehemu moja kwenda nyingine ...viungo watatu ( Chama Nyoni Mzamiru ) + mawinga wawili ( Banda na Sakho ) wote wanacheza mbele ya Dodoma ...hakukuwa na mikimbio ya kutosha nyuma ya kiungo cha Dodoma na safu ya ulinzi ya Dodoma ( Easy to defend ) ✍Nafikiri Dodoma walicheza bila imani kwamba wanaweza kufunga au kupata chochote kitu dhidi ya Simba ,kuna muda walikuwa " Casual " sana , jinsi idadi ya mipira waliyokuwa wanapoteza kirahisi , iwe kwenye kiungo mpaka pembeni ya uwanja ( Sloppy ) nafikiri hata Wawa na Onyango wanaweza wakaangaliana na kujiuliza " Hivi leo mbona hatuna kitu cha kuzuia ? " 😀 NOTE 1: George Wawa sijui alikuwa anafikiria nini ? Alijua refa hatomuona kushika mpira kwa staili ile ? Doh 😀😀 na bado akabisha,Chama Jr alituliza akili licha ya wachezaji wa Dodoma kumfanyia " Mind game" 2: Cleophace Mkandala ..amekosa tu msaada kutoka kwa wenzake,maana ndio mchezaji pekee ambaye akiwa na mpira ndio unaona anaweza kufanya jambo. 3: Positive nyingine kwa Simba ukiacha alama 3 ni kurejea kutoka kwenye majeraha baadhi ya wachezaji 4: Peter Banda hakuacha kujaribu kutengeneza nafasi mpaka akapata assist yake kwa Kagere. Never give up 5: Dodoma inaonekana bado inasukwa ..muda unakimbia FT: Simba 2-0 Dodoma FC