Content removal request!


Kwanini penati ya Simba dhidi ya African Lyon haikuwa halali - KIPYENGA CHA MWISHO 28/02/2019

Kipindi hiki cha Februari 28, kimechambua matukio kadhaa yenye utata katika mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara, likiwemo lile la Simba kupewa penati katika mchezo wao dhidi ya African Lyon uliopigwa Februari 19 mwaka huu kwenye Dimba la Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha. Tazama ni kwanini kipindi hiki kimesema kuwa penati ile haikuwa halali. Matukio mengine ni ya off-side, ambapo katika wiki hiyo mhanga mkubwa amekuwa ni Stand United aliyenyimwa magoli mawili halali kwenye mchezo wake na Mbeya City uliopigwa kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya kwa kigezo cha off-side. Matukio mengine ni kwenye mchezo kati ya Azam FC dhidi ya Simba, Lipuli FC dhidi ya Azam FC, pamoja na mchzo wa Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC) kati ya KMC na Mtibwa Sugar ambapo kuna penati ilirudiwa. Tupo na waamuzi wastaafu Osman Kazi na Manyama Bwire. #KipyengaChaMwisho ni kila Alhamisi saa 3:30 usiku #AzamSports2