Kwanini penati ya Simba dhidi ya African Lyon haikuwa halali - KIPYENGA CHA MWISHO 28/02/2019 by @Azam TV - Post Details

Kwanini penati ya Simba dhidi ya African Lyon haikuwa halali - KIPYENGA CHA MWISHO 28/02/2019

Kipindi hiki cha Februari 28, kimechambua matukio kadhaa yenye utata katika mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara, likiwemo lile la Simba kupewa penati katika mchezo wao dhidi ya African Lyon uliopigwa Februari 19 mwaka huu kwenye Dimba la Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha. Tazama ni kwanini kipindi hiki kimesema kuwa penati ile haikuwa halali. Matukio mengine ni ya off-side, ambapo katika wiki hiyo mhanga mkubwa amekuwa ni Stand United aliyenyimwa magoli mawili halali kwenye mchezo wake na Mbeya City uliopigwa kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya kwa kigezo cha off-side. Matukio mengine ni kwenye mchezo kati ya Azam FC dhidi ya Simba, Lipuli FC dhidi ya Azam FC, pamoja na mchzo wa Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC) kati ya KMC na Mtibwa Sugar ambapo kuna penati ilirudiwa. Tupo na waamuzi wastaafu Osman Kazi na Manyama Bwire. #KipyengaChaMwisho ni kila Alhamisi saa 3:30 usiku #AzamSports2

Similar Posts!

USIKU WA VITASA | Karim Mandoga Vs Mada Maugo (TKO) - 11/04/2024
USIKU WA VITASA | Karim Mandoga Vs Mada Maugo (TKO) - 11/04/2024

Kwa TKO raundi ya sita, Mada Maugo amemkalisha Karim Mandonga.



Mashujaa FC 1-1 (6-5) Simba SC | Penati | CRDB Bank Federation Cup - 09/04/2024
Mashujaa FC 1-1 (6-5) Simba SC | Penati | CRDB Bank Federation Cup - 09/04/2024

Tazama mikwaju yote ya penati iliyopigwa kwenye mchezo CRDB Bank Federation Cup kati ya Mashujaa FC dhidi ya Simba SC. Simba imetolewa kwa jumla ya penati 6-5 Waliopiga kwa upande wa Simba ni Mohamed Hussein, Israel Mwenda, Freddy Michael Koublan, Willy Onana, Mzamiru Yassin, Ladack Chasambi, Sadio Kanoute Waliopiga kwa upande wa Mashujaa ni Zuberi Dabi, Samson Madeleke, Masinda, Idrissa Stambuli, Adam Adam, Mpoki Mwakinyuke, Baraka Mtui



Yanga kupeleka malalamiko CAF yaliyojiri mechi yao na Mamelodi Sundowns
Yanga kupeleka malalamiko CAF yaliyojiri mechi yao na Mamelodi Sundowns

“Kama klabu lazima tuoneshe kwamba kuna namna ambavyo hatujaridhishwa na kile ambacho kimetokea katika mchezo ule” sehemu ya maneno ya Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe akizungumzia hatua ambazo timu hiyo imepanga kuzichukua juu ya yale yaliyojiri katika dimba la Loftus kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Mamelodi Sundowns.



MSHIKESMSHIKE VIWANJANI - 03/04/2024
MSHIKESMSHIKE VIWANJANI - 03/04/2024

Tazama taarifa mbalimbali za maandalizi ya Simba na Yanga SC kuelekea mechi zao za marudiano za robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika Afrika.



MSHIKEMSHIKE VIWANJANI 01/04/2024
MSHIKEMSHIKE VIWANJANI 01/04/2024

Tazama kipindi cha Mshikemshike Viwanjani ambacho kimekusanya habari mbalimbali ikiwemo taarifa ya Rais wa Yanga, Hersi Said akizungumzia mchakato wa mabadiliko ya klabu hiyo. Mashabiki wa Yanga wameanza safari ya kwenda Mamelodi



Azam FC 2 -1 Yanga SC | Highlights | NBC Premier League 17/03/2024
Azam FC 2 -1 Yanga SC | Highlights | NBC Premier League 17/03/2024

DAR DERBY: Yanga SC imeangukia pua kwa kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Azam FC, katika #DarDerby iliyopigwa leo Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Yanga imetangulia kupata bao kupitia kwa Clement Mzize dakika ya 10 kabla ya Azam kuchomoa dakika ya 19 kwa goli la Gibril Sillah na kisha Feisal Salum akafunga la ushindi dakika ya 51.



Magoli | Azam FC 2-1 Yanga SC | NBC Premier League 17/03/2024
Magoli | Azam FC 2-1 Yanga SC | NBC Premier League 17/03/2024

DAR DERBY: Yanga SC imeangukia pua kwa kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Azam FC, katika #DarDerby iliyopigwa leo Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Yanga imetangulia kupata bao kupitia kwa Clement Mzize dakika ya 10 kabla ya Azam kuchomoa dakika ya 19 kwa goli la Gibril Sillah na kisha Feisal Salum akafunga la ushindi dakika ya 51.



Simba 2-0 Mashujaa | Highlights | NBC Premier League 15/03/2024
Simba 2-0 Mashujaa | Highlights | NBC Premier League 15/03/2024

Clatous Chama amefunga magoli mawili muhimu dakika ya 57 na 73, Simba ikipata ushindi wa 2-0 dhidi ya Mashujaa FC, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa #AzamComplex, Chamazi .