Goli la kujifunga dakika za jioooooooooooooooni limewapa Namungo FC sare ya mabao 2-2 dhidi ya Simba kwenye Dimba la Majaliwa, Lindi, ukiwa ni mchezo wa Ligi Kuu ya NBC..... Simba walitangulia kwa goli la Willy Onana dakika ya 34 kabla ya Namungo kusawazisha dakika ya 39 kupitia kwa Kelvin Kongwe Sabato, na Edwin Balua kuifungia Simba la pili kwa free-kick dakika ya 70.