Meneja Habari na Mawasiliano wa Yanga SC Ally Kamwe akizungumza mipango ya kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Mabingwa wapya wa soka kutoka Safari lager,utakaochezwa Juni 29,2024 Uwanja wa Benjamin Mkapa. Pia ameeleza lengo la kuwaleta Wachezaji wao wa Zamani kuzungumza na Mabingwa hao wapya wa Soka.