Meneja wa timu ya Simba Abbas Ally amewataka wapenzi na mashabiki wa timu hiyo kutulia na kujiandaa na furaha katika mechi zijazo baada ya kufanya vibaya katika mechi mbili mfululizo. Abbas ametoa kauli hiyo mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati yao na Mbao FC uliomalizika kwa Simba kufungwa bao 1-0 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza leo Septemba 20, 2018. Amesema ligi siyo mashindano ya mtoano bali ina mechi mechi nyingi hivyo atakayemaliza vizuri ndiye atakaye kuwa bingwa, na Simba bado ina nafasi hiyo. Kuhusu mabadiliko ya Kocha wa timu hiyo kwenye safu ya ushambuliaji, Abbas amesema kocha anapanga kikosi kulingana na jinsi wachezaji walivyofanya mazoezi na mchezaji atakayeonekana kuwa vizuri zaidi ndiye anayepewa nafasi kwenye mechi. Kwa upande wake beki wa Simba ambaye pia ni nahodha msaidizi wa timu hiyo Mohamed Hussein 'Zimbwe Jr' amewataka mashabiki wa timu hiyo wasikate tamaa baada ya kufungwa na Mbao FC.
Goli pekee la Stephane Aziz ki limeipeleka Yanga fainali yake ya tano ya michuano ya #CRDBBankFederationCup ikishinda 1-0 dhidi ya Ihefu SC, mchezo wa nusu fainali uliopigwa Sheikh Amri Abeid Arusha. Yanga sasa itakutana na Azam FC katika mchezo wa fainali, Juni 02, 2024.
Goli pekee la Freddy Michael Koublan limeipa Simba pointi tatu muhimu, wakiichapa Dodoma Jiji 1-0 kwenye Dimba la Jamhuri, Dodoma. Hii ni #NBCPremierLeague
Yanga SC imeichapa Mtibwa Sugar 3-1 na kutangaza ubingwa wake wa 30 kwenye ligi kuu ya NBC Tanzania Bara ikiwa na mechi tatu mkononi baada ya kufikisha alama 71 ambazo hazifikiwi na timu nyingine. Mtibwa ndiyo waliotangulia kupata bao dakika ya 32 kupitia kwa Charles Ilanfya lakini Yanga wakachomoa dakika ya 62 kwa goli la Kennedy Musonda, Nasry Kombo akajifunga dakika ya 66 na Clement Mzize akamaliza kazi dakika ya 81. Tazama highlights...
Yanga SC imeichapa Mtibwa Sugar 3-1 na kutangaza ubingwa wake wa 30 kwenye ligi kuu ya NBC Tanzania Bara ikiwa na mechi tatu mkononi baada ya kufikisha alama 71 ambazo hazifikiwi na timu nyingine. Mtibwa ndiyo waliotangulia kupata bao dakika ya 32 kupitia kwa Charles Ilanfya lakini Yanga wakachomoa dakika ya 62 kwa goli la Kennedy Musonda, Nasry Kombo akajifunga dakika ya 66 na Clement Mzize akamaliza kazi dakika ya 81. Haya hapa magoli yote...
MZIZIMA DERBY: Simba FC imeshinda 3-0 dhidi ya Azam FC, mchezo wa ligi kuu ya NBC ukipigwa kwenye Dimba la Benjamin Mkapa Dar es Salaam. Magoli yote yamefungwa kipindi cha pili akianza Sadio Kanoute dakika ya 63, Fabrice Ngoma dakika ya 77 na David Kameta dakika ya 89. Azam FC walipata penati mapema lakini walikosa kupitia kwa Feisal Salum.... lakini pia kuna utata kuhusu tukio la Azam kupata goli iliyoamuliwa kuwa ilikuwa ni off-side.
MZIZIMA DERBY: Simba FC imeshinda 3-0 dhidi ya Azam FC, mchezo wa ligi kuu ya NBC ukipigwa kwenye Dimba la Benjamin Mkapa Dar es Salaam. Magoli yote yamefungwa kipindi cha pili akianza Sadio Kanoute dakika ya 63, Fabrice Ngoma dakika ya 77 na David Kameta dakika ya 89. Azam FC walipata penati mapema lakini walikosa kupitia kwa Feisal Salum.... lakini pia kuna utata kuhusu tukio la Azam kupata goli iliyoamuliwa kuwa ilikuwa ni off-side.
Simba SC imepata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Tabora United katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania bara uliopigwa leo kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi. Magoli ya Simba yametoka kwa Sadio Kanoute dakika ya 19 na Edwin Balua dakika ya 77.
Goli pekee kutoka kwa Joseph Guede limeipa yanga ushindi wa 1-0 dhidi ya Mashujaa FC ugenini kwenye Dimba la Lake Tanganyika Kigoma, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC. Tazama highlights....