SIMBA SC 2-0 NDANDA SC; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 19/05/2019) by @Azam TV - Post Details

SIMBA SC 2-0 NDANDA SC; HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 19/05/2019)

Simba SC imebakiza pointi mbili katika michezo mitatu iliyosalia kutetea taji lake la Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya leo kuichapa Ndanda SC kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam na kufikisha pointi 88 kileleni mwa msimamo wa ligi. Mabingwa hao watetezi wamepata ushindi wa mabao 2-0 yote yakifungwa na Meddie Kagere ndani ya dakika kumi, akianza dakika ya 6 kwa pasi ya John Bocco, kisha dakika ya 11 kwa pasi ya Clatous Chama. Mabao hayo yamemfanya Kagere kufikisha jumla ya magoli 22 kwenye ligi kuu msimu huu, akimuacha kwa mbali mshambuliaji wa Yanga Heritier Makambo na mshambuliaji wa Mwadui FC Salim Aiyee wenye magoli 16 kila mmoja, huku Emmanuel Okwi na John Bocco wa Simba pia wakiwa nyuma yao na mabao 15 kila mmoja. Baada ya mchezo wa leo, Simba inasafiri kwenda mjini Singida ambako itacheza na Singida United Jumanne ya Mei 21, 2019, na endapo watapata ushindi basi shughuli itakuwa imekwisha msimu huu kwani watakuwa wamefikisha pointi 91 ambazo hazitaweza kufikiwa na timu yoyote. Kwa upande wao Ndanda SC wameendelea kubaki kwenye nafasi yao ya nane wakiwa na pointi 47 na wamekiza mechi mbili ambzo zote watacheza nyumbani kwao Mtwara.

Similar Posts!

Simba SC 4-0 Coastal Union | Highlights | Nusu Fainali CRDB Bank Fed, Cup 20/06/2026
Simba SC 4-0 Coastal Union | Highlights | Nusu Fainali CRDB Bank Fed, Cup 20/06/2026

Mnyama Simba ametinga fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank kwa kuichapa Coastal Union mabao 4-0 katika mchezo mchezo wa nusu fainali uliopigwa kwenye Dimba la Sheikh Amri Abeid, Arusha. Magoli ya mchezo huu yamefungwa na Libase Gueye, Nickson Kibabage, Rushine de Reuck kwa penati na Clatous Chama.



Mbeya City 0-1 Simba SC | Highlights | NBC Premier League - 17/06/2026
Mbeya City 0-1 Simba SC | Highlights | NBC Premier League - 17/06/2026

Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo kati ya Simba SC dhidi ya Mbeya City ambapo Elie Mpanzu ndio amepeleka alama tatu unyamani. Simba imeshinda kwa goli 1-0 ndani ya dimba la Sokoine jijini Mbeya



Simba SC 2-1 Pamba Jiji | Highlights | NBC Premier League - 14/06/2026
Simba SC 2-1 Pamba Jiji | Highlights | NBC Premier League - 14/06/2026

#NBCPL: Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mechi ya NBC Premier League kati ya Simba SC dhidi ya Pamba Jiji FT: Simba SC 2-1 Pamba Jiji Magoli ya Simba yamefungwa na Elie Mpanzu na Libasse Gueye huku goli la Pamba Jiji likifungwa na Mathew Momanyi. #NBCPL #NBCPremierLeague #LigiKuuTanzania #ImenogaZaidi #SimbaVsPambaJiji #SimbaSC #PambaJiji #SimbaPamba



Mashujaa 0-2 Yanga | Highlights | NBC Premier League - 13/06/2026
Mashujaa 0-2 Yanga | Highlights | NBC Premier League - 13/06/2026

#NBCPL: Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo wa NBC Premier League kati ya Yanga SC ikiwa ugenini dhidi ya Mashujaa FC. Mechi imepigwa katika dimba la Lake Tanganyika Kigoma. Magoli yamefungwa na Mudathir Yahya na Bakari Mwamnyeto FT: Mashujaa 0-2 Yanga #NBCPL #NBCPremierLeague #LigiKuuTanzania #ImenogaZaidi #MashujaaVsYanga #Mashujaa #YangaSC #MSHYNG



Magoli | Fountain Gate 0-2 Azam FC | NBC Premier League 12/06/2026
Magoli | Fountain Gate 0-2 Azam FC | NBC Premier League 12/06/2026

Jean Jaques Ngita na Jephte Kitambala Bola wameipa Azam FC magoli mawili muhimu ugenini wakiondoka na ushindi wa mabao 2-0 kwenye Dimba la Sheikh Amri Abeid, Arusha dhidi ya Fountain Gate FC. Haya hapa magoli yote mawili...



Yanga SC 1-1 Simba SC | Highlights | U17 Clubs Premier League 06/06/2026
Yanga SC 1-1 Simba SC | Highlights | U17 Clubs Premier League 06/06/2026

LIGI YA VIJANA U17 | Ni Kariakoo Derby ya vijana, Yanga U17 na Simba U17, mchezo umemalizika kwa sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa TFF, Kigamboni Dar es Salaam. Yanga wametangulia kwa goli la Issa Ramadhan dakika ya 15, na Simba kuchomoa dakika za majeruhi... Tazama highlights



Yanga SC 3-1 Namungo FC | Highlights | NBC Premier League 25/05/2026
Yanga SC 3-1 Namungo FC | Highlights | NBC Premier League 25/05/2026

Kiungo Allan Okello amefunga magoli mawili katika ushindi wa 3-1, Yanga dhidi ya Namungo FC, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa KMC Complex, Dar es Salaam. Aliyeitanguliza Yanga kwenye mchezo huu alikuwa ni Duke Abuya, kabla ya Hassan Kabunda kuchomoa kipindi cha kwanza... na Allan Okello akapiga mawili kipindi cha pili.



Magoli | Okello apiga mawili, Yanga ikiichapa 3-1 Namungo FC | NBC Premier League 25/05/2026
Magoli | Okello apiga mawili, Yanga ikiichapa 3-1 Namungo FC | NBC Premier League 25/05/2026

Kiungo Allan Okello amefunga magoli mawili katika ushindi wa 3-1, Yanga dhidi ya Namungo FC, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa KMC Complex, Dar es Salaam. Aliyeitanguliza Yanga kwenye mchezo huu alikuwa ni Duke Abuya, kabla ya Hassan Kabunda kuchomoa kipindi cha kwanza... na Allan Okello akapiga mawili kipindi cha pili. Haya hapa magoli...