Lipuli FC ya Iringa wameichapa Alliance kutoka Jijini Mwanza bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa leo kwenye dimba la Samora mjini Iringa. Bao pekee la Lipuli limepatikana dakika ya 6 ya mchezo kupitia kwa Miraji Athuman kwa kichwa akiitumia vizuri kros kutoka upande wa kulia. Katika mchezo huo Lipuli walitawala zaidi kipindi cha kwanza kwa mashambulizi mfululizo, lakini Kipindi cha pili alliance waliamka na kuonesha dalili za kusawazisha, lakini haikuwa hivyo. Hata hivyo dakika ya 50, Alliance walifanikiwa kutikisa nyavu za Lipuli lakini mwamuzi akaamua kuwa mfungaji alikuwa off-side na hadi mwisho wa mchezo, Alliance wakaondoka na kipigo hicho cha bao 1-0, kikiwa ni kipigo cha tatu mfululizo. Tazama highlights za mchezo.
#CRDBBankFederationCup: Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo kati ya Simba dhidi ya TRA United kwenye mchezo wa robo fainali ya CRDB Bank Federation Cup. Magoli ya Simba yamefungwa na Clatous Chama, Anicet Oura, Selemani Mwalimu na Bashiri Kibaila. Mchezo wa nusu fainali ni Coastal Union dhidi ya Simba SC. FT: Simba SC 4-0 TRA United #KombeLaShirikishoLaCRDBBank #CRDBCup #FACup #SimbaSCVsTRAUnited #SimbaSC #TRAUnited #SimbaTRAUnited
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara, Yanga SC wamepoteza mchezo kwa mara ya kwanza msimu huu, wakichapwa 3-2 na Dodoma Jiji, mchezo, mchezo ukipigwa Airtel Stadium, Singida. Magoli ya Yanga yamefungwa na Allan Okello dakika ya 2 na 41, huku magoli ya Dodoma Jiji yakitoka kwa Bakari Mwamnyeto aliyejifunga dakika ya 29, Mwana Kibuta David dakika ya 90 na Wazir Junior Shemtembo dakika za nyongeza. Haya hapa magoli yote..
#NBCPL: Tazama magoli yote matano yaliyofungwa kwenye mchezo wa NBC Premier League kati TRA United dhidi ya Azam FC. FT: TRA United 4-1 Azam FC Magoli ya TRA United yamefungwa na Ally Ng'azi, Ammy Mapaka na Ramadhan Salum 'Chobwedo' Goli la Azam FC limefungwa na Jephte Kitambala Bola. #NBCPremierLeague #LigiKuuYaNBC #NBCPL #NBCPLUpdates #ImenogaZaidi #TRAUnitedvsAzamFC #TRAUnited #AzamFC #TRAUnitedAzamFC
KARIAKOO DERBY | Imepigwa dabi moja ya maana sana kwenye Dimba la Amaan, Zanzibar, Yanga na Simba wakimaliza dakika 90 bila bao, lakini burudani za kutosha. Hii ni mechi ya Ligi Kuu ya NBC Tanzania
Yanga SC imeichakaza JKT Tanzania mabao 5-0 katika mchezo wa ligi kuu ya NBC uliopigwa leo kwenye Dimba la KMC Complex, Dar es Salaam. Wafungaji wa magoli haya ni Mohamed Hussein Zimbwe Jr,, Aurellio Depu, Mudathir Yahya, Prince Dube na Shekhan Ibrahim.
Ni mechi ya kirafiki ya kalenda ya FIFA iliyopigwa kwenye Dimba la Al Salaam, Cairo nchini Misri, na timu ya taifa ya Tanzania #TaifaStars kuchwa 4-3 na Kuwait. Magoli ya Tanzania yamefungwa na M’mombwa 6’, 87’, na Taryin Allarakhia 34’ huku ya Kuwait yakitoka kwa Daham 46’, 52’ Nasser 63’ na Hamdan 69’
KMC vs SINGIDA BS: Kocha Marcio Maximo wa KMC, amesema mataifa ya Argentina na Brazil ni wapinzani ndani ya uwanja, ...
KARIAKOO DEEBY | Fahamu ukweli kuhusu matukio yote yaliyozua utata kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii kati ya Yanga na Simba uliopigwa Septemba 16, 2025. Moja kati ya matukio yaliyozua gumzo ni goli pekee walilofunga Yanga na kuamua mshindi wa Ngao ya Jamii 2025. Osman Kazi na jopo lake wanamaliza utata kwa kutumia sheria na kanuni za soka