Timu ya Mwadui FC imeendeleza wimbi lake la ushindi kwenye Uwanja wake wa nyumbani wa Mwadui Complex baada ya leo kuichapa Biashara United mabao 2-1 katika mchezo wa ligi Kuu Tanzania Bara. Mwadui walianza kupata bao dakika ya 45 kwa tiki taka ya Salim Salim Aiyee na kisha Biashara kusawazisha dakika ya 51 kwa penati iliyopigwa na Wazir Rashid Jr kabla ya Salim Aiyee kufunga bao la ushindi dakika ya 64 akimalizia krosi ya Ditram Nchimbi. Mwadui wamefikisha pointi 33 baada ya kuchezo mechi 28 na kukaa katika nafasi ya nane huku Biashara wakisalia katika nafasi yake ya 19 na pointi 23 katika michezo 26 waliyocheza.
Simba SC imekabwa koo na kulazimishwa suluhu na Mogadishu City Club ya Somalia, katika mchezo wake wa kwanza wa Kombe la Kagame 2026, ukipigwa kwenye Dimba la Kigali, Rwanga. Kwenye mchezo huu Simba imewatumia baadhi ay nyota wake wapya akiwemo Ibrahim Doumbia , Cooper, Kelvin Nashon na wengine. Tazama highlights.
KAMWE AKWEPA KUMZUNGUMZIA AZIZ KI: Meneja Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe anasema hakuna timu Afrika ambayo haipendi kuwa na mchezaji mwenye daraja la Stephane Aziz Ki, japo amekwepa kuzungumzia kwa undani tetesi zinazomhusisha kurejea mitaa ya Jangwani. Kamwe pia amesema kuna mchezaji walimpandisha thamani makusudi ili watu walipe hela nyingi. Kamwe amesema hayo leo kwenye mahojiano maalumu kupitia kipndi cha U-LIVE cha @ufmradiotz #YangaSC #Kamwe #UFM #ULIVE
Simba SC imenyakua Kombe la Shirikisho la CRDB Bank kwa kuichapa Azam FC bao 1-0 katika mchezo wa fainali uliopigwa kwenye Dimba la Gombani Pemba. Goli pekee la ubingwa limefungwa Yahya Zayd ambaye amejifunga dakika ya 62.
Yanga SC imehitimisha msimu wa Ligi Kuuya NBC 2025/26 kwa kishindo, ikiichapa JKT Tanzania mabao 3-0 kwenye Dimba la Meja Jenerali Isamuhyo na kutwaa ubingwa wa tano mfululizo. Magoli yamefungwa na Prince Dube, Maxi Nzengeli na Laurindo Dilson Maria Depu.
Allan Okello 'Star Boy', amepiga magoli yote matatu #Hattrick , Yanga ikishinda 3-0 dhidi ya TRA United, mchezo wa raundi ya 29, Ligi Kuu ya NBC, uliopigwa KMC Complex, Dar es Salaam. Haya hapa magoli yote.
Yanga SC imezidi kuusogelea ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu, kwa kuwachapa Azam FC mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Amaan Zanzibar. Magoli ya Yanga yamefungwa na Ibrahim Abdullah 'Bacca', Laurindo Dilson Depu, na Pacome Zouzoua. Hii ni Ligi Kuu ya NBC, raundi ya 28 (bado mbili tu) Tazama highlights
Yanga SC imezidi kuusogelea ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu, kwa kuwachapa Azam FC mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Amaan Zanzibar. Magoli ya Yanga yamefungwa na Ibrahim Abdullah 'Bacca', Laurindo Dilson Depu, na Pacome Zouzoua. Haya hapa magoli yote...