Simba SC imetinga hatua ya makundi Kombe la Shirikisho barani Afrika #CAFCC kwa jumla ya mabao 4-2 licha ya kufungwa 2-1 katika mchezo huu wa marudiano uliochezwa leo kwenye Dimba National Heroes, nchini Zambia. Magoli ya Red Arrows yamefungwa na Ricky Banda pamoja na Sadam Phiri huku goli la Simba likifungwa na Hassan Dilunga.